211 Kuna Maumivu Ndani ya Moyo Wangu

1

Kuna maumivu ndani kabisa ya moyo wangu. Kila ninapofikiria kuhusu zamani ni kama kisu kilipinda moyoni mwangu.

Wakati mmoja nilimpinga na kumkufuru Kristo. Nilimwamini Mungu lakini sikumjua, na nikampinga.

Nilimshuhudia Kristo akionyesha ukweli lakini bado nilimkana, mimi si tofauti na Mafarisayo.

Sitasahau kamwe somo hili lililoandikwa kwa damu. Nimeachwa na toba na majuto ya milele.

2

Nilimwamini Bwana kwa miaka mingi lakini sikufuatilia ukweli. Nilijizatiti kwa maarifa ya kibiblia ili kuringa.

Nilizungumza juu ya nadharia za teolojia ili kuwafanya wengine waniabudu na kuniheshimu. Nilijitahidi kwa ajili ya baraka na thawabu.

Nilikuwa mbinafsi na mwovu, bila kujali kamwe mapenzi ya Mungu. Nilipiga kelele nyingi juu ya kumpendeza Mungu lakini sikutenda ukweli.

Niliapa kuwa mwaminifu kwa Mungu kwa maneno lakini sikutekeleza wajibu wangu. Nilikuwa mcha Mungu kwa nje lakini sikumtii Mungu.

3

Hukumu na kuadibu kwa Mungu vinanifanya nisujudu. Natetemeka kwa hofu ninapoona tabia ya Mungu ya haki.

Nachukia upotovu wangu wa kina na ukatili. Nimetenda dhambi nyingi sana na nimeuvunja moyo wa Mungu.

Kwa yote niliyoyafanya ningeangamizwa na Mungu muda mrefu uliopita. Lakini Mungu ni mvumilivu na mstahimilivu kwangu, Akanipa nafasi ya kutubu.

Kuona wokovu wa Mungu kunaujaza moyo wangu majuto. Nimeamua kutenda ukweli na kuishi kwa kudhihirisha mfano wa binadamu.

Niko tayari kutumia maisha yangu kwa ajili ya Mungu na kulipa mapenzi ya Mungu. Nitamtii Mungu na kumwabudu Mungu milele.

Iliyotangulia: 210 Matamanio ya Dhati ya Kutubu

Inayofuata: 212 Toba ya Dhati

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp