Kwa miaka elfu mbili, imani ya mwanadamu katika Bwana imekuwa imetegemezwa Biblia, na kuja kwa Bwana Yesu hakukuikanusha Biblia ya Agano la Kale. Baada ya Mwenyezi Mungu kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho, kila mtu anayemkubali Mwenyezi Mungu atalenga kula na kunywa maneno ya Mwenyezi Mungu na aitasoma Biblia mara chache tena. Kile ninachopenda kufuatilia ni, baada ya mtu kuikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, ni mtazamo gani sahihi hasa mtu anafaa kuwa nao kwa Biblia, na mtu anafaa kuitumia kwa jinsi gani? Imani ya mtu katika Mungu inafaa itegemezwe nini ili mtu aitembee njia ya imani katika Mungu na kupata wokovu wa Mungu?

08/06/2019

Jibu:

Biblia ni kumbukumbu halisi ya hatua za kwanza mbili za kazi ya Mungu. Kwa maneno mengine, ni ushuhuda wa hatua mbili za kwanza za kazi ya Mungu, ambazo zinahitimisha uongozi na ukombozi wa wanadamu baada ya kuumbwa kwa mbingu na dunia na vitu vyote, pamoja na wanadamu. Kutokana na kuisoma Biblia, kila mmoja anaweza kuona jinsi Mungu aliwaongoza wanadamu wakati wa Enzi ya Sheria na kuwafundisha kuishi mbele Zake na kumwabudu Yeye. Tunaweza kuona pia jinsi Mungu aliwakomboa wanadamu wakati wa Enzi ya Neema na kuwasamehe dhambi zao zote zilizopita huku akiwapa amani, furaha, na kila aina ya neema. Watu hawawezi tu kuona kwamba Mungu alikuwa amewaumba wanadamu, bali pia kwamba Yeye alikuwa amewaongoza kwa uthabiti na halafu akawakomboa. Wakati huo huo, Mungu amewakimu na kuwalinda wanadamu pia. Aidha, tunaweza kusoma kutoka kwa unabii wa Biblia kwamba siku za mwisho, maneno ya Mungu yatachoma kama moto ili kuwahukumu na kuwatakasa watu Wake. Yatawaokoa wanadamu kutoka kwa dhambi zote na kutusaidia kuutoroka ushawishi wa giza la Shetani ili tuweze kumrudia Mungu kabisa na hatimaye kurithi baraka na ahadi Zake. Hili ndilo alilolimaanisha Mungu aliposema, “nashuhudiwa na hayo.” Kwa hiyo, yeyote ambaye ameisoma Biblia kwa makini anaweza kuona kiasi kidogo cha matendo ya Mungu na kutambua kuweko Kwake na uweza na hekima ambayo kwayo Yeye aliumba, Anatawala, na Hudhibiti kila kitu mbinguni na duniani. Hivyo, Biblia ni yenye maana sana kwa watu katika kumwamini Mungu, kumjua Mungu na kuingia njia ya imani—njia halisi ya uzima. Yeyote ambaye anamwamini Mungu kwa unyofu na anaupenda ukweli anaweza kupata lengo na mwelekeo katika maisha kwa kuisoma Biblia, na kujifunza kumwamini, kumtegemea, kumtii, na kumwabudu Yeye. Haya yote ni matokeo ya ushuhuda wa Biblia kwa Mungu; huu ni ukweli usiokanushika.

…………

Thamani ya Biblia huwa kabisa katika kumbukumbu yake ya hatua mbili za kwanza za kazi ya Mungu. Ikiwa watu wanaweza kufafanua matamshi na matendo ya Mungu ndani yake, na wanaweza kuwa na imani na maarifa ya uweza na hekima ambayo kwayo Yeye aliumba na anatawala kila kitu, hili litakuwa na maana ya kina sana kwa watu katika kumjua Mungu, wakimfuata na kumwabudu Yeye. Kwa sababu hii, Biblia ni ushuhuda tu wa kazi ya Mungu, na inaweza kuwasaidia waumini kuujenga msingi. Naam, ni kitabu cha kuvutia sana kinachopaswa kusomwa na kila mtu ambaye anamwamini Mungu. Biblia inaweza kuwasaidia watu kufahamu na kutambua hatua mbili za kwanza za kazi ya Mungu ili kuwaokoa wanadamu, na ni yenye manufaa sana kwa ufahamu wao wa ukweli na kuingia kwao katika maisha. Hata hivyo, haiwezi kuchukua mahali pa kazi ya Mungu siku za mwisho, sembuse matamshi yake ya siku hizi; inaweza tu kutusaidia kufahamu hatua za kwanza mbili za kazi ya Mungu na kujua tabia na uweza na hekima Yake. Hii ndio njia pekee ya kuihakiki Biblia ambayo inauandama moyo wa Mungu, na Ninaamini hili lilikuwa kusudi la kawaida la kila mmoja wa waandishi na wakusanyaji habari za Biblia.

Kimetoholewa kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu

Biblia ni rekodi tu ya kazi ya Mungu, na ushuhuda kwa Mungu; ingawa ni muhimu sana kwa ajili ya kuwaadilisha wanadamu, hata hivyo haiwezi kuchukua nafasi ya kazi ya Roho Mtakatifu katika hali zozote zile. Kwa wale wetu ambao tuna imani katika Mungu, kupata wokovu lazima kuwe kwa msingi wa kazi ya Roho Mtakatifu. Kama tungefuata tu Biblia bila kazi ya Roho Mtakatifu, tungekuwa tukitembea kwenye njia yetu wenyewe. Kushindwa kwa Mafarisayo walioamini katika Mungu lakini kumpinga ni kielezo kizuri kuwa ni makosa mtu kuweka msingi wa imani kwenye Biblia tu na sio kwenye kazi ya Roho Mtakatifu. Watu wengi wameichunguza Biblia kwa miaka mingi, lakini wamekosa nuru na mwanga wa Roho Mtakatifu, na hatimaye hawajaweza kupata ufahamu wa ukweli au maarifa ya Mungu. Kwa hivyo, sisi ambao tuna imani katika Mungu lazima tuikabili na tutumie Biblia ifaavyo. Hatupaswi kuiamini wala kuiabudu Biblia bila kufikiria. Tunaweza kuona neno la Mungu katika Biblia na vilevile jinsi Mungu anavyofanya kazi Yake ya kumwokoa mwanadamu, lakini ufahamu wetu kulihusu daima utakuwa mdogo sana, hasa kuhusu neno la Mungu. Bila nuru na mwanga wa Roho Matakatifu, tunaweza kukariri neno lote la Mungu, lakini bado hatutauelewa ukweli. Hii imethibitishwa na watakatifu wengi mno katika historia ambao wamepitia kazi ya Mungu. Kuna idadi kubwa ya watu wa dini ambao wana imani pofu katika Biblia na wanaoiabudu Biblia, lakini mioyoni mwao hawamchi Mungu, na wanamwekea Mungu mipaka ndani ya mawazo na fikira zao wenyewe. Wakati ambapo Mwenyezi Mungu Mwenye mwili wa siku za mwisho anafanya kazi Yake ya hukumu na kuonyesha ukweli utakaomtakasa na kumwokoa mwanadamu, watu hawa hawaitambui sauti ya Mungu. Badala yake, wanamshutumu na kumkataa Mungu, wakimhukumu na kumkufuru Mungu ovyovyo. Wanapoona kwamba washiriki wa Kanisa la Mwenyezi Mungu wanalila na kulinywa neno la Mwenyezi Mungu katika mikusanyiko yao na tafuta maoni toka katika Biblia kumekuwa kitu cha muda wao wa ziada, wao hushutumu na kuhukumu hata zaidi. Je, wanauelewa ukweli au kumjua Mungu kwa kweli? La hasha! Wao ni waabudu Biblia wanaompinga Mungu, kama Mafarisayo. Mafarisayo walipoona kwamba wafuasi wa Bwana Yesu walifanya ushirika tu kuhusu kazi na maneno ya Bwana Yesu katika mikusanyiko yao, Mafarisayo waliwahukumu, wakisema kwamba hawayakusoma Maandiko, bali maneno ya Bwana Yesu pekee. Hii ni sawa na jinsi ambavyo wachungaji na wazee wa kanisa wa kisasa husema; wote wanaishutumu kazi ya Mungu bila kujua ina maana gani kumfuata Mungu au ina maana gani kupitia kazi ya Mungu. Na wanachoweza tu kufanya ni kuifafanua Biblia, kufanya sherehe za dini, na kufuata kanuni za dini. Ikiwa, wakati wa Enzi ya Neema, waumini katika Bwana wangesoma tu Agano la Kale walipokusanyika, je, wangeweza kuwa na kibali cha Bwana Yesu? Sasa Bwana Yesu amerejea, Ameonyesha ukweli, na Anafanya kazi ya hukumu ya siku za mwisho. Je, tunaweza kutelekeza maneno na kazi ya Mungu ya siku za mwisho huku tukishikilia kaida za dini na sheria za Biblia? Je, inamaanisha nini hasa kumwamini Mungu? Ikiwa muumini hali, hanywi, na kupitia neno la sasa la Mungu, je, hii ni imani katika Mungu kweli? Watu wengi wa kidini hawana hata maarifa ya msingi na ukweli kuhusu imani katika Mungu. Wanahisi kwamba Biblia ni neno la Mungu tu na kwamba kizazi baada ya kizazi lazima kifuate Biblia milele, na kwamba kuifuata Biblia ni sawa na imani katika Mungu. Je, hiyo inakubaliana na ukweli wa imani katika Mungu? Kazi ya Mungu daima inasonga mbele na kukua, na hata katika Enzi ya Milenia, bado Mungu atalitumia neno Lake kuwaongoza wanadamu wote. Mungu hafuati kanuni—Mungu ni mpya daima na si mzee kamwe, na maneno na kazi Yake huendelea mbele daima, havikomi kamwe, hata hivyo wengi hushindwa kuelewa jambo hili. Je, si wao ni wa kuchekesha? Kuna wengi ambao, baada ya kuikubali kazi ya Mungu katika siku za mwisho, bado hawajui jinsi ya kuishughulikia Biblia kulingana na mapenzi ya Mungu. Ukweli kuhusu suala hili unaonyeshwa waziwazi na Mwenyezi Mungu, basi hebu tusome vifungu vichache vya neno Lake.

Mwenyezi Mungu anasema, “Leo, Ninaichambua Biblia kwa namna hii na haimaanishi kwamba Naichukia, au kukana thamani yake kwa ajili ya marejeleo. Ninakuelezea na kukufafanulia thamani ya asili na chanzo cha Biblia ili uweze kuondoka katika giza. Maana watu wana mitazamo mingi kuhusu Biblia, na mingi yao ina makosa; kusoma Biblia kwa namna hii sio tu kunawazuia kupata kile wanachopaswa kupata, lakini, muhimu zaidi, kunazuia kazi Niliyokusudia kufanya. Inaingilia kati kazi ya siku zijazo kwa kiasi kikubwa, na inatoa hasara tu, na wala sio faida. Hivyo, Ninachokufundisha ni hulka tu na kisa cha ndani cha Biblia. Sikwambii kwamba usisome Biblia, au uzunguke ukitangaza kwamba haina thamani kabisa, bali kwamba uweze kuwa na maarifa na mtazamo sahihi juu ya Biblia. Usiegemee upande mmoja sana! Ingawa Biblia ni kitabu cha historia kilichoandikwa na wanadamu, pia kinaandika kanuni nyingi ambazo kwazo watakatifu wa zamani na manabii walimhudumia Mungu, vilevile uzoefu wa hivi karibuni wa mitume katika kumhudumia Mungu—yote haya yalishuhudiwa na kujulikana kwa watu hawa, na inaweza kutumika kama rejeleo kwa ajili ya watu wa enzi hii katika kutafuta njia ya kweli(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuhusu Biblia (4)).

Biblia imekuwa sehemu ya historia ya binadamu kwa miaka mingi. Zaidi ya hayo, watu huichukulia kuwa Mungu, kufikia kiwango ambapo katika siku za mwisho, imechukua nafasi ya Mungu, jambo ambalo linamchukiza Mungu. Hivyo, muda uliporuhusu, Mungu alihisi kulazimishwa kubainisha maelezo ya ndani na vyanzo vya Biblia; Asingefanya hivi, Biblia ingeendelea kushikilia nafasi ya Mungu mioyoni mwa watu, na watu wangetumia maneno ya Biblia kupima na kushutumu matendo ya Mungu. Kwa kuelezea asili, muundo na dosari za Biblia, Mungu hakuwa akikana kuwepo kwa Biblia hata kidogo, wala Hakuwa anaishutumu; badala yake, Alikuwa akitoa maelezo yaliyofaa na kustahili yaliyorejesha picha asilia ya Biblia, Akazungumzia suitafahamu za watu kuhusu Biblia, na kuwapa maoni sahihi ya Biblia, ili wasiiabudu Biblia tena, na wasipotee tena; yaani, ili wasichanganye tena imani yao pofu ya Biblia kuwa imani katika Mungu na ibada ya Mungu, wakihofia hata kukabili usuli na dosari zake za kweli. Mara tu watu wanapopata ufahamu wa Biblia usiochanganywa na mambo duni, wanaweza kuiweka kando bila majuto na kuyakubali maneno mapya ya Mungu kwa ujasiri. Hili ndilo lengo la Mungu katika sura hizi kadhaa. Ukweli ambao Mungu angetaka kuwaambia watu hapa ni kwamba hakuna nadharia ama ukweli ambao unaweza kuchukua nafasi ya kazi na maneno ya Mungu ya leo, na kwamba hakuna kitu kinachoweza kuwa mbadala wa Mungu. Ikiwa watu hawawezi kuepuka mtego wa Biblia, hawatawahi kuweza kuja mbele za Mungu. Ikiwa wanataka kuja mbele za Mungu, lazima kwanza waitakase mioyo yao na kuondoa chochote kinachoweza kuchukua nafasi Yake; kisha watamridhisha Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Kristo Alipokuwa Akitembea Makanisani, Utangulizi).

Ikiwa unatamani kutembea katika njia ya leo, basi mnapaswa kutengana na Biblia, unapaswa kwenda mbele zaidi ya vitabu vya unabii au historia ya Biblia. Baada ya hapo tu ndipo utaweza kutembea njia mpya vizuri, na baada ya hapo ndipo utaweza kuingia katika ufalme mpya na kazi mpya. Unapaswa kuelewa ni kwa nini leo unaambiwa usisome Biblia, kwa nini kuna kazi nyingine ambayo inajitenga na Biblia, kwa nini Mungu haonekani mpya na wa kina zaidi katika Biblia, kwa nini badala yake kuna kazi kubwa zaidi nje ya Biblia. Haya ndiyo yote mnayopaswa kuelewa. Unapaswa kuelewa tofauti kati ya kazi ya zamani na kazi mpya, na hata kama hausomi Biblia, unapaswa kuitenganisha; kama hautaweza, bado utakuwa unaiabudu Biblia, na itakuwa ni vigumu sana kwako kuingia katika kazi mpya na kupitia mabadiliko mapya. Kwa kuwa kuna njia ya juu, kwa nini mjifunze hiyo ya chini, njia ya kale? Kwa kuwa kuna matamshi mapya, na kazi mpya, kwa nini uishi katikati ya rekodi za kale za kihistoria? Matamshi mapya yanaweza kukupa, ambayo yanathibitisha kwamba hii ni kazi mpya; rekodi za kale haziwezi kukushibisha, au kutosheleza mahitaji yako ya sasa, kitu ambacho kinathibitisha kwamba ni historia, na sio kazi ya hapa na sasa. Njia ya juu zaidi ni njia mpya zaidi, na kazi mpya, bila kujali njia ya zamani ni ya juu kiasi gani, bado ni historia ya kumbukumbu ya watu, na haijalishi ina thamani kiasi gani kama rejeleo, bado ni njia ya kale. Ingawa imerekodiwa katika ‘kitabu kitakatifu,’ njia ya kale ni historia; ingawa hakuna rekodi yake katika ‘kitabu kitakatifu,’ njia mpya ni ya hapa na sasa. Kwa njia hii inaweza kukuokoa, na kwa njia hii inaweza kukubadilisha, maana hii ni kazi ya Roho Mtakatifu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuhusu Biblia (1)).

Agano la Kale lilijiri baada ya Mungu kumaliza kazi Yake katika Enzi ya Sheria, na Agano Jipya Bwana Yesu alipomaliza kazi Yake ya ukombozi. Katika Miaka 2,000 iliyopita, hakuna kitu kilichochapishwa kwa kiasi kikubwa au kusomwa zaidi kuliko Biblia, na binadamu wamepokea ujenzi mkubwa mno wa maadili kutoka kwa Biblia. Kwa sababu maneno ya Mungu ambayo Alionyesha wakati wa kazi Yake yameandikwa katika Biblia, na pia hutumika kama maelezo yaliyoandikwa ya uzoefu na ushuhuda wa wale waliotumiwa na Mungu, kutoka kwayo watu wanaweza kuona kuwepo kwa Mungu, pamoja na kuonekana kwa Mungu na kazi Yake. Kutoka kwayo, wanaweza kutambua ukweli kwamba Mungu ndiye Muumba na Mtawala wa vitu vyote, na pia wanaweza kuzijua hatua mbili za kazi katika Enzi ya Sheria na Enzi ya Neema ambazo Mungu alifanya baada ya uumbaji wa wanadamu. Hii ni kweli hasa kuhusiana na rekodi ya Biblia ya Enzi ya Neema, wakati ambapo Bwana Yesu Mwenyewe alifanya kazi Yake ya ukombozi, Akawapa wanadamu neema Yake nyingi, na kuonyesha ukweli mwingi. Hii inatuwezesha kuona upendo wa kweli ambao Mungu anao kwa wanadamu, kuelewa kwamba lazima mwanadamu awe na imani katika Mungu na kumtii Mungu ili awe kwenye njia sahihi katika maisha, na kwamba wakati tu ambapo tunaupata ukweli kama uzima wetu hasa ndipo tunaweza kupokea wokovu kutoka kwa Mungu na kupata kibali cha Mungu. Haya ndiyo matokeo ambayo hatua hizi mbili za kazi ya Mungu zilifanikisha juu ya binadamu. Isingekuwa kwa ajili ya rekodi iliyotolewa na Biblia, ingekuwa vigumu sana kwa wanadamu kuielewa kazi ya awali ya Mungu. Ndiyo maana Biblia inahitajika kusomwa kwa wale kati yetu wenye imani katika Mungu. Hata hivyo, bila kujali Biblia ni ya thamani kiasi gani, hatupaswi kuiweka kwenye kiwango sawa na Mungu, na muhimu zaidi, hatupaswi kuitumia kumwakilisha Mungu au kuchukua nafasi ya kazi ya Mungu. Kwa hiyo lazima tuichukulie Biblia ifaavyo, tusiiamini kamwe bila kufikiri au kuiabudu. Zaidi ya hayo, kuhusu suala la maneno ya Mungu ni yapi na maneno ya mwanadamu ni yapi, Biblia inaonyesha waziwazi kile kilichosemwa na Mungu na kile kilichosema na mwanadamu; ni dhahiri kwa mtazamo mmoja. Hata hivyo, watu wengi hawana ufahamu kuhusu nyaraka za mitume na sehemu ambazo ni uzoefu na ushuhuda wa mwanadamu. Wengine hata wanaamini kwamba maneno yoyote yanayotokana na kutiwa nuru na Roho Mtakatifu, au maneno yoyote ambayo yanafuatana na ukweli ni maneno ya Mungu. Lakini si huo ni upuuzi? Je, mtu anaweza kulionyesha neno la Mungu? Roho Mtakatifu anapompa nuru na kumwangazia mwanadamu na mwanadamu apokee mwanga kidogo, je, inamaanisha kwamba Roho Mtakatifu anamfichulia mwanadamu maneno ya Mungu au kumtia msukumo kwa maneno hayo? Athari ya kazi ya Roho Mtakatifu iliyonuiwa ni kumfanya mwanadamu auelewe ukweli na kuingia katika uhalisi wake. Inawezekana kuwa ushuhuda wa mwanadamu kuuelewa ukweli na kuingia katika uhalisi wake ni maneno yaliyoonyeshwa na Mungu kwa kweli? Lazima tuwe na hakika kabisa kwamba hata wakati ambapo maneno ya mwanadamu yanakubaliana na ukweli, kwa kweli hayawezi kuonekana kuwa ukweli wenyewe, au maneno ya Mungu. Maneno ya mwanadamu na maneno ya Mungu hayawezi kutajwa hapohapo kwa sababu maneno ya Mungu pekee ndiyo ukweli; Maneno ya Mungu tu ndiyo yanayoweza kumkomboa na kumwokoa mwanadamu na kuwa uzima wa mwanadamu. Maneno ya mwanadamu yanaweza tu kuwakilisha uzoefu na ufahamu wake mwenyewe, nayo ni kwa ajili tu ya kumbukumbu. Yanaweza kuwa na manufaa na kuwaadilisha watu, lakini hayawezi kabisa kuchukua nafasi ya maneno ya Mungu. Maneno ya Mungu katika Biblia hayakinzani kamwe, na ukiyalinganisha maneno ya mwanadamu na maneno ya Mungu katika Biblia, inatarajiwa kwamba ukinzani fulani utatokea. Hata hivyo, hakuna ukinzani katika kazi ya Mungu au maneno katika enzi zote. Maneno ya Yehova Mungu, maneno ya Bwana Yesu yaliyoandikwa katika Biblia, na maneno ya Mwenyezi Mungu wa siku za mwisho: Chanzo cha haya yote ni kazi ya Mungu mmoja. Yote yanatokana na maneno ya Roho Mtakatifu. Huu ni ukweli ambao hakuna mtu anayeweza kukataa. Hata hivyo, mara nyingi watu wengi wa dini huyachukua maneno ya mwanadamu ndani ya Biblia na kuyalinganisha na maneno ya sasa ya Mungu. Mafarisayo walifanya hivi pia, kila mara wakitumia maneno katika Maandiko kutafiti na kuyalinganisha na maneno ya Bwana Yesu. Kwa hiyo, Mafarisayo walipata sababu kadhaa za kumkana Bwana Yesu, na hata walimkataa na kumhukumu kipumbavu, hata kumsulubisha Bwana Yesu. Kwa hiyo, tatizo ni lipi hapa? Kuna wengi leo ambao hawaelewi jambo hili waziwazi. Kazi ya Mungu haijawahi kufanywa kwa msingi wa Biblia, na zaidi ya hayo Mungu hazuiwi na Biblia. Tukimchunguza Mungu kila mara kulingana na Biblia, au kuipima kazi ya sasa ya Mungu kwa njia hiyo, basi tutashindwa mara kwa mara, na makosa yetu yatakuwa mabaya hata zaidi. Leo watu wengi wa dini hutumia maneno kutoka kwa Biblia kumchunguza Mwenyezi Mungu na kazi Yake ya siku za mwisho, hata kuinukuu Biblia nje ya muktadha ili kumhukumu na kumpinga Mwenyezi Mungu. Wao huchukua maneno kutoka katika Biblia, hasa maneno ya mwanadamu, na kuyatumia kama ubadili wa maneno ya Mungu. Zaidi ya hayo, wao huelewa vibaya maneno ya Mungu na kuyatumia vibaya maneno ya mwanadamu kuihukumu na kuipinga kazi ya Mungu katika siku za mwisho. Hivi hasa ndivyo Mafarisayo walivyofanya katika kumpinga Bwana Yesu, kwa hiyo matokeo yatakuwa gani? Watalaaniwa na Mungu kwa namna hiyo hiyo tu. Mwenyezi Mungu asema: “Ole wao wale wamsulubishao Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Waovu Hakika Wataadhibiwa). Tukiendelea kutumia mafundisho ya kibiblia kumpinga Mungu, tutafichuliwa kama wapinga Kristo na kulaaniwa na Mungu. Je, si huo ni ukweli?

Kushindwa kwa Mafarisayo hawa wa dini katika imani yao katika Mungu kunatufundisha kwamba Mungu anapofanya kazi mpya, lazima mwanadamu aangalie nje ya maandiko yaliyomo na kukubali na kutii maneno na kazi ya Mungu ya sasa. Hii ni sawa na jinsi, katika Enzi ya Sheria, mwanadamu alivyopaswa kufuata sheria na amri zilizotolewa kutoka kwa Yehova Mungu ili kupata baraka za Mungu. Katika Enzi ya Neema, Bwana Yesu alikuja kufanya kazi Yake ya ukombozi, na mwanadamu alipaswa kutoka nje ya sheria ili kukubali na kutii maneno na kazi ya Bwana Yesu ili aweze kupokea kibali Chake. Katika siku za mwisho, Mwenyezi Mungu anafanya kazi ya hukumu Akianzia nyumba ya Mungu. Ameitamatisha Enzi ya Neema na kuanzisha Enzi ya Ufalme. Kwa hiyo lazima tuikubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, na kuweka kwenye vitendo na kuyapitia maneno ya Mwenyezi Mungu ili tuweze kupata kazi ya Roho Mtakatifu, kuupata ukweli kama uzima wetu, na kuwa mtu anayemjua Mungu, anayetii na kumcha Mungu, na mtu anayepatwa na Mungu kwa njia ya wokovu Wake. Hii ndiyo njia pekee ambayo mtu anaweza kuingia katika ufalme Wake. Kutokana na hili tunaweza kuona kwamba imani yetu katika Mungu lazima iende mwendo sawa na kazi ya Mungu na ni lazima tupate kazi ya Roho Mtakatifu, kwa sababu ni wakati huo tu ndipo tutakapoweza kuuelewa ukweli, kumjua Mungu, na kuingia katika uhalisi wa kweli. Ikiwa imani yetu inategemea tu kusoma Biblia na kuyafuata maandishi ya Biblia kwa uaminifu, huenda tutaondolewa na kutelekezwa na kazi ya Mungu, jinsi Mafarisayo walivyofanya, ambao walifuata tu Maandiko lakini walimpinga Mungu, hivyo wakajiletea laana za Mungu juu yao wenyewe. Je, kuifuata Biblia ndiko msingi wa imani yetu katika Mungu? Ikiwa imani yetu katika Mungu haina kazi ya Roho Mtakatifu, basi tumepotoka kutoka kwenye njia ya kweli, na hakuna njia ya kupata wokovu wa Mungu. Kwa hiyo, imani yetu haiwezi kutegemezwa kwenye ufuataji thabiti wa Biblia; lazima tuende kwa kasi sawa na kazi ya Mungu, tuyasome maneno ya sasa ya Mungu na kuipata kazi ya Roho Mtakatifu. Huu ndio msingi wa imani katika Mungu nacho ni kipengele muhimu zaidi. Sasa tunapaswa kuwa na ubayana kuhusu jinsi sisi kama waumini tunavyopaswa kuikabili Biblia na kile ambacho imani ya mtu katika Mungu lazima itegemezwe kwacho ili aweze kupokea kibali cha Mungu katika kuitembea njia ya imani, je, sivyo?

Kimetoholewa Kutoka Katika Majibu ya Mswada wa Filamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp