Chanzo cha Mafanikio ya Umeme wa Mashariki

17/01/2021

Kutajwa kwa Umeme wa Mashariki kunawafadhaisha ndugu wengi katika Bwana huhisi mafadhaiko: Ni kwa nini jumuiya ya kidini kwa ujumla huzidi kuhuzunika na kupotoka, wakati kila dhehebu linazidi kuwa na hadhari na kushikilia ukale katika kushutumu na kufukuza Umeme wa Mashariki, Umeme wa Mashariki halikosi kuhuzunika au kudhoofika tu, lakini huendelea mbele kama wimbi linalojongea lisiloweza kusimamishwa, likienea kote bara China, na sasa kwa kuwa hata limepanuka hata nje ya mipaka ya China hadi nchi za kigeni na maeneo na linakubaliwa na watu zaidi na zaidi duniani kote? Kama wamekabiliwa na ukweli huu, watu wa kidini wamefadhaika kabisa, huku kwa kweli sababu ni rahisi kabisa: Kile ambacho madhehebu mbalimbali kinaita Umeme wa Mashariki ni Mwokozi Yesu aliyerudi wa siku za mwisho, akishuka kutoka mbinguni juu ya “wingu jeupe”; ni Mungu mwenye vitendo Mwenyewe, ambaye alirejea kwa mwili! Kwa sababu hii, licha ya ukweli kwamba kila dhehebu ulimwenguni humpinga, kumshambulia, au kumshutumu Mungu mwenye mwili wa siku za mwisho au kazi Yake, hakuna mtu yeyote wala nguvu yoyote ambayo inaweza kuzuia au kukomesha kamwe kile Anachotaka kufanikisha. Mamlaka ya Mungu, nguvu, na uweza Wake na hekima haviwezi kushindwa kwa nguvu yoyote ya Shetani.

Watu wengi huamini kwamba chochote kilichoshutumiwa na viongozi wa dini na chama cha utawala hakiwezi kuwa njia ya kweli, lakini mtazamo huu unakubaliana na ukweli? Fikiria nyuma kwa Enzi ya Neema wakati Mungu alipata mwili kama Bwana Yesu ili kuanza kazi Yake mpya huko Yudea. Kuanzia mwanzo hadi mwisho Alishutumiwa, kupingwa, na kuteswa na wakuhani wakuu wa Kiyahudi, waandishi na Mafarisayo. Walimhukumu Bwana Yesu kwa ajili ya kuwa mwana wa seremala, wakajaribu kupata kila aina za lawama dhidi Yake, na kuzungumza maneno ya kukufuru kwamba Alifukuza pepo kwa usaidizi wa mfalme wa pepo. Walifanya kila kitu ambacho wangeweza kumuua Bwana Yesu. Mwishowe, walishirikiana na Roma kumfanya Bwana Yesu akamatwe, na wakamsulubisha Bwana Yesu mwenye huruma msalabani. Hata baada ya Bwana Yesu kufufuka na kupaa mbinguni, bado walibuni kila aina za uvumi, na vile vile wakawasingizia na kuwakashifu Yohana, Paulo, na mitume na wanafunzi wengine, wakiwaita “kikundi kiovu cha Wanazareti,” “wazushi” na “washirika wa dhehebu mbaya” Walifanya kila kiwezekanacho kuwakamata na kuwatesa wanafunzi wa Bwana Yesu. Lakini hekima ya Mungu daima hutumia na hujenga juu ya hila za Shetani; kazi Yake ingewezaje kuzuiwa au kuharibiwa na Shetani? Mungu alitumia mateso matundu na ufukuzaji wa Uyahudi na Ufalme wa Kirumi kuwashurutisha wanafunzi kukimbia kwa mataifa mengi, hivyo basi kueneza wokovu wa Bwana Yesu kotekote, kwa miisho ya dunia. Ndugu, hebu tufikirie: viongozi wa Kiyahudi na serikali ya Kirumi walimpinga na kumshutumu Bwana Yesu na kazi Yake kwa shauku. Hilo lingeweza kuwa kwa sababu Bwana Yesu hakuwa Mungu wa kweli? Ingeweza kuwa kwa sababu Bwana Yesu hakuwa akileta njia ya kweli? Ingeweza kuwa kwa sababu kile wanafunzi na mitume wa Bwana Yesu walikuwa wakieneza hakikuwa wokovu wa Mungu? Ingeweza kuwa kwamba kile viongozi wa dini na serikali ya Kirumi kiliacha na kupinga hakikuwa njia ya Mungu? Ingeweza kuwa kwamba njia ya kweli inaamuliwa na viongozi wa dini na watu wa siasa wenye mamlaka? Sote tunafahamu kwamba hii ingalikuwa kazi ya Mungu, hata kama jamii ya dini na dunia nzima ingaliipinga na kuitelekeza, kazi ya Mungu haiwezi kukanwa; hakuna ubaguzi. Bwana Yesu Kristo alisema: “Na hii ndiyo shutuma, ya kwamba mwanga umekuja duniani, na wanadamu walipenda kiza badala ya mwanga, kwa kuwa vitendo vyao vilikuwa viovu. Kwa kuwa kila mtu afanyaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwa mwanga, vitendo vyake visije vikashutumiwa(Yohana 3:19-20). “Ikiwa dunia ikiwachukia, ninyi mnajua ya kwamba ilinichukia mimi kabla iwachukie ninyi(Yohana 15:18). “Hiki ni kizazi kiovu(Luka 11:29). 1 Yohana 5:19 inasema, “Ulimwengu mzima uko ndani ya maovu.” Baada ya mwanadamu kupotoshwa na Shetani, alianguka hadi kiwango ambapo anadharau na kuchukia ukweli, na kuwa adui wa Mungu. Dunia nzima inadhibitiwa na Shetani kabisa, na jamii nzima ya dini imedhibitiwa kwa muda mrefu na Mafarisayo wanafiki na wapinga Kristo. Yote yanatawalwa na Shetani. Kwa hivyo, wakati Mungu mwenye mwili anaonekana kufanya kazi Yake, haiepukiki kwamba viongozi wa dini na nguvu za Shetani zitaibuka kumshutumu na kumpinga Mungu na kazi Yake. Ni wazi kwamba, si sahihi na ni upuuzi kutathmini ukweli na iwapo viongozi wa dini au utawala wa kishetani unaushutumu!

Sasa, katika siku hizi za mwisho, Mungu amekuwa mwili tena huko Uchina—ngome thabiti ya ukana Mungu, maficho halisi ya joka kubwa jekundu—kutekeleza kazi Yake ya hukumu kuanzia na nyumba Yake. Mungu hutoa ukweli kuwahukumu na kuwatakasa wanadamu, kusudio likiwa kumwokoa mwanadamu kabisa kutokana na ushawishi muovu wa Shetani, na hatimaye, waliookolewa wataletwa ndani ya ufalme wa Mungu na Yeye na kuingia rahani pamoja na Mungu. Hata hivyo, tanzia ya kihistoria ya upinzani wa Kiyahudi kwa Bwana Yesu inatendwa tena. Kwa kuwa Mungu hufanya kazi Yake mpya ya siku za mwisho ambayo hulipiza dhidi ya mawazo ya watu kutoka madhehebu mbalimbali, hawakaribishi kurudi kwa Bwana Yesu. Badala yake, wanaeneza kila aina ya uzushi na uwongo. Wanamshambulia na kumkashifu Mungu mwenye mwili, wakishutumu kazi Yake kama “dhehebu ovu” ama “uzushi.” Hata wanafika kiwango cha kushirikiana na serikali ya Kikomunisti ya Kichina kuwatesa na kuwakamata wale wanaoeneza injili ya Mungu katika siku za mwisho, Matendo yao si tofauti na yale ya jamii ya dini ya Kiyahudi ambayo wakati mmoja ilimsingizia na kumtesa Bwana Yesu. Ukweli huu umetimiza unabii wa Bwana Yesu kabisa, “Kwani kama umeme, unavyomulika chini ya mbingu kutoka sehemu moja, huangaza hadi sehemu nyingine chini ya mbingu; vivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika siku yake. Bali kwanza lazima apitie mambo mengi, na akataliwe na kizazi hiki(Luka 17:24-25). Mungu amepata mwili mara mbili miongoni mwa mwanadamu kuzungumza na kufanya kazi, kuwakomboa wanadamu na kuwaokoa wanadamu, na nyakati zote mbili Amepitia shutuma, kufuru, na upinzani wa viongozi wa dini na utawala wenye mamlaka; ukweli huu pekee unatosha kudhibitisha kwamba njia ya kweli imesumbuliwa tangu nyakati za zamani. Kadri njia ilivyo ya kweli na kadri ilivyo kuonekana na kazi ya Mungu, ndivyo inavyopitia kukanwa na kushutumiwa zaidi na viongozi wa dini na utawala wa kishetani. Werevu wanaweza kuamua kutoka kwa mateso na shutuma fidhuli ya Mwenyezi Mungu na kazi Yake ya siku za mwisho na wachungaji na wazee wa dunia ya dini na serikali ya CCP iwapo ni njia ya kweli au la, na hivyo kufanya uchaguzi wa hekima.

Kwa hivyo, kwa kuwa Umeme wa Mashariki ni njia ya kweli, kwa nini unapingwa na viongozi wa dini? Kuna sababu mbili za msingi za hili: 1.) Watu hawaelewi mwelekeo wa kazi ya Roho Matakatifu na hawana ufahamu wa kifungu, “Kazi ya Mungu milele husonga mbele.” Wanapima kazi mpya ya Mungu kwa msingi wa maarifa ya Biblia na mawazo ya dini na kile ambacho Mungu alifanya zamani tu. Iwapo hawakubaliani na kile wanachoona, basi watachukulia kazi mpya ya Mungu kama “ya uzushi” au “ya dhehebu mbaya.” 2.) Kwa sababu asili ya kishetani ya wanadamu ni kudharau na kuchukia ukweli. Viongozi hawa wa dini wanaogopa kutengwa na kukataliwa baada ya waumini wao kusoma neno la Mwenyezi Mungu, kuelewa ukweli, na kurudi kwa Mwenyezi Mungu, kwa hivyo ili kuhakikisha udhibiti wao wa milele wa dunia ya dini na kulinda hadhi na riziki zao wenyewe, wanashutumu na kumpinga Mwenyezi Mungu kwa shauku. Kwa hivyo, sababu ya kazi Yake yote kukumbana na upinzani kutoka kwa watu si kwa ajili ya kosa lolote katika kazi mpya ya Mungu, wala kwa ajili ya kosa katika njia Yake. Badala yake, ni kwa sababu watu hawaelewi kazi ya Mungu na kwa sababu wanadharau na kuchukia ukweli. Litakuwa jambo la upuuzi na la mzaha ikiwa watu wangeamua kwamba hii si njia ya kweli kwa sababu tu viongozi wa dini wanaipinga na kuitelekeza kazi mpya ya Mungu. Itakuwa hasara ya milele kwa watu wakipoteza wokovu wa Mungu katika siku za mwisho kwa sababu ya hili, kosa la kufisha lisilookoleka na lisilo na shaka.

Basi ni kwa jinsi gani hasa, tunavyotofautisha kati ya njia ya kweli na njia ya uongo? Neno la Mungu hutupa kanuni ambazo kwazo tunaweza kutofautisha. Mwenyezi Mungu anasema: “Kuijua kazi ya Mungu si jambo rahisi. Unapaswa kuwa na viwango na malengo katika utafutaji wako, unapaswa kujua jinsi ya kutafuta njia ya kweli, na jinsi ya kupima kujua kama ni njia ya kweli au si ya kweli, na kama ni kazi ya Mungu au kinyume chake. Kanuni ya msingi kabisa katika kuutafuta ukweli ni nini? Unapaswa kuangalia kama kuna kazi ya Roho Mtakatifu au la kwa njia hii, iwapo maneno haya ni maonyesho ya ukweli, yanamshuhudia nani, na ni kitu gani yanaweza kukupatia. Kutofautisha kati ya njia ya kweli na hizi njia za uongo kunahitaji njia kadhaa za maarifa ya msingi, ya msingi kabisa kati ya zote ni kusema iwapo kuna Kazi ya Roho Mtakatifu au la. Maana kiini cha imani ya mwanadamu katika Mungu ni imani katika Roho Mtakatifu. Hata imani yake katika Mungu mwenye mwili ni kwa sababu mwili huu ni mfano halisi wa Roho wa Mungu, ikiwa na maana kwamba imani hiyo bado ni imani katika Roho. Kuna tofauti kati ya Roho na mwili, lakini kwa kuwa mwili unatokana na Roho, na ndio Neno linakuwa mwili, hivyo kile ambacho mwanadamu anaamini katika ni uungu halisi wa Mungu. Na hivyo, katika kutofautisha kama ni njia sahihi au la, zaidi ya yote unapaswa kuangalia kama kuna kazi ya Roho Mtakatifu, na baada ya hapo unapaswa kuangalia kama kuna ukweli katika njia hii. Ukweli huu ni tabia ya maisha ya ubinadamu wa kawaida, ni sawa na kusema, kile ambacho Mungu alitaka kwa mwanadamu alipomuumba hapo mwanzo, yaani, ubinadamu wote wa kawaida (ikiwa ni pamoja na hisia za kibinadamu, umaizi, hekima, na maarifa ya msingi ya kuwa mwanadamu). Yaani, unapaswa kuangalia iwapo njia hii inaweza kumpeleka mwanadamu katika maisha ya ubinadamu wa kawaida au la, iwapo ukweli uliozungumzwa unahitajika kulingana na uhalisi wa ubinadamu wa kawaida au la, iwapo ukweli huu ni wa kiutendaji au hali, na iwapo ni wa wakati muafaka au la. Ikiwa kuna ukweli, basi unaweza kumpeleka mwanadamu katika uzoefu wa kawaida na halisi; aidha, mwanadamu anakuwa wa kawaida zaidi, hisia za kawaida za kibinadamu zinakuwa kamili zaidi, maisha ya mwanadamu katika mwili na maisha ya kiroho yanakuwa katika mpangilio mzuri zaidi, na mihemko ya mwanadamu inakuwa ya kawaida kabisa. Hii ni kanuni ya pili. Kuna kanuni nyingine moja zaidi, ambayo ni iwapo watu wana maarifa mengi juu ya Mungu au la, kama unapitia uzoefu wa kazi hiyo na ukweli unaweza kuchochea upendo wa Mungu ndani yao au na kuwasogeza karibu zaidi na Mungu. Katika hili, inaweza kupimwa iwapo ni njia sahihi au la. Kanuni ya msingi ni iwapo njia hii ni ya uhalisi badala ya kuwa ya kimiujiza, na iwapo inaweza kutoa maisha ya mwanadamu. Kama inakubaliana na kanuni hizi, hitimisho linaweza kuwekwa kwamba njia hii ni njia ya kweli(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Wale tu Wanaomjua Mungu na Kazi Yake Ndio Wanaoweza Kumridhisha Mungu). Kimsingi kuna mambo matatu kutoka kwa maneno ya Mwenyezi Mungu ambayo tunapaswa kutambua ili tutofautishe kama kitu fulani ni njia ya kweli:

Kwanza, lazima tuangalie kuona ikiwa kina kazi ya Roho Mtakatifu, ambalo ni jambo muhimu. Kama ni njia ya kweli, basi ni kazi ya Mungu Mwenyewe, ambayo inamaanisha lazima kiwe na kazi ya Roho Mtakatifu. Sababu watu huamini katika Mungu mwenye mwili ni kwa sababu mwili huu ni mfano wa Roho wa Mungu, kwa hiyo yote ambayo Yeye hufanya ni kazi ya Roho Mtakatifu na huwa na uthibitisho wa Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, watu humwamini Yeye na kumfuata Yeye. Hii ni kama tu wakati Bwana Yesu alifanya kazi Yake: Ingawa kwa juu juu huenda ilionekana kwamba Yeye alikuwa mtu wa kawaida na wa desturi, kupitia neno Lake na kazi Yake mwanadamu aliona kazi ya Roho Mtakatifu. Hii ni kwa sababu binadamu wote waliweza kuona kwamba maneno na kazi ya Bwana Yesu yamejaa mamlaka na nguvu. Aliweza kumfanya kipofu aone au mtu aliyepooza atembee, na kuponya wakoma. Aliweza kutumia mikate mitano na samaki wawili kuwalisha watu elfu tano. Aliweza hata kuwafufua wafu. Aliweza kuona ndani ya mioyo ya wanadamu kwa kina na kufichua siri zao mbovu zaidi. Aidha, Aliweza kuwaambia wanadamu siri za mbinguni. Baada ya watu kumfuata, wao walipata amani na furaha katika mioyo yao. Sababu watu walimfuata Bwana Yesu na kutambua kwamba Yeye alikuwa Masihi ni kwa maana yote Anayofanya ni kazi ya Roho Mtakatifu. Tunaweza kuona kwamba almradi ndiyo njia ya kweli, itakuwa na kazi ya Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, wakati wa kuangalia kama kitu ni njia ya kweli, tunapaswa kwanza kukiangalia ili kuona kama kina kazi ya Roho Mtakatifu.

Kipengele cha pili ambacho tunapaswa kupima wakati wa kuangalia kama kitu ni njia ya kweli ni kuona kama kina ukweli na ikiwa kinaweza kubadilisha tabia ya maisha ya mtu hatua ya kwa hatua ili kufanya ubinadamu uwe wa kawaida kwa kuongezeka hatua kwa hatua. Sote tunajua kwamba Mungu ni ukweli, njia, na uzima, na kwamba kila hatua mpya ya kazi Yake inategemea ukweli ambao Mungu hutoa kwa mtu, ambao huonyesha njia ya matendo katika enzi mpya. Mungu huhakikisha mtu ana ruzuku anazohitaji kwa maisha ili hatua kwa hatua aweze kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wa kawaida na ili hatua kwa hatua arudi kwa mfano wa asili wa wakati Mungu alipomuumba mwanadamu. Hii ni sifa bainifu dhahiri ya njia ya kweli. Ni kama tu wakati Bwana Yesu alipoanza kazi Yake katika Enzi ya Neema. Wakati huo, alitoa ukweli mwingi kwa watu ili wauweke katika matendo, na kuwafundisha kuwapenda wengine kama wanavyojipenda wenyewe, kuubeba msalaba, kujinyima, na kuwasamehe wengine mara saba mara sabini. Bwana Yesu aliwaambia watu kumwabudu Mungu katika roho na ukweli. Kila muumini wa kweli angeweza kuwa na mabadiliko fulani katika mwenendo wake wa nje kupitia mafundisho ya Bwana Yesu. Kwa njia ya Bwana Yesu, angeweza kujiendesha kwa unyenyekevu na uvumilivu, na kwa njia hiyo kumiliki mfano fulani wa mtu wa kawaida. Kwa hiyo, alimradi ni njia ya kweli, kutakuwa na maonyesho ya ukweli. Hili, basi litafanya ubinadamu na akili ya mtu iwe ya kawaida zaidi na zaidi, na ataonekana zaidi jinsi mtu halisi anavyopaswa kuwa.

Kipengele cha tatu tunachopaswa kuangalia katika kutafakari njia ya kweli ni kuona kama njia hii inaweza huwapa watu ujuzi zaidi juu ya Mungu na kama inatia msukumo upendo wa Mungu ndani yao na huwaleta karibu na Mungu. Sote tunajua kwamba kwa kuwa ni njia ya kweli, ni kazi ya Mungu Mwenyewe na kwamba kazi Yake huleta bila kuzuilika tabia Yake na chote kile ambacho Mungu anacho na alicho. Wakati watu wanapopitia kazi ya Mungu, kwa kawaida wao hufikia ufahamu wa kweli wa Mungu, na kwa njia hiyo kuonyesha moyo wa upendo kwa Mungu ndani yao. Hii ni kama tu katika Enzi ya Sheria Yehova Mungu alipotoa sheria za kuyaongoza maisha ya watu duniani. Kutokana na uzoefu wao na kazi Yake, walitambua kuwa Yehova Mungu ni Mungu mmoja wa kweli. Aidha, walitambua uadhama na hasira ya Mungu na kwamba tabia Yake ni sharti isikosewe, ambayo ilisababisha ndani yao moyo wa kumchaji Mungu. Katika Enzi ya Neema, Mungu mwenye mwili alikuja duniani kufanya hatua ya kazi ya kuwakomboa wanadamu. Kupitia uzoefu wao na kazi ya Bwana Yesu, watu walitambua tabia ya Mungu ya upendo na huruma. Watu pia waliona kwamba Mungu hakuwa tu Roho lakini pia Angeweza kuchukua mfano wa unyenyekevu wa binadamu, na kwamba Angetenda miujiza, kuponya magonjwa na kuwatoa pepo…. Na kazi hii yote ambayo Bwana Yesu alifanya iliwafanya watu wawe na ufahamu mpya wa Mungu, ambao ulivutia kuabudu kwa Mungu ndani ya mioyo ya watu. Kwa hiyo, kama ni njia ya kweli, itawafanya watu kuelewa zaidi kuhusu Mungu na kutia msukumo ufahamu mkubwa zaidi kuhusu tabia ya Mungu.

Ingawa kazi ya Mungu huenda mbele daima, almuradi ni kazi ya Mungu Mwenyewe na njia ya kweli, hakika itamiliki na kuonyesha sifa tatu zilizotajwa. Hiyo ni kusema, njia ya kweli hakika itakuwa na kazi ya Roho Mtakatifu, itatoa ukweli, na itawafanya watu kupata ufahamu mkubwa zaidi wa Mungu na kuwaleta karibu zaidi na Yeye. Kwa hiyo, tukipambanua njia ya kweli kwa kupima viwango hivi vitatu, tutaweza kutofautisha yale ya kweli na ya uongo, hivyo tutaweza kwenda sambamba na kazi ya Mungu ya sasa kwa wakati wa kufaa, kupata ukweli, njia, na uzima, na vile vile kupata ahadi kubwa zaidi na baraka za Mungu.

Katika siku hizi za mwisho, Mungu anatekeleza kazi mpya tena, ambayo inahusisha kutoa maneno Yake ili kufanya kazi Yake ya hukumu na utakaso juu ya wanadamu waliopotoka. Kazi hii inafanywa kulingana na mpango Wake na inategemea mahitaji halisi ya watu wa siku za mwisho. Ni kazi mpya, ya juu zaidi iliyotegemezwa kwa msingi wa kazi ya Bwana Yesu. Tukitafuta na kuchunguza kwa uangalifu na moyo wa utulivu, tunaweza kuona kwamba hatua hii ya kazi mpya ya Mungu haiwi na kazi ya Roho Mtakatifu tu, lakini pia hutoa ukweli na inaweza kuturuhusu kuwa na ufahamu zaidi wa kweli, mpana, na wa vitendo wa tabia ya Mungu na yote ambayo Mungu anayo na aliyo. Hapa chini, tutafanya ushirika kuhusu uzoefu wetu na ufahamu wa kazi ya Mungu katika siku za mwisho ukitegemezwa viwango vitatu vilivyojadiliwa awali vya kutathmini njia ya kweli.

Kwanza, njia ya kweli ina kazi ya Roho Mtakatifu. Mwenyezi Mungu amekuja na kuanzisha Enzi ya Ufalme, alitekeleza kazi mpya ya hukumu kuanzia na nyumba ya Mungu, akatoa neno Lake kuwahukumu na kuwatakasa watu, na Aliwaruzuku wanadamu ruzuku mpya za uhai. Waumini miongoni mwa kila dhehebu, mmoja baada ya mwingine, wamerudi kwa Mwenyezi Mungu chini ya jina Lake. Bila kujali jinsi mwanadamu alipinga au ni vizuizi vipi vilivyoonekana, injili ya Mungu ya siku ya mwisho bado imeenda mbele kama mawimbi ya bahari na kuenea kote China bara. Watu wote wanamiminika kwa mlima mtakatifu kwa sherehe yenye furaha. Ingawa sote tulikuja kutoka kwa madhehebu tofauti, sisi bado tuna uwezo wa kuishi kwa umoja pamoja na kusaidiana. Hakuna magenge hapa na maisha ya kanisa yanafurika kwa uchangamfu. Ndugu wa kiume na wa kike hapa wanahisi kuwa mikutano yetu kamwe haitoshi, na kuna nyimbo za kuimba na kufurahia na sala zinazotupa nuru. Kila wakati tunapokusanyika sisi wote tunaweza kupata ruzuku mpya kutoka kwa neno la Mwenyezi Mungu, tunaweza kutambua mapungufu yetu wenyewe, na kutoka kwa neno la Mungu sisi hupata njia ya kutenda. Tunaweza kuishi pamoja kwa kawaida na kupendana kwa mujibu wa neno la Mungu. Tunapokabiliwa na maoni tofauti, sote tunaweza kuweka kando maoni yetu wenyewe na kusikiliza kwa makini mawazo ya watu wengine. Wakati upotovu unafunuliwa, tunaweza kujiwazia na kujichunguza kwa msingi wa neno la Mungu. Tunapofanya mambo yanayodhuru maslahi ya kanisa, tuna ujasiri wa kukabiliana na ukweli wa mambo na kukubali kupogolewa na kushughulikiwa, na tunajitoa kwa mamlaka ya ukweli wa maneno ya Mungu katika Kanisa; ndugu zetu wa kiume na wa kike wamejawa na imani, wanaweza kuwa na agizo la Mungu kwa kujitolea, na kutelekeza anasa za mwili kwa ajili ya kazi ya kueneza injili ya ufalme ya Mungu kwa mioyo yetu yote. Bila kujali jinsi tunavyotendewa na madhehebu mbalimbali, au kama tunakataliwa, kuteswa, kupigwa, au kulaaniwa, tuko tayari kuvumilia shida yoyote na tunaendelea kama kawaida kuihubiri injili ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho ili kufanya mapenzi ya Mungu. Leo, wateule wa Mungu wamepitia hukumu na kuadibu kwa Mungu kwa miaka mingi, tabia zao za maisha zimebadilika kwa viwango tofauti, na wateule wengi wa Mungu wameandika makala na nyimbo za kidini zinazodhibitisha uzoefu wa kweli wa kile ambacho wamepata kupitia uzoefu wao wa kazi ya Mungu na kuzipakua kwa mtandao ili kumshuhudia Mungu, nyingi ambazo zimetengenezwa kuwa filamu na video. Makala, nyimbo na filamu hizi zinashuhudia mabadiliko ya kweli katika tabia ya maisha ya wateule wa Mungu, na zinashuhudia ufahamu wa wateule wa Mungu wa ukweli na maarifa ya uaminifu ya Mungu. Ni ushuhuda wa washindi. Je, idadi inayoongezeka daima ya ushuhuda kama huu siyo matokeo ya kazi ya Mungu ya hukumu na kuadibu? Bila kazi ya Roho Mtakatifu, ni nani angeweza kupata matokeo kama hayo? Mtu anaweza kuona mamlaka na nguvu za Mwenyezi Mungu kutokana na uzoefu na ushuhuda wa ndugu zetu wa kiume na wa kike. Kazi ya Mwenyezi Mungu ina kazi ya Roho Mtakatifu. Lakini kwa madhehebu mbalimbali ambayo hayajafuata kazi mpya wa Mungu, wale ambao wanahubiri hawana mahubiri, waumini wako hasi na wadhaifu, na imani yao ni baridi. Ni wenye wivu na wa mkabala, wanaunda makundi, na ingawa wanaweza kuwa wakifanya kazi ile ile, siyo kwa sababu sawa. Hili linatosha kuthibitisha kuwa jumuiya ya kidini tayari inakosa kazi ya Roho Mtakatifu. Kwa sababu Kanisa la Mwenyezi Mungu lina kazi ya Roho Mtakatifu, kwa hivyo huwa linaonekana likiwa na uchangamfu, wakati madhehebu mbalimbali hayana mvuto, ni ya ukiwa, na yamepoteza kazi ya Roho Mtakatifu, yakiwa tofauti kabisa na Kanisa ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo, ni dhahiri ni njia ipi iliyo ya kweli na ni ipi ambayo ni njia ya zamani.

Pili, njia ya kweli ina ukweli, inaweza kuashiria kwa watu njia ya matendo katika enzi mpya na inaweza kuwaruhusu watu kupata ruzuku mpya kwa ajili ya maisha. Tabia za maisha yao ya hupitia mabadiliko zaidi na zaidi na ubinadamu wao huwa wa kawaida zaidi na zaidi. Katika kazi Yake ya siku za mwisho, Mwenyezi Mungu hutoa ukweli mwingi katika nyanja mbalimbali. Haya ni pamoja na ukweli kuhusu kufahamu kazi ya Mungu na pia ukweli wa jinsi ya kutenda na kuingia katika enzi mpya. Kwa mfano haya ni pamoja na: Madhumuni ya usimamizi wa Mungu; kanuni ya Kazi Yake; ukweli wa ndani wa kazi ya Mungu kwenye Enzi ya Sheria na Enzi ya Neema, jinsi Mungu hufanya kazi Yake ya hukumu; umuhimu wa Mungu kupata mwili; jinsi wanadamu wameendelea hadi siku ya leo; jinsi Shetani huwapotoa wanadamu; jinsi Mungu huwaokoa wanadamu; vile hatima ya wanadamu ya baadaye itakavyokuwa; vile mwisho utakavyokuwa kwa aina mbalimbali za watu; ni maoni gani waumini wanapaswa kuwa nayo; jinsi ya kutekeleza wajibu wa mtu kwa uaminifu; jinsi ya kuwa mtu mwaminifu; jinsi mwanadamu anavyopaswa kuishi kwa kudhibitisha ubinadamu wa kawaida; jinsi ya kumtumikia Mungu kwa njia ambayo huyaridhisha malengo Yake; na jinsi ya kupata utii na upendo wa kweli kwa Mungu. Utoaji wa ukweli huu na Mwenyezi Mungu huwaruhusu watu kuwa na ufahamu bora zaidi wa kazi ya Mungu na tabia Yake, na pia kuwaruhusu kuwa na ufahamu bora juu wa asili na dutu yao na ukweli wa upotovu wao. Zaidi ya hayo, ukweli huu huwaruhusu watu kuona wazi njia ambayo lazima wafuate ilikubadilisha tabia zao. Kupitia kwa kupata uzoefu wa hukumu na kuadibu kwa Mungu,, watu hatimaye huja kuelewa mchanganyiko wa vipengele vya imani yao ya zamani na kutambua kuwa hata kama wamepokea ukombozi wa Mungu na neema kubwa, hata hivyo bado wao hutamani sana kupanga hila kwa ajili ya radhi zaidi za kimwili na baraka za mali kutoka kwa Mungu na kufanikisha ustawi wa ndoto zao kupitia kwa Mungu. Zaidi ya hayo, hata kama wao hushughulika wakifanya kazi kwa ajili ya Mungu, wanaifanya kwa ajili ya kubarikiwa na kupewa taji. Wao hufanya hivyo kwa sababu ya umaarufu wa kibinafsi na faida Huwa hawafanyi mambo haya ili kutimiza wajibu wao kama kiumbe aliyeumbwa. Bila kujali ni kiasi gani cha neema au ni baraka ngapi watu hupata kutoka kwa Mungu, kama chochote Mungu hufanya hukosa kwa njia fulani ndogo kuridhisha dhana zao, mara moja wao hupinga na kumlalamikia Mungu. Wao hata huenda kwa kadiri ya kuwa wapinzani wa Mungu hadharani au hata kumtelekeza Mungu. Watu walilipoteza zamani sana dhamiri uwezo wao wa awali wa kuwa na fikira za kirazini mbele ya Mungu. Watu walikuwa tumepotoshwa sana na Shetani kiasi kwamba wamepoteza kabisa mfanano wao wa binadamu. Ukweli uliotolewa na Mwenyezi Mungu huwaruhusu watu kuwa na ufahamu wa kweli wa upotovu wao wenyewe na huwaonyesha kwamba wao ni wenye ubinafsi, wenye kustahili dharau, na wasio na ubinadamu. Wakati huo huo, anapata kuelewa umuhimu wa kazi ya wokovu ya Mungu ambayo wao hufanyiwa, na vile vile nia angalifu na karimu za Mungu na juhudi ya bidii na thamani iliyolipwa ili kumwokoa mwanadamu. Kwa njia hii roho za watu zinaanza kuamka kidogo kidogo na dhamira yao na uwezo wa kufikiri kirazini uaanza kurejeshwa siku baada ya siku. Watu hawatafuti tena kuiridhisha miili yao wenyewe na hawafanyi mapatano na Mungu tena. Badala yake, wanatafuta tu kutosheleza nia za Mungu na kutoa kwa Mungu kila kitu walicho nacho. Kwa njia hii, watu, kama viumbe walioumbwa, hatua kwa hatua tunarejesha uhusiano wa kawaida na Muumba. Wanakuwa wa kumpenda Mungu zaidi na zaidi, watiifu na watu wa kuabudu zaidi na zaidi, na hatimaye wanaanza kuonekana zaidi jinsi mtu ni lazima awe. Kwa kifupi, Mwenyezi Mungu hutupa ukweli tunaouhitaji kwa dharura sana kuelewa ili kupata wokovu katika imani yetu kwa Mungu. Yeye hutuonyesha mwelekeo wa njia katika enzi mpya na Yeye hutukubalia kupata riziki halisi zaidi tunazohitaji kwa uhai. Haya yote yanathibitisha kuwa njia ya Mwenyezi Mungu ndiyo njia ya kweli.

Tatu, njia ya kweli humpa mwanadamu ufahamu mpya na wa utendaji kuhusu Mungu, na kumwezesha mwanadamu kumpenda Mungu kwa kuongezea. Ndugu, kama mnaweza kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu ninyi binafsi na kwa kweli mwasiliane na wale ambao wamekubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, si vigumu kugundua kwamba ndugu wa Kanisa la Mwenyezi Mungu wamepata maarifa mapya na ufahamu tofauti kidogo zaidi kuhusu Mungu kupitia njia ambayo wanatafuta ukweli wa Mwenyezi Mungu. Kwa kupitia hukumu na kuadibu kwa Mwenyezi Mungu, watu wanaelewa tabia ya haki ya Mungu na kuona kwamba tabia ya asili ya Mungu haina upendo na rehema tu, lakini pia uadhama na hasira, na tabia Yake haivumilii kosa la wanadamu. Kwa kupata uzoefu wa kazi ya Mwenyezi Mungu, watu huona kwamba Mungu humwokoa mwanadamu sio tu kwa kuonyesha ukweli ili kumhukumu, lakini pia kwa kupanga kila aina za hali na mazingira kuwafichua watu, na hatimaye kutumia maafa kuwasafisha na kuwatakasa watu. Wakati uo huo, watu pia wanaona jinsi Mungu huwafichua wapinga Kristo, watenda maovu, na wasioamini katika kanisa, na jinsi Mungu hutumia werevu kwa joka kubwa jekundu ili kufanya huduma kwa ajili ya kukamilisha wateule Wake. Hivyo watu hupata maarifa kiasi ya utendaji kuhusu uweza, hekima, hali ya ajabu na kutoeleweka kwa Mungu. Zaidi ya hayo, pia wanapata ufahamu wa utendaji zaidi kuhusu nia karimu za Mungu katika kuwaokoa wanadamu, upendo Wake wa kweli kwa wanadamu, na dutu Yake ya utakatifu na uzuri. Kupata uzoefu wa kazi na neno la Mwenyezi Mungu husaidia kutatua dhana nyingi za uongo ambazo watu wamekuwa nazo kuhusu Mungu na huwasaidia kutambua kwamba Mungu sio tu Mungu wa Waisraeli, ila pia Mungu wa mataifa yote ya wasio Wayahudi, na Mungu wa viumbe vyote. Watu pia wanaelewa kwamba kazi ya Mungu ni mpya daima na wala siyo nzee na haifungwi na sheria zozote. Kwa njia nyingi, watu huona kwamba kuwa vipengele vingi vipendezavyo vya Mungu, kwamba upendo wa Mungu kwa wanadamu ni mkuu na wa utendaji, na baada ya hapo upendo wa kweli kwa Mungu unafanyizwa mioyoni mwao, wanatamani kufuatilia ukweli, na wanajitahidi kwa nguvu zao zote kutimiza wajibu wao kama viumbe na kumridhisha Mungu. Kutokana na hili, tunajua kwamba kazi na maneno ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho yanaweza kumpa mwanadamu ufahamu wa kina zaidi kuhusu Mungu kuliko jinsi ilivyowezekana katika Enzi ya Neema; ni ufahamu ulio wa utendaji zaidi na pia pana zaidi. Uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu unakuwa wa karibu zaidi kadiri ufahamu wa mwanadamu kuhusu Mungu unavyokuwa wa kina. Ni kazi ya Mungu mwenyewe pekee inayoweza kuwa na matokeo haya, na ni Mungu Mwenyewe pekee anaweza kutoa tabia Yake na chote Anacho na alicho kwa wanadamu. Ni hakika kwamba njia ya Mwenyezi Mungu ni njia ya kweli.

Kwa muhtasari, Umeme wa Mashariki, ambao umepingwa na kushutumiwa na viongozi wa kidini, ni Bwana Yesu, ambaye amerejea kwa mwili katika siku za mwisho–ni Mungu Mwenyewe wa kipekee. Kwa hiyo, bila kujali jinsi madhehebu mbalimbali huupinga na kuushambuliwa na bila kujali jinsi serikali ya CCP hubuni uvumi ili kuushutumu na kuusingizia, hayajaweza kuzuia hata kidogo upanuzi wa kazi ya Mungu katika siku za mwisho. Kwa takriban miaka ishirini tu, injili ya ufalme ya Mwenyezi Mungu imeenea kotekote katika China bara nzima. Neno la Mungu na jina la Mungu yameenea kwa kaya nyingi sana. Miongoni mwa madhehebu mbalimbali, wale ambao huufuata ukweli na kwa kweli wanataka Mungu wamerudi kwa Mwenyezi Mungu. Watu milioni nyingi wanafurahia neno la Mungu, wakipokea hukumu ya Mungu, utakaso, wokovu na ukamilifu, na wakiyasifu matendo ya ajabu ya Mungu. Mungu ametengeneza kundi la washindi nchini China na amechuma kundi la watu ambao ni wa moyo mmoja na akili moja naye. Kazi ya Mungu itamalizika punde kwa kutukuzwa Kwake na inaenda kwa kasi kutoka Mashariki–China hadi dunia ya magharibi na Kanisa la Mwenyezi Mungu limeanzisha matawi katika idadi kubwa ya nchi, ambalo ni utimizaji kamili wa unabii wa Bwana Yesu, “Kwa kuwa kama umeme unavyotokea mashariki, na kumulika pia magharibi; ujio wa Mwana wa Adamu utakawa hivyo pia(Mathayo 24:27). Wenzangu wa kiroho, wekeni chini kwa haraka dhana zenu za kufikiriwa na badala yake mtafute kusikia sauti ya Mungu, tafadhali njooni mbele ya Mungu kwa dhati: Mwenyezi Mungu anasubiri kurejea kwenu!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp