Wimbo wa Ufalme

Umati wa watu Wangu unanishangilia, umati wa watu Wangu unanisifu; midomo isiyohesabika inalitaja jina la Mungu mmoja wa kweli, watu wasiohesabika wanayainua macho yao, wakiangalia mbali ili kuvitazama vitendo Vyangu. Ufalme unashuka juu ya dunia ya mwanadamu, nafsi Yangu ni yenye fahari na utele. Nani asingesherehekea kwa ajili ya hili? Ni nani asingecheza kwa furaha? Ee Sayuni! Inua bendera yako ya ushindi unisherehekee! Imba wimbo wako wa ushindi ili ulitangaze jina Langu takatifu! Viumbe wote hadi miisho ya dunia! Harakisheni kujitakasa ili muweze kufanywa kuwa sadaka Kwangu! Thurea ya nyota juu! Rudini kwenye maeneo yenu kwa haraka ili muonyeshe nguvu Yangu kuu katika anga! Ninalitoa sikio Langu kusikiliza kwa makini sauti za watu Wangu duniani, wanaomimina upendo na uchaji wao usio na mwisho kwa ajili Yangu kwa nyimbo! Katika siku hii, uumbaji wote unapotiwa nguvu tena, Ninashuka katika dunia ya mwanadamu. Katika wakati huu hasa, maua yanachanua kwa wingi, ndege wote wanaimba kwa sauti moja, vitu vyote vinajawa na furaha tele! Katikati ya saluti za mizinga ya ufalme, ufalme wa Shetani unaanguka, ukiangamizwa katika mngurumo wa wimbo wa ufalme, usiinuke tena kamwe!

Nani duniani anathubutu kuinuka na kupinga? Ninaposhuka duniani Ninaleta moto, Ninaleta ghadhabu, Ninaleta majanga yote. Falme za dunia sasa ni ufalme Wangu! Juu angani, mawingu yanagaagaa na kujongea kama mawimbi; chini ya anga, maziwa na mito inasonga mbele kwa mawimbi na kutoa muziki unaogusa sana. Wanyama wanaopumzika wanaibuka kutoka kwenye matundu yao, na watu Wangu wasiohesabika wanaamshwa na Mimi kutoka usingizini mwao. Siku ambayo watu Wangu wasiohesabika wameingojea hatimaye imefika! Wananitolea nyimbo nzuri kabisa!

Katika wakati huu mzuri, katika wakati huu wa kusisimua,

sifa zinasikika kila mahali, juu mbinguni na chini duniani. Nani asingesisimka kwa ajili ya hili?

Ni moyo wa nani usingechangamka? Ni nani asingelia kwa sababu ya tukio hili?

Anga si anga ya zamani, sasa ni anga ya ufalme.

Dunia si dunia ya awali, sasa ni nchi takatifu.

Baada ya mvua kubwa kupita, ulimwengu mchafu wa kale unafanywa upya kabisa.

Milima inabadilika … maji yanabadilika …

watu pia wanabadilika … vitu vyote vinabadilika….

Aa, milima iliyo mitulivu! Inukeni na mnichezee!

Aa, maji yaliyotuama! Endeleeni kutiririka!

Ninyi mnaoota ndoto! Jiinueni na mfuatilie!

Nimekuja … Mimi ni Mfalme….

Wote watauona kwa macho yao wenyewe uso Wangu, wataisikia sauti Yangu kwa masikio yao wenyewe,

watapitia wao wenyewe maisha ya ufalme….

Matamu sana… mazuri sana….

Yasiyosahaulika … yasiyoweza kusahaulika….


Katika mwako wa ghadhabu Yangu, joka kubwa jekundu linapambana;

katika hukumu Yangu adhimu, pepo wanaonyesha sura zao za kweli;

kwa maneno Yangu makali, watu wote wanaona aibu sana, na hawana popote pa kujificha.

Wanakumbuka zamani, jinsi walivyonidhihaki na kunikejeli,

jinsi hakukuwahi kuwa na wakati ambapo hawakujiringa, hakukuwa kamwe na wakati ambapo hawakuasi dhidi Yangu.

Lakini leo, ni nani asiyelia? Ni nani asiyejishutumu?

Ulimwengu dunia wote umejawa na kilio …

umejaa sauti za kushangilia … umejaa sauti za vicheko….

Raha isiyofananishwa … raha isiyo na kifani….


Mvua ya rasharasha inatarakanya … theluji nzito inapepesuka….

Ndani ya watu, huzuni na furaha zinachanganyika … baadhi wakicheka …

baadhi wakilia … na baadhi wakishangilia….

Kana kwamba watu wote wamesahau … ikiwa haya ni majira ya kuchipua yaliyojaa mvua na mawingu,

majira ya joto yenye maua yanayochanua, majira ya kupukutika kwa majani yenye mavuno mengi,

au majira ya baridi yaliyo baridi kama barafu na jalidi, hakuna anayejua….

Angani mawingu yanaenda pepe, duniani bahari zinavurugwa.

Wana Wangu wasiohesabika wanapunga mikono yao … watu Wangu wasiohesabika wanasogeza miguu yao wakicheza….

Malaika wanafanya kazi … malaika wanachunga….

Watu wote duniani wanashughulika, na vitu vyote duniani vinazidishwa.

Iliyotangulia: Sura ya 10

Inayofuata: Sura ya 11

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp