Neno la Mungu Lilibadilisha Mawazo na Mitazamo Yangu Mibaya

12/01/2018

Peihe Jiji la Xianning, Mkoa wa Hubei

Daima niliamini kwamba mimi na mume wangu tulipitia maisha yetu “na nyuso zetu kwa mchanga na migongo yetu kwa jua” kwa sababu hatukusoma vya kutosha tulipokuwa vijana, na kwa sababu hatukuwa na elimu. Ndiyo sababu niliamua kuwa bila kujali ni kwa ugumu gani au kiasi gani ningeteseka, ningewapeleka wanangu wa kiume na binti zangu shuleni ili waweze kufanikisha kitu fulani, na hawangelazimika kufuata nyayo zetu. Hilo likituongoza, mume wangu nami tulikula na kuvaa pasipo anasa na tulitafuta pesa kwa shida ili kumpeleka binti yetu mkubwa kwa chuo cha ufundi na mwana wetu wa kiume mkubwa kwa chuo kikuu. Lakini bado tulikuwa na watoto wengine wawili, hivyo kuwapeleka chuo kikuu, ilibidi mume wangu kutoka nyumbani kwenda kufanya kazi kwa miaka mingi kila kipindi, na wala sikuwa bila kazi; nilitunza mashamba na nguruwe nyumbani kutoka mapambazuko hadi magharibi. Wakati wowote kazi ya shamba ilipochosha mno, nilitamani ningeiacha tu. Lakini kwa kufikiria jinsi jamii ilivyo na ushindani leo, vile kama singewapeleka wanangu shuleni, wangekuwa na mategemeo tu katika kazi ya matope kama mimi, vile wasingeweza kamwe kufanikisha chochote na wangeangaliwa kwa dharau, na kwamba ni kwa kuhitimu kuingia chuo kikuu tu ndio wangeweza kupata kazi nzuri au kuwa mtu mwenye madaraka rasmi, kufanikisha kitu fulani, kupata mategemeo yao ya baadaye, na kutupatia utukufu, maumivu na uchovu nilivyonipata vilionekana kuwa na thamani. Na hivyo, kila siku nilipoamka, nilijihusisha sana na kazi yangu kiasi kwamba mara nyingi sikuwa na wakati wa kula na kunywa maneno ya Mungu au maisha ya kawaida ya kiroho, na sembuse wakati wa maisha ya kawaida kanisani au kutekeleza wajibu wangu, lakini sikulitilia maanani, na niliendelea kufanya kazi kwa bidii sana kwa sababu ya watoto wangu … hadi hivi karibuni, niliposikia maneno haya kutoka kwa ushirika wa Mungu: “Kuwahusu watoto, wazazi wote hutumaini kwamba watoto wao watapata elimu ya juu na kwamba siku moja wataendelea, wawe na nafasi katika jamii na kuwa na mapato thabiti na ushawishi—kwa njia hiyo wanaweza kuheshimu nasaba. Kila mtu ana mtazamo huu. Ni mtazamo sahihi kutumaini kwamba ‘mwana wa kiume atakuwa joka, binti anakuwa finiksi’? Kila mtu hutaka watoto wake waende katika chuo kikuu cha kifahari na kisha kufuatilia masomo ya juu, akidhani kwamba baada ya kupata digrii wataonekana tofauti na wengine. Hii ni kwa sababu ndani ya mioyo yao, kila mtu huabudu elimu, akiamini kwamba ‘Thamani ya ufuatiliaji mwingine ni ndogo, masomo ya vitabu huwa bora zaidi kuliko yote.’ Aidha, mashindano katika jamii ya kisasa ni makali kabisa, na bila shahada hujahakikishiwa kuweza hata kujimudu. Hivi ndivyo kila mtu hulifikiria jambo hili. … Lakini uliwaza kuhusu ni sumu kiasi gani na ni mawazo mangapi na nadharia za Shetani vitakavyoingizwa ndani yao baada ya kupata elimu ya aina hiyo? … Mpaka siku moja, watoto wako wanarudi na unawaambia kuhusu kumwamini Mungu, na wanaonyesha hali ya kutojali. Baada ya kuwaambia juu ya ukweli, wanasema wewe ni mpumbavu na wanacheka, na wanakejeli unachokisema. Wakati huo utafikiri kuwa kuwapeleka watoto wako katika shule hizo kupata elimu ya aina hiyo kulikuwa kuchagua njia mbaya, lakini hakutakuwa na muda wa majuto. … linapohusu watoto wao, hakuna mtu anayekubali kuwaleta mbele ya Mungu kukubali kabisa maoni na mawazo ambayo Mungu huhitaji, au kuwa aina ya mtu ambaye Mungu huhitaji. Watu hawapendi kufanya hili na hawathubutu kulifanya. Wanaogopa kwamba kama wakilifanya, watoto wao hawataweza kupata riziki au kuwa na mustakabali katika jamii. Mtazamo huu unathibitisha nini? Unathibitisha kuwa wanadamu hawana haja, imani na zaidi ya hayo hawana imani ya kweli katika ukweli au katika Mungu. Kile ambacho wanadamu hutegemea na kuabudu mioyoni mwao bado ni dunia hii, wakidhani kwamba watu ambao huiacha dunia hii hawataendelea kuishi. … mawazo na mitazamo hii ya binadamu ina upinzani kwa Mungu, ni ya usaliti na ya kumkataa Mungu, na hayapatani na ukweli(“Ni kwa Kutambua Maoni Yako Yaliyopotoka Tu Ndipo Unapoweza Kujijua Mwenyewe” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Kila moja ya maneno ya Mungu lilinisisimua mno. Miaka mingi sana ya kuweka akiba kwa uchungu na ugumu, kazi ngumu, kuacha kila kitu ili watoto wangu waweze kwenda chuo kikuu, na kwa nini? Kwa sababu niliamini “Thamani ya ukimbizaji mwingine ni ndogo, utafiti wa vitabu huwafanya bora wote” ya Shetani ilikuwa kanuni ya kusalia! Chini ya ushawishi wa sumu ya Shetani, niliweka elimu juu ya mambo mengine yote, na nikafikiri ni kuwa na elimu tu mtu anapoweza kujitokeza, kufanikisha mambo, kuwa na mategemeo, na kupata hadhi katika jamii. Nilidhani kuwa wale wasiokuwa na elimu walikuwa wa kiwango cha chini kabisa cha kijamii wanaostahili dharau, wa chini kuliko wote. Hivyo, kuhakikisha kuwa watoto wangu wangeweza kufanikiwa duniani na kuepuka maisha “wakiwa na nyuso zao kwa mchanga na migongo yao kwa jua,” nilifanya kila kitu nilichoweza ili kuwapeleka kusoma na kuwapa elimu ya juu. Kwa miaka mingi sana, niliweka lengo langu kabla ya kitu kingine chochote ndani ya moyo wangu, wakati ule ule nilizika maneno ya Mungu, wajibu wangu, na wokovu wangu nyuma ya mawazo yangu. Sumu ya Shetani iliniumiza kwa kina sana! Ingawa nimemfuata Mungu kwa miaka mingi, sijaupata ukweli, na maoni yangu hayajabadilika hata kidogo. Ninachokiabudu bado ni elimu, na kile ninachokitamani sana na kukitegemea ni Shetani. Mimi bado ni asiyeamini ambaye hufuatilia mielekeo ya kidunia na kumpinga Mungu!

Katika ushirika wa Mungu, pia nilikuja kutambua kwamba Shetani hutumia mafunzo na kusoma kuwadanganya waipokee elimu yake na kuikubali sumu yake na fikra katika mawazo yao, na mara sumu inapowasilishwa, watu humilikiwa kabisa na fikira na hoja za uongo za wakanamungu ambazo humkana na kumpinga Mungu, ambayo ndiyo jinsi Shetani hutimiza malengo yake ya kuwapotosha na kuwameza wanadamu. Kwa sababu sikuweza kubaini udanganyifu wa Shetani, niliwatuma watoto wangu kwa shauku kupokea elimu ya Shetani, kuwapeleka kwa uovu bila kufikiria jinsi ya kuwaleta mbele ya Mungu au kuwafanya wakubali ukweli ambao hutoka kwa Mungu na kuwafanya waishi kulingana na matakwa ya Mungu. Hivi karibuni, mwanangu wa kiume alihitimu kutoka chuo kikuu kimoja cha kifahari, na wakati aliporudi nyumbani, ingawa amepata elimu nyingi, amejazwa na uongo na uvumi wote wa Shetani. Wakati ninapotaja chochote kuhusu imani katika Mungu, yeye hunionyesha kila aina za elimu ya kisayansi na nadharia kunikanusha, yeye huniita nisiyesoma, mjinga, na nisiyetambuzi, yeye husema ni lazima niamini katika sayansi…. Ni wakati nilipokuja kulijutia tu nilipotambua kuwa kuwapeleka watoto wangu kupata elimu ya juu lilikuwa kosa. Uhalisi hatimaye ulinifanya nielewe kwamba utamaduni wote wa kidunia na elimu zinazompinga Mungu na kinyume cha ukweli. Ni vyombo ambavyo Shetani hutumia kuwapotosha na kuwadhibiti watu. Jinsi elimu wapokeayo watu ilivyo ya juu, ndivyo elimu wanayofahamu inavyozidi, ndivyo sumu ya Shetani iliyo ndani yao inavyozidi, ndivyo wanavyozidi kuwa mbali na Mungu, ndivyo wanavyozidi kuwa adui za Mungu, na ndivyo inavyozidi kuwa vigumu kwao kupokea wokovu wa Mungu. Mtu anaweza kusema kuwa jinsi mtu anavyosoma vitabu vingi ndivyo anavyozidi kuwa na elimu, ndivyo upinzani wake kwa Mungu unavyozidi kuwa wa kina sana. Elimu ni jambo la hatari sana!

Kupata nuru kutoka kwa Mungu hatimaye kulinifanya kuelewa kuwa “Thamani ya ukimbizaji mwingine ni ndogo, utafiti wa vitabu huwafanya bora wote” ni uwongo wa Shetani, ni mojawapo tu ya uongo wa Shetani kuwadanganya, kuwalaghai, na kuwapotosha watu. Pia nilielewa kuwa kuwapeleka watoto wangu kwa shule ya Shetani kulikuwa sawa na kuwatupa katika lindi kuu la kifo na moto wa kuzimu. Mungu, sitaki kudanganywa na kuumizwa na Shetani tena, nataka kufuatilia ukweli na kubadili maoni yangu yenye uongo, nataka maneno Yako kuwa msingi wa kuwepo kwangu, na ninataka kuwaleta watoto wangu wawili wadogo zaidi mbele Yako, ili waweze kupokea wokovu Wako na kuwa jinsi wanadamu wanapaswa kuwa.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Uzinduzi wa Kiroho wa Mkristo

Na Lingwu, Japani Mimi ni mtoto wa miaka ya themanini, na nilizaliwa katika kaya ya kawaida ya mkulima. Kakangu mkubwa alikuwa mgonjwa na...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp