292 Upendo wa Mungu Umeuyeyusha Moyo Wangu

1

Ee Mungu! Nimesikia sauti Yako na nimerudi mbele Yako.

Maneno Yako yananifichua na kunihukumu, na nimeona jinsi nimepotoka kwa kina.

Nilimwamini Bwana ili nizawadiwe tu, niliteseka ili nipate baraka za ufalme wa mbinguni.

Mara nyingi nilikataa wokovu Wako; hata nilifanya hukumu kukuhusu na kukupinga.

Bado Ulinisamehe, lakini nilikuletea uchungu mwingi.

Nilidharau jinsi moyo wangu ulivyokuwa mgumu, na jinsi nilikosa ubinadamu.

2

Ee Mungu! Hukumu ya maneno Yako imeuamsha moyo wangu.

Mara nyingi, nikikabiliwa na upendo Wako, umejawa na maumivu na majuto.

Wakati wa kuadibiwa kwangu, Wewe uko kando yangu; wakati wa kusafishwa kwangu, moyo Wako unauma kwa ajili yangu.

Maneno Yako hunitolea kile ninachokosa; nikiwa na huzuni, maneno Yako hunifariji.

Mimi ni mchafu na mpotovu sana, na ninajua kwa kina kuwa sistahili upendo Wako.

Mwasi na asiyetii sana, napaswa kukubali hukumu na utakaso Wako zaidi.

3

Ee Mungu! Kupata mwili Kwako kunafichua upendo Wako.

Unavumilia udhalilishaji mkubwa ili kuwaokoa wanadamu.

Unapitia maumivu ya kukataliwa na wanadamu, lakini kamwe Hulalamiki juu ya ukiwa wa ulimwengu.

Unanena na kufanya kazi, ukivumilia kila aina ya mateso, bila mahali pa kupumzisha kichwa Chako.

Hujawahi kufurahia furaha ya kifamilia. Hakuna anayekupa upendo hata kidogo.

Mnyenyekevu na Uliyejificha, Unaonyesha ukweli ili kuwatakasa na kuwapata watu.

4

Ee Mungu! Kwa uvumilivu Unangojea toba ya mwanadamu—nawezaje kuchelewa zaidi?

Sasa nimepitia upendo Wako na nitayadhukuru mapenzi Yako.

Niko tayari kuvumilia majaribu na usafishaji, na kuwa shahidi ili nikurudhishe.

Upendo Wako umeuyeyusha moyo wangu, nitakupenda kwa kweli na kukuishia.

Nimeamua kufuatilia ukweli na kuishi kwa kufuata maneno Yako.

Nitakupenda, kukufuata na kuwa na ushuhuda Kwako milele.

Iliyotangulia: 291 Upendo wa Mwenyezi Mungu Ndio Safi Zaidi

Inayofuata: 293 Mungu Pekee Ndiye Bora Zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp