Kupenya Ukungu ili Kuona Mwanga

07/11/2018

Na Xinxin, China

Mimi ni mfanyakazi wa kawaida. Mwishoni mwa Novemba, 2013, mfanyakazi mwenza aliona kwamba mke wangu na mimi tungefanya kelele nyingi sana juu ya vitu vidogo, kwamba kila siku tulikuwa na wasiwasi na huzuni, hivyo alipitisha kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku mwisho kwetu. Kutoka kwa neno la Mwenyezi Mungu, tumejifunza kwamba mbingu na dunia na vitu vyote viliumbwa na Mungu, na kwamba uhai wa mtu amekirimiwa na Mungu. Tumeelewa pia ukweli wa fumbo la mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita, fumbo la kupata mwili, hatua tatu za Mungu za kazi katika kuwaokoa wanadamu, umuhimu wa kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho, na tondoti zingine. Mke wangu na mimi tulifikiri kwamba kumpata Mungu aliyekuwa tayari amekuja kuwaokoa wanadamu wakati wa uhai wetu ilikuwa ni baraka kubwa. Tulikubali kwa furaha kazi ya Mungu katika siku za mwisho, na tukaishi maisha ya kanisa. Chini ya uongozi wa neno la Mungu, sisi wawili tulifuatilia ukweli na kujibadilisha wenyewe, na wakati wowote jambo lilipotokea na tukaanza kubishana, hatungepata tu kosa kwa kila mmoja wetu kama tulivyozoea kufanya, ila tungeakisi juu yetu na kujaribu kujijua wenyewe. Baada ya hayo, tulitenda kwa namna ambayo ilinyima mwili kulingana na mahitaji ya Mungu, na uhusiano wetu wa ndoa ukawa bora na mzuri, na mioyo yetu ikawa na amani na thabiti. Tulihisi kwamba kumwamini Mungu ni kuzuri kweli. Hata hivyo, huku tukiwa na shangwe na kufurahia kumfuata Mungu, tulipokuwa tukifurahia maisha yenye heri, tulikabiliwa na mashambulizi makali kutoka kwa familia zetu…. Wakati tu nilipokuwa nikipoteza njia yangu, ilikuwa ni neno la Mungu lililoniongoza kubaini mpango wa Shetani, na kupenya ukungu na kuingia kwenye njia angavu na sahihi kwa uzima.

Nilipokuwa nimestaafu tu mwezi wa Februari mwaka 2014, binti mkwe wangu alituletea watu wawili wazee kusafiri kwenda Sichuan kumwangalia mjukuu wetu wakati wazazi wake hawakuwa. Nilimwomba Mungu: “Mwenyezi Mungu! Binti mkwe wangu ameniomba kumwangalia mjukuu wetu wakati wazazi wake hawapo, lakini sijazoea maisha ya mahali hapo, na sio rahisi kumwamini Mungu au kusoma neno la Mungu katika mahali hapo. Natumaini Wewe utatupa suluhisho….” Muda mfupi baadaye, binti mkwe wangu alinipigia simu tena kusema kwamba angetuletea mjukuu wangu. Niliposikia habari hii nilifurahi sana, na nikahisi jinsi Mungu alivyo mwenyezi. Mungu alisikia sala yangu na akanipa suluhisho. Kabla ya siku nyingi sana kupita, binti mkwe wangu na wazazi wake walileta mjukuu wangu. Yalipokuwa yakijiri, siku moja baada ya hayo nilikuwa nikielekea kwa mkusanyiko, na nikawaambia kuwa niliamini katika Mwenyezi Mungu. Baada ya kusikia hili, binti mkwe wangu alisema bila furaha, “Baba, unawezaje kuamini katika Mwenye Mungu? Nina hakika unajua kwamba serikali hairuhusu watu kuamini katika Mwenyezi Mungu, na katika miaka ya hivi karibuni wamekuwa wakiwakamata wanaoamini katika Mwenyezi Mungu. Huwezi kuendelea kumwamini Yeye.” Nilikanusha aliyoyanena kwa kusema, “Tunapomwamini Mungu, hatufanyi hivyo kwa sababu ya upinzani kwa serikali. Sisi huhudhuria tu mikusanyiko, kusoma neno la Mungu, kufuatilia ukweli, na kufuata njia sahihi. Je, wanawezaje kutoturuhusu tuamini?” Binti mkwe wangu akasema, “Bila kujali unalolisema, na hata kama kuamini katika Mungu ndiyo njia sahihi, mradi serikali hulikataa, huwezi kumwamini Yeye!” Nikafikiria mwenyewe, “Bila kujali unalolisema, ni Mungu wa kweli ambaye ninamwamini. Hata kama serikali ya CCP hairuhusu hilo, mimi bado nitaamini.” Baadaye, binti mkwe wangu alikwenda na kumpata mke wangu na kumsihi kwamba hatupaswi kuamini katika Mungu…. Baadaye, mwanangu wa kiume aliyekuwa mbali sana huko Sichuan akanipigia simu na kusema, “Baba, nilisikia kwamba unaamini katika Mwenyezi Mungu. Hicho ni kitu ambacho CCP hupinga, hivyo huwezi kuuamini katika Yeye tena.” Niliposikia mwana wangu akisema jambo hilo, nilihisi kuwa na shida moyoni mwangu: Kuamini kwa Mungu ni sheria ya mbinguni kwangu, hivyo kwa nini nyote mnajaribu kunizuia mara kwa mara? Ni vigumu sana kuamini katika Mungu na kufuata njia sahihi! Baadaye niliomba kimoyomoyo kwa Mungu kunilinda ili nipate kupinga usumbufu wa mwanangu wa kiume na binti mkwe wangu. Baada ya kuomba, moyo wangu hatua kwa hatua ukawa mtulivu. Ingawa mwanangu wa kiume na binti mkwe wangu hawakuelewa, nilijua wazi kuwa imani yangu katika Mungu na kufuata njia sahihi hakukuwa kukosea, na kwamba singeweza kushawishiwa nao. Baada ya siku tatu, binti mkwe wangu alikuja kwa haraka nyumbani, na nikaona kwamba alikuwa na marundo mawili ya kitu kilichochapishwa mikononi mwake. Akanisihi kuiangalia haraka, na wakati nilipoangalia nikaona kwamba vilikuwa vimejazwa na uvumi na uongo wa serikali ya CCP ikikashifu, kushutumu, na kuliharibia jina Kanisa la Mwenyezi Mungu. Kwa muda kidogo nilihisi mchafuko ndani ya moyo wangu, na nikafikiri: Haiwezekani, nimekuwa nikihudhuria mikutano kwa miezi kadhaa na sijawahi kuona ndugu wowote wa kiume au wa kike waliopoteza mikono au miguu! Kwa nini serikali ya CCP inataka kueneza uvumi na kashfa kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu? Nini kweli kinachoendelea hapa? Jioni siku hiyo, sikuweza kulala kwa sababu niliendelea kufikiri jambo hili katika akili yangu. “Ole wangu! Serikali ya CCP pia inawatesa waumini wa Mungu kwa hasira sana, na mwanangu na binti mkwe wanajaribu kwa nguvu sana kunizuia, na, hivyo nifanye nini?”

Siku iliyofuata, nilienda nje kutembea katika kitongoji, na pia niliona uvumi huu ukikashifu na kulilaani Kanisa la Mwenyezi Mungu kama umetundikwa kwenye ubao wa matangazo. Nilifikiri: Ninachokiamini ni katika Mungu wa kweli, hivyo kwa nini serikali ya CCP hupinga suala hilo kwa njia hii? Inaonekana kuwa katika nchi ya kumkana Mungu inayodhibitiwa na CCP, kuamini katika Mungu kweli silo jambo rahisi! … Wakati nilipofikiria hili, nilihisi udhaifu katika moyo wangu, na nikarudi nyumbani mwenye huzuni na kuvunjika moyo. Nilipofika tu nyumbani, binti mkwe wangu aliniambia tena, “Baba, ninakuomba uiache imani yako. Serikali ikigundua kuwa unamwamini Mungu, sitaweza kuihifadhi kazi yangu, na mwanao wa kiume ambaye hivi karibuni atapata shahada ya udaktari hataweza hata kupata kazi. Hata mjukuu wenu mdogo huenda akafyonzwa katika hili, na inawezekana kwamba katika siku za baadaye hataweza kuhudhuria shule.” Niliposikia haya, nilifikiri lilikuwa ni baa. Kuamini katika Mungu kunaweza pia kuhusisha mustakabali wa watoto wa mtu! Nikawa na hofu zaidi na zaidi, na nilijua kwamba njia za serikali ya CCP za kufundisha nidhamu na kuwaadhibu watu ni ya ukatili mno, ya kikatili sana kiasi kwamba unaweza kusema kwamba “wao huwaua watu bila kushangaa hata kidogo.” Pia nilifikiri haingekuwa si rahisi kwangu kumfanya mwanangu wa kiume kuhitimu kwa shahada yake ya udaktari, na sasa nitafanya nini ikiwa kumwamini Mungu hata humhusisha mwanangu? Ni bora hata kulisahau. Thamani ambayo ningelipa kwa kumwamini Mungu na kufuata njia sahihi ni ya juu sana. Kisha, binti mkwe wangu alinitisha, akisema, “Baba yangu alisema kwamba ikiwa utaendelea kuamini, atawapasha polisi habari. Unajua kwamba baba yangu ni katibu wa chama, na amepeana zaidi ya miaka thelathini ya maisha yake kwao. Yeye husikia na kutii chochote ambacho CCP hutaka. Yeye ni mwaminifu kwa ahadi yake, na hili siyo kujaribu kukushtua tu.” Kisha kinga katika moyo wangu zikaporomoka kabisa na kutikisika, na nikahisi kuwa ni vigumu sana kuamini katika Mungu, kwamba shinikizo lilikuwa kubwa mno. Mwana wangu na binti mkwe wangu wakinishambulia jinsi hii, kama kweli walitaka kutoa taarifa yangu kwa serikali ya CCP ili nikamatwe na kufungwa, mtu mzee kama mimi singeweza kuvumilia kitu kama hicho. Yasahau hayo, ni bora tu kuacha imani yangu. Baada ya hapo, sikuhudhuria mikusanyiko tena, na ndugu wa kike walikuja nyumbani kwangu kunitafuta mara kadhaa na siku zote nilijificha ili wasiweze kunipata.

Lakini wakati huo nilipokuwa sihudhurii mikusanyiko, mradi nilifikiria jinsi ilivyokuwa upendo mkubwa wa Mungu ambao uliniokoa kutoka kwa mateso yangu na uzuri na furaha ya ndugu wa kiume na wa kike na mimi tukiimba nyimbo na kumsifu Mungu pamoja, niliukosa na kuutamani sana lakini bado niliogopa binti mkwe wangu na wengine kutoa taarifa yangu kwa polisi. Nilihisi maumivu mengi na mateso ndani ya moyo wangu na sikujua ni ipi iliyokuwa njia bora ya amali. Wakati huo, mfanyakazi mwenzangu (ndugu wa kiume aliyeamini katika Mungu) alikuja nyumbani kwangu kunitembelea ili kuona ni kwa nini sikuwa nikihudhuria mikutano hivi karibuni. Nilimwelezea jinsi binti mkwe wangu alivyokuwa akinisumbua juu ya kuamini katika Mungu. Baada ya kusikia haya, yeye alifanya ushirika kwangu, “Tunapozongwa na mambo haya, hakika ni mapambano ya kiroho. Ni kama baa ambalo Ayubu alikabiliwa nalo, kwa vile kwa juu lilionekana kama ilikuwa limesababishwa na wezi waliokuwa wakimwibia, lakini kwa kweli kilichokuwa nyuma yake ni maumivu makali ya Shetani ya watu na kupigana juu ya wanadamu na Mungu. Kwa sababu Ayubu alimheshimu Mungu na aliweza kuepuka uovu, hatimaye angeweza kumshuhudia Mungu wakati Shetani alidhalilishwa katika ushinde. Kwa hiyo, tunapozongwa na mambo haya, nia ya Mungu ni kutufanya tutambue asili ya Shetani ya uovu. Tunapomwamini Mungu, tunachopaswa kufanya tu ni kumtegemea Mungu, kutafuta ukweli, na kuwa makini kiroho, na ni hapo tu ndio tutaweza kubaini mpango wa Shetani na kushuhudia! Kisha tunaweza kuepuka kutekwa na Shetani. Vinginevyo, tutapoteza fursa ya kupokea wokovu.”

Baada ya hapo, mfanyakazi mwenzangu alinisomea kutoka kwa neno la Mwenyezi Mungu: “Mungu anafanya kazi, Mungu anamtunza mtu, anamwangalia mtu, na Shetani anafuata hatua Yake yote. Yeyote anayefadhiliwa na Mungu, Shetani pia anatazama, akifuata nyuma. Iwapo Mungu anamtaka mtu huyu, Shetani atafanya kila kitu kwa uwezo wake kumzuia Mungu, akitumia mbinu mbalimbali mbovu kujaribu, kusumbua na kuharibu kazi anayofanya Mungu ili kufikia lengo lake lililofichwa. Lengo lake ni nini? Hataki Mungu awe na mtu yeyote; anataka wale wote ambao Mungu anataka, kuwamiliki, kuwatawala, kuwaelekeza ili wamwabudu, ili watende maovu pamoja naye. Je, hii siyo nia ya husuda ya Shetani? Kwa kawaida, ninyi husema mara nyingi kwamba Shetani ni mwovu sana, mbaya sana, lakini umemwona? Mnaweza kuona tu jinsi ambavyo mwanadamu ni mbaya na hamjaona kwa uhakika jinsi ambavyo Shetani ni mbaya sana. Lakini mmemwona kwa hili swala linalohusiana na Ayubu? (Ndiyo.) Swala hili limeufanya uso wenye sura mbaya wa Shetani na kiini chake kuwa wazi kabisa. Shetani yuko vitani na Mungu, akifuata nyuma Yake. Lengo lake ni kubomoa kazi yote ambayo Mungu anataka Kufanya, kuwamiliki na kudhibiti wale wote ambao Mungu anawataka, kuwafisha kabisa wale ambao Mungu anataka. Kama hawajafishwa, basi wanakuja kwa milki ya Shetani kutumiwa naye—hili ndilo lengo lake(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IV). “Lazima muwe macho na kusubiri kila wakati, na ni lazima mje mbele Yangu zaidi. Lazima mtambue mipango ya njama na hila mbalimbali za Shetani, mjue roho, mjue watu na mweze kupambanua watu wa aina zote, masuala na mambo; lazima mle na mnywe maneno Yangu zaidi na, muhimu zaidi, lazima mweze kuyala na kuyanywa nyinyi wenyewe. Jiandaeni wenyewe na ukweli wote, njooni mbele Yangu ili nifungue macho yenu ya kiroho na kuwaruhusu kuona siri zote zilizo rohoni(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 17).

Baada ya yeye kumaliza kusoma kutoka kwa neno la Mungu, mfanyakazi mwenzangu alifanya ushirika kwangu kuhusu hilo, akisema: Ni mapambano makali ya kiroho tunapozongwa na vitu hivi. Kwa sasa, dunia nzima inamilikiwa na Shetani, yule mwovu, na Shetani huendelea kufanya kazi yake ya kuwapotosha wanadamu. Shetani anataka kuwamiliki kikamilifu na kuwaangamiza wanadamu ambao Mungu aliumba, na hili ndilo lengo bovu la Shetani. Mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita wa Mungu ni kwa ajili ya kuwaokoa wanadamu kutoka kwa ushawishi wa giza wa Shetani. Hasa wakati wa sasa wa siku za mwisho, katika kueleza neno Lake, Mungu anafanya hatua ya mwisho ya kazi, hiyo ya kuwatakasa na kuwaokoa wanadamu, na Shetani anaogopa kwamba tutaikubali kazi ya Mungu, na kwamba tutauelewa ukweli na kuupokea wokovu. Anaogopa kwamba tutatofautisha asili yake ya uovu na ya kupinga maendeleo, kumwacha, na kumtelekeza. Kwa sababu ya hili yuko kwa maumivu makuu ya mapambano yake ya mwisho ya kifo—kupigana na Mungu kwa ajili ya wateule wa Mungu na akitumia kila mkakati wa kudharauliwa ili kutuzuia kuja mbele ya Mungu. Njama kama ukandamizaji na utekaji unaofanywa na CCP, kuvuruga na kuwatesa wanafamilia, pamoja na uvumi na kashfa zinazoenezwa na jamii za kidini pamoja na serikali CCP zote zinatekelezwa ili kutuzuia kumgeukia Mungu. Lakini hekima ya Mungu hutumiwa kulingana na njama ya Shetani, na sasa Mungu anatumia vurugu ya Shetani kufanya huduma kwa kazi ya Mungu. Kwa njia hii Yeye hukamilisha imani yetu na uaminifu. Kutoka nje, ni mwana wako wa kiume na binti mkwe wako pamoja na serikali CCP wakitumia kila aina za mbinu na njia kutuzuia na kutukinza kuamini katika Mungu, lakini kwa kweli kisirisiri ni ujanja unaofanywa na Shetani. Mradi tunatia bidii zaidi kutafuta ukweli na kuelewa mapenzi ya Mungu, kuwa na ujuzi fulani wa kazi ya Mungu, tunaweza kutambua hila zote za Shetani na ujanja, na tunaweza kuwa mashahidi kwa Mungu, Shetani ataaibishwa katika ushinde. Mradi hatutafuti kuelewa ukweli na hatuelewi mapambano ya kiroho, wakati Shetani husababisha vurugu kwetu tunaweza kupotoshwa na kuibua shaka juu ya Mungu hata kiasi cha kumkataa Mungu, kumsaliti Mungu, na tukimwacha Mungu nyuma. Kwa njia hii itatokea kwamba utakuwa mwathiriwa wa hila za Shetani na kukosa fursa ya kupokea wokovu. Mwishowe utamezwa na Shetani. Kwa hiyo lazima kwa ukamilifu tutie bidii zaidi kuomba na kumkaribia Mungu, na tuinue usomaji wetu wa neno la Mungu na kujiandaa na ukweli. Ni kwa njia hii tu tunapoweza kuyaelewa mapenzi ya Mungu, kubaini hila za Shetani, na kuwa mashahidi kwa Mungu.

Kwa njia ya kusoma neno la Mungu na kile mfanyakazi mwenzangu alichofanyia ushirika, kwa ghafla nikagundua: Haya kweli ni mapambano ya kiroho. Mungu huonyesha ukweli katika siku za mwisho ili kuwaokoa binadamu, lakini Shetani hufikiria kila njia inayowezekana kutumia shinikizo na mateso kupitia mwanangu wa kiume, binti mkwe wangu, na serikali ya CCP kunizuia kuamini katika Mungu na kumfuata Mungu. Anaogopa kwamba nitaikubali kazi ya Mungu katika siku za mwisho na kuuelewa ukweli. Kwa hiyo nitatofautisha asili yake mbovu, ya kutisha, ya kishetani, ya pepo na kumsaliti na kumtelekeza, na kupata wokovu wa Mungu. Leo, nimekwisha kuona uovu wa kudharauliwa wa Shetani na kuelewa utunzaji wa kujitahidi na fikra ambazo Mungu aliweka katika kunikomboa. Baadaye, nitalisoma zaidi neno la Mungu na kujiandaa na ukweli ili nisitumiwe na Shetani kwa manufaa yake. Hisia nilizozizuia kwa muda mrefu hatimaye zimewekwa huru katika neno la Mungu, na nilihisi furaha sana kama kwamba nilikuwa nikiona mwanga wa mchana tena.

Ingawa nilielewa kwamba binti mkwe wangu kunisumbua kwa kuamini katika Mungu kulikuwa mojawapo tu ya hila za Shetani, na kwamba sipaswi kudanganywa na Shetani, bado nilikuwa na wasiwasi kiasi kwamba kama serikali ya CCP ingegundua kuhusu imani yangu ingekuwa na athari juu ya kazi za mwanangu wa kiume na binti mkwe wangu. Hata nilikuwa na hofu zaidi ya athari ambayo ingekuwa nayo kwa mjukuu wangu kwenda shule. Hivyo nikamwambia mfanyakazi mwenzangu kuhusu masikitiko yangu naye akanisomea kifungu kingine kutoka kwa neno la Mwenyezi Mungu: “Mamlaka ya Mungu yapo licha ya hali mbalimbali; katika hali zote, Mungu anaamuru na kupangilia hatima ya kila binadamu na mambo yote kulingana na fikira Zake, mapenzi Yake. Hali hii haitabadilika kwa sababu binadamu hubadilika, na iko huru wala haitegemei mapenzi ya binadamu, haiwezi kubadilishwa na mabadiliko yoyote ya muda, anga, na jiografia, kwani mamlaka ya Mungu ndiyo hali yake halisi kabisa. … Siku zote Mungu hushikilia mamlaka Yake, huonyesha uwezo Wake, huendeleza usimamizi Wake wa kazi kama kawaida; kila wakati Anatawala viumbe wote, hutosheleza viumbe wote, huunda na kupangilia viumbe wote, kama Alivyofanya siku zote. Hakuna anayeweza kubadilisha hili. Hii ni hoja; huu umekuwa ukweli usiobadilika tangu zama za kale!(Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III). Baada yakusoma neno la Mungu, mfanyakazi mwenzangu akaendelea kufanya ushirika kulihusu: Mungu ni Muumba, na ni mwenye enzi juu ya mbingu, nchi, na kila kitu ndani yake. Pia Yeye hudhibiti jaala ya kila mtu, na aina yoyote ya kazi au mustakabali kila mmoja wetu anayo yaliamuliwa na Mungu muda mrefu uliopita. Hiki ni kitu ambacho hakuna mtu anayeweza kuamua au kubadilisha mwenyewe. Kazi za mwanao wa kiume wako na binti mkwe wako zote zinadhibitiwa na Mungu. Haijalishi kama wanaamini kwa Mungu au la; jaala yao inaamuriwa na kupangwa na Mungu. Haihitajiki sisi kuwa na wasiwasi juu ya hili au lile. Ayubu hakuwa na wasiwasi juu yalo, kwa sababu ilikuwa dhahiri kwake kwamba yote aliyokuwa nayo alipewa na Mungu, na chochote alichotunukiwa au kuondolewa kwake vyote vilifanywa na Mungu. Kwa hiyo tunapaswa kujishughulisha tu na kuomba kwa Mungu, na kuuaminisha mustakabali wa wana wetu wa kiume na binti zetu katika mikono ya Mungu na kuwa na imani kwamba Mungu ana mpango mwafaka…. Kwa njia ya maneno haya yaliyoshirikiwa kwangu kuhusu kuyajua mamlaka ya Mungu, nikaja kuwa na imani kwa Mungu, na nilikuwa thabiti na mwenye amani ndani ya moyo wangu. Singeweza tena kuwa na wasiwasi juu ya mustakabali wa mwanangu au binti yangu.

Baadaye, kupitia kusoma neno la Mungu, nilifanya maendeleo katika kujua asili mbovu ya uadui wa serikali ya CCP kwa Mungu. Neno la Mwenyezi Mungu linasema: “Ibilisi anaufunga mwili wote wa mwanadamu, anafumba macho yake yote, na kufunga kinywa chake kwa nguvu. Mfalme wa pepo amefanya ghasia kwa maelfu kadhaa ya miaka, hadi leo hii, wakati bado anaangalia kwa karibu mji ulio mahame kana kwamba ulikuwa kasiri la pepo lisilopenyeka; kundi hili la walinzi, wakati uo huo, wakiangalia kwa macho yanayong’aa, wakiogopa sana kwamba Mungu atawakamata bila wao kujua na kuwafutilia wote mbali, Akiwaacha wakiwa hawana sehemu ya amani na furaha. Inawezekanaje watu wa mji wa mahame kama huu wawe wamewahi kumwona Mungu?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi na Kuingia (8)). Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha pia husema: “Katika moyo wa joka kubwa jekundu, huwa likifikiri kuwa Mungu amekuja kulinyang’anya watu wote ambao ni walo, na Yeye anafanya uadui nalo. Joka hili jekundu ni kitu kisichopingwa na ni muhali! Wanadamu wameumbwa na Mungu, na Mungu ana mamlaka ya kuwaokoa wanadamu. Mwanzoni, wanadamu ni wa Mungu, na ni joka kubwa jekundu ambalo limejitwalia bila haki wateule wa Mungu, kuwapotosha na kuwakanyaga linapopenda, na hatimaye likiwameza wote. Hata hivyo, wakati Mungu anapokuja kuwaokoa wanadamu, joka hili humpinga Yeye. Tunaweza kuona kutokana na hili kwamba asili muhimu ya joka kubwa jekundu ni katika upinzani dhidi ya mbingu, mpinga mageuzi, muhali, na ya kipumbavu mno. Ni mnyama wa mwitu na pepo” (Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha). Sasa, ninaelewa kwamba katika nchi hii ya kumkana Mungu mamlaka ya CCP ni mamlaka ya Shetani. Haimruhusu Mungu kuja katika nchi hii na kufanya kazi ya kuwaokoa watu, wala haiwaruhusu watu kujinasua kutoka kwa ushawishi wake wa giza na kupatwa na Mungu, kuongozwa na Mungu kwenye hatima nzuri wa safari. Kwa hiyo hufanya yote inayoweza kumpinga na kumshutumu Mwenyezi Mungu na kazi ya Mwenyezi Mungu, ikitusumbua na kutuzuia kwa hasira dhidi ya kumfuata Mwenyezi Mungu. Kama hatuna ukweli, hatuzijui hila za CCP, na hatubaini asili yake, itakuwa rahisi kupotoshwa na aina zote za uongo inazosambaza, au kutishika hadi kujisalimisha kwa ukandamizaji wake na mateso. Hatutathubutu kuja katika uwepo wa Mungu, na hili linamaanisha kuwa imefanikisha lengo lake la kuwala watu na kuangamiza kazi ya Mungu ya kuwaokoa watu. Lakini hakuna yeyote anayeweza kuipenya hekima ya Mungu. Mungu huyatumia kikamilifu mateso ya CCP kufanya huduma ya kuwakamilisha watu walioteuliwa wa Mungu, ili kuwaruhusu watu kuuelewa ukweli, na kuelewa kabisa kwamba serikali ya CCP ni pepo ya shetani ambayo imejaa uadui kwa ukweli na humchukua Mungu kama adui wake, ili waweze kuitelekeza kabisa na kumgeukia Mungu kikamilifu. Ni kama wakati nilipopata uzoefu wa mateso haya, kwa kuwa mtoto wangu wa kiume na binti mkwe wangu, na pia wazazi wakwe zangu, wote walipotoshwa na uongo wa serikali ya CCP. Chini ya vitisho vya CCP kutumia vibaya madaraka yake, walinilazimisha kumwacha Mwenyezi Mungu na kunisababisha kukosa kupokea wokovu kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Lakini sasa, kwa njia ya kusoma neno la Mungu, nimeona kwa dhahiri kuwa serikali ya CCP hutumia uongo kuwapotosha watu, na hutumia mbinu za nguvu nyingi zaidi kuwawekea watu mipaka na kuwazuia kuamini katika Mungu. Nimeona kuwa lengo lake ni kutuleta sote chini ya udhibiti wake na hatimaye kudhuriwa na kumezwa nayo. Jinsi ninavyozidi kufikiri kuhusu hilo, ndivyo ninavyozidi kumchukia huyu pepo wa kishetani, hili joka kubwa jekundu ambalo ni CCP. Ni ya kikatili, ya kuwapuuza watu kabisa, na huwadhulumu na kuwatesa wale wanaomwamini Mungu. Uhalifu wake wa uovu kwa kweli hufurika katika mbingu, na bila kuepuka itakabiliwa na adhabu ya Mungu! Nina shukurani kwa uongozi wa neno la Mungu, ambao uliniruhusu kutofautisha asili ya kishetani ya upinzani wa CCP kwa Mungu na kwa kutozuiwa tena na vitisho vyake. Ninashukuru pia kwamba Mungu alisababisha mfanyakazi mwenzangu kuja nyumbani kwangu na kunisaidia wakati nilipokuwa hasi na dhaifu, na nilipokuwa nimeanguka chini na kupotea njia. Alitumia neno Lake kuniongoza na kuniokoa kutokana na kujaribiwa na Shetani, na kunifanya kupenya wavu wa Shetani na kurudi mbele ya Mungu na kuwa na fursa ya kupokea wokovu. Nimeamua kwamba bila kujali shida nyingi zilizoko kwenye barabara iliyo mbele, nitamfuata Mwenyezi Mungu kwa njia yote hadi mwisho wa barabara!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp