43. Kupotea na Kurejea Tena

Na Xieli, Marekani

Nilikuja Marekani kufanya kazi kwa bidii kama vile ningeweza kutafuta maisha yenye furaha na hali ya juu ya maisha. Ingawa niliteseka kidogo kwa miaka michache ya kwanza, baada ya muda niliweza kuanzisha kampuni yangu mwenyewe, kupata gari langu mwenyewe, nyumba yangu mwenyewe, n.k. Mwishowe nilikuwa naishi maisha ya “furaha” ambayo niliyaota. Katika kipindi hiki, nilipata marafiki wachache; katika wakati wetu wa ziada tungeenda kula, kunywa, na kupata raha kiasi. Sote tulishirikiana vizuri pamoja, na nilidhani nimepata kundi nzuri la watu. Lakini kisha nilikuja kugundua kuwa wote walikuwa tu marafiki wa kunywa nao ambao hawakuwa na hata neno moja la maana la kusema, na nilipokuwa na wasiwasi au mwenye mfadhaiko hakuna hata mmoja wao ambaye ningeweza kwenda kushiriki naye shida zangu. Isitoshe, lakini walikula njama kuniibia: Mmoja wao alinidanganya kwamba mama yake huko Uchina alikuwa mgonjwa sana na nilipomkopesha pesa alipotea bila kujulikana aliko. Mwingine, kutoka katika mji wa nyumbani kwangu, alisema uwongo mwingi kwamba alihitaji ufadhili wa mradi na akanidanganya nikampa pesa fulani. Na hata mtu wa karibu na mpendwa sana kwangu—rafiki yangu wa kike—alinisaliti na kuniibia pesa nyingi ambazo zilinichukua miaka ya kujitahidi kwa bidii kukusanya. Ukatili wa watu hawa na kutokujali kwa jamii kuliniacha nikiwa mwenye huzuni na mwenye kukata tamaa. Kwa muda fulani nilipoteza imani ya kuendelea kuishi; moyo wangu ulikuwa tupu, na nilikuwa na uchungu na mwenye kutojiweza. Baada ya hayo, mara nyingi niliishia kula, kunywa na kula raha nijaze utupu uliokuwa ndani yangu, lakini nilijua kuwa raha hizi za muda mfupi za mwili hazingetatua mateso yangu ya kiroho hata kidogo.

Katika msimu wa kupukutika kwa majani wa 2015, kwa ajali ya majaliwa, nilifahamiana na mwanamke ambaye ni mke wangu hivi leo. Wakati huo alikuwa amekwisha kubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Aliposhiriki nami injili ya ufalme, kuwa na imani kulionekana bora na kuzuri kwangu, lakini kwa sababu nilikuwa na shughuli nyingi sana za kazi nikamwambia: “Sina wakati wa imani katika Mungu, lakini ikiwa unataka kuamini, endelea. Kujua moyoni mwangu kuwa Mungu yuko kunanitosha.” Siku moja miezi sita baadaye mke wangu alinifanya nitazame moja ya video kutoka katika Kanisa la Mwenyezi Mungu pamoja naye—Siku za Nuhu Zimekuja. Kile nilichokiona kwenye video kilinishtua sana: Wanapokabiliwa na maafa, wanadamu walikuwa wadogo na dhaifu, wasiweze kuhimili mapigo hata madogo. Nilihisi ghafla kuwa haijalishi kiasi cha pesa alicho nacho mtu, anafurahia starehe kiasi gani au hadhi yake ni ya juu kiasi gani, yote hayana maana. Mbele ya maafa, wakati kifo kinatujia, mambo haya yote hayana thamani na hayana maana. Kama maneno ya Mwenyezi Mungu yanavyosema: “Hata hivyo, lazima Nikuelezee kuwa wakati wa Nuhu, wanadamu walikuwa wamekula na kunywa, wakifunga ndoa na kupeana katika ndoa hadi kiwango ambacho Mungu asingevumilia kushuhudia, hivyo, Alituma chini mafuriko makubwa kuangamiza wanadamu na kuacha tu nyuma familia ya Nuhu ya watu wanane na aina yote ya ndege na wanyama. Katika siku za mwisho, hata hivyo, wale waliohifadhiwa na Mungu ni wale wote ambao wamekuwa waaminifu Kwake hadi mwisho(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Je, Ulikuwa Unajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu). “Kisha angalia enzi ya sasa: Hawa watu wenye haki kama Nuhu, ambao wangeweza kumwabudu Mungu na kuepuka uovu, wamekoma kuwepo. Lakini bado Mungu ana fadhili kwa mwanadamu huyu, na Anamsamehe mwanadamu wakati huu wa enzi ya mwisho. Mungu anawatafuta wanaomtaka Yeye ajitokeze. Anawatafuta wale wanaoweza kuyasikia maneno Yake, wale ambao hawajasahau agizo Lake na wanatoa mioyo na miili yao Kwake. Anawatafuta wale walio watiifu kama watoto wachanga mbele Yake, na hawampingi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 2: Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote). Katika maneno haya niliweza kuhisi umuhimu wa kusudi la Mungu la kuwaokoa wanadamu. Nilifikiria juu ya jinsi katika nyakati hizi hakuna mtu anayeonekana kupenda vitu chanya au kutamani kurudi kwa Mungu. Mioyo ya watu imejaa ubinafsi, kiburi, na hila. Kwa sababu ya umaarufu na faida, wanapanga na kula njama wao kwa wao, kudanganyana, na hata kuamua kuuana. Watu ni watumwa wa tamaa zao za kihisia, na mara kwa mara hukiuka maadili na wema na huzika dhamiri zao. Watu wamepoteza ubinadamu wote…. Kiwango cha upotovu wa wanadamu katika siku za mwisho kweli ni zaidi ya ule wa enzi ya Nuhu. Hata hivyo, Mungu hajawaangamiza kabisa wanadamu kwa sababu ya uovu na upotovu huu, lakini badala yake anashusha aina tofauti za majanga kuwaonya wanadamu na kutupa nafasi ya kumrudia Mungu. Nilipotafakari juu ya maneno ya Mungu, moyo wangu uliguswa sana na upendo wa Mungu. Nilifikiria pia kuhusu jinsi ulimwengu ulivyozidi kuwa mwovu na uliopotoka kila siku, majanga yalikuwa yanakua makubwa zaidi na zaidi, na juu ya jinsi Mungu anavyotoa hasira Yake juu ya wanadamu waovu na kuwaangamiza binadamu, pesa zote na hadhi ambayo nilikuwa nikifuatilia isingeweza kuniokoa. Ni kwa kuja mbele za Mungu na kutafuta ukweli tu ndipo mtu anaweza kupata ulinzi. Nilipofikiria yote haya kwa makini ilikuwa kama kuamka kutoka ndotoni—uwezo wangu wa kuelewa haraka bila kufikiria sana uliniambia kwamba ninapaswa kuja mbele za Mungu na kukubali wokovu Wake, kwani hii ndiyo njia pekee ya kuokolewa. Ikiwa ningepoteza nafasi yangu ya kufikia wokovu kwa sababu ya starehe za mwili za muda mfupi, hayo yangekuwa majuto ya maisha! Kwa sababu hiyo, mnamo Mei 2016 nilianza kumwamini Mungu na kushiriki katika mikutano ya kanisa.

Sio muda mrefu baada ya kupata imani yangu, nilikuwa nikipitiapitia mtandaoni na nikakutana na habari fulani hasi zikilishutumu na kulikashifu Kanisa la Mwenyezi Mungu. Kusoma habari hizo kuliniacha nikiwa nimeshangaa kwa muda. Je, huku “kuwafanya watu watoe pesa na kutoheshimu mipaka kati ya wanaume na wanawake” kulikuwa nini? Kile nilichosoma kilionekana kuwa cha busara, na kufanya iwe vigumu kutofautisha kati ya mema na mabaya, ukweli na uwongo. Nilielea katika kuchanganyikiwa, na moto mkali wa imani yangu katika Mungu ulizimwa papo hapo na mambo hayo mabaya ambayo nilikuwa nikisoma. Na wakati huo huo tu, nilimsikia mama mkwe wangu kwenye simu na mke wangu wakiongea juu ya kulitola kanisa pesa, jambo ambao lilinifanya niwe na mwelekeo zaidi wa kuamini kile nilichokuwa nikisoma mtandaoni. Baada ya hapo, nilimkomesha mama mkwe wangu kulitolea kanisa pesa na pia nikamhimiza mke wangu aache imani yake ili tusihadaiwe. Lakini hakunisikiliza hata kidogo, akaniambia kwa kauli moja: “Ukweli wa hali ilivyo si kama ulivyosoma mtandaoni. Vitu vilivyo mtandaoni vyote ni uvumi, vyote ni ushuhuda wa uwongo! …” Kisha akachukua kitabu cha maneno ya Mungu kushiriki nami, lakini tayari nilikuwa nimepofushwa na uvumi na sikuelewa chochote alichokuwa akisema. Sio muda mrefu baadaye, ndugu fulani walikuja nyumbani kwetu, lakini niliwaapuuza tu, hata hivyo. Kwa siku hizo chache nilikuwa naishi gizani, kila wakati nikihofu kuhusu mke wangu na mama mkwe kudanganywa. Nilikuwa na wasiwasi kila wakati—singeweza kula chakula, singeweza kulala vizuri usiku, na niliteswa kisaikolojia. Kuona jinsi ninavyoteseka, mke wangu alijaribu kushirikiana nami tena. Alifungua kitabu cha maneno ya Mwenyezi Mungu na akachagua kifungu hiki kunionesha: “Ninachotaka si dhana wala fikira za binadamu, sembuse pesa zako wala mali yako. Ninachotaka ni moyo wako, unaelewa? Haya ni mapenzi Yangu, na hata zaidi ni kitu ambacho Nataka kupata(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 61). Kisha akanisomea kanuni kadhaa za kusimamia maisha ya kanisa: “Kanisa halimruhusu mtu yeyote kuuliza michango katika mahubiri, au kuuliza michango kwa sababu nyingine yoyote” (“Misingi ya Kuanzisha Kanisa na Kusimamia Maisha ya Kanisa” katika Mipango ya Kazi). Alishiriki haya kwa ushirika na mimi: “Katika Kanisa la Mwenyezi Mungu kuna viwango na kanuni kali zinazohitajika kwa kila kipengele cha maisha ya kanisa. Kuhusu kutoa pesa, maneno ya Mwenyezi Mungu yanasema wazi kuwa Mungu hataki pesa za wanadamu au vitu vya kidunia. Kanuni za kazi za kanisa pia zinasema wazi kwamba kanisa halimruhusu mtu yeyote kuhubiri juu ya kutoa pesa au kuwahimiza watu kutoa pesa kwa sababu yoyote. Tangu nianze kumfuata Mwenyezi Mungu, kanisa halijaniuliza nitoe hata senti moja. Sio tu kwamba kanisa halitoi wito kwa watu watoe pesa, lakini hata huwapa ndugu wote ambao ni waumini wa kweli vitabu vyote, CD, na vitu vingine bure. Sasa, mama yangu anataka kutoa mchango fulani kuwasaidia ndugu wengine ambao wanakabiliwa na shida. Anafanya hivyo kwa hiari yake mwenyewe; hakuna mtu anayemlazimisha kulifanya. Hata hivyo, kuwasaidia watu wanaohitaji msaada ni kitendo kizuri, kwa hivyo hakuna sababu ya shutuma, sivyo?”

Baada ya kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu na kusikiliza ushirika wa mke wangu, kitu ambacho mmoja wa dada hao alikuwa ameshiriki nami katika ushirika hapo awali ghafla kilinijia: Kanisa la Mwenyezi Mungu halikubali michango ya pesa kutoka kwa washiriki wapya, na mtu yeyote anayetaka kuchangia pesa lazima kwanza apitie raundi kadhaa za maombi hadi ahakikishe kwamba yuko tayari kabisa kufanya hivyo, na kwamba hatajuta kamwe. Ikiwa hayuko tayari kabisa kufanya hivyo, kanisa halitakubali kabisa. Nilipokumbuka hili, wasiwasi na mashaka fulani ambayo nilikuwa nayo yalipungua kwa namna fulani, lakini fundo lililokuwa moyoni mwangu halikufunguka kabisa. Mke wangu aliona nilivyokunja kipaji, na akijua nilichokuwa nikifikiria, alisema: “Usiamini uvumi huo. Ili kuvuruga na kuihujumu kazi ya Mungu ya kuwaokoa watu na kutuzuia kuja mbele za Mungu na kukubali wokovu Wake, Shetani atasema kila aina ya takataka na atoe kila aina ya ushuhuda wa uwongo. Mungu ni mtakatifu na Mungu huchukia uovu wa wanadamu. Na kuhusu wale walio na sifa mbaya na ambao hawajui jinsi ya kutenda vizuri karibu na watu wa jinsia tofauti, Kanisa la Mwenyezi Mungu haliwakubali kamwe. Hili ni jambo ambalo Mwenyezi Mungu amezungumza waziwazi kulihusu.” Kisha mke wangu akafungua maneno ya Mungu na kusoma: “Watu wengi watapiga magoti kwa ajili ya huruma na msamaha kwa sababu ngurumo saba zinatoa sauti. Lakini hii haitakuwa tena Enzi ya Neema: itakuwa wakati wa ghadhabu. Na kuhusu watu wote watendao uovu (wale ambao huzini, au hujihusisha na fedha chafu, au wana mipaka isiyo wazi kati ya wanaume na wanawake, au ambao hukatiza au kuharibu usimamizi Wangu, au ambao roho zao zimezibwa, au waliopagawa na mapepo mabaya, na kadhalika—wote isipokuwa wateule Wangu), hakuna kati yao ataachiliwa, wala yeyote kusamehewa, lakini wote watatupwa chini Kuzimu na kufa milele!(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 94). Maneno ya Mwenyezi Mungu ni bora na ya hasira ili kuleta woga na uchaji katika mioyo ya watu; hili lilinifanya nifahamu tabia nzuri ya Mungu ambayo haitavumilia makosa ya wanadamu. Mungu anachukizwa sana na wale wanaojihusisha na uasherati, na watu hao mwishowe watapitia adhabu ya Mungu yenye haki. Baadhi ya wasiwasi wangu ulipotea. Mke wangu alishiriki yafuatayo na mimi: “Mungu alipokuwa akifanya kazi Yake katika Enzi ya Sheria mtu yeyote ambaye alikuwa na tabia ya uasherati angepigwa kwa mawe hadi afe. Hili linaonyesha wazi tabia ya Mungu yenye haki, adhimu na yenye ghadhabu. Katika Enzi ya Ufalme, sheria za Mungu ndani ya utawala Wake ni kali hata zaidi kuhusu wanaume na wanawake kuandamana wao kwa wao. Kama inavyosema katika maneno ya Mungu: ‘Mwanadamu anayo tabia ya upotovu na, zaidi ya hayo, amejawa na hisia. Kwa hivyo, ni marufuku kabisa kwa watu wa jinsia mbili tofauti kufanya pamoja kazi wakati wa kumtumikia Mungu bila kuwepo na mtu mwingine. Yeyote yule atakayepatikana na kosa hili atatupiliwa mbali, bila ubaguzi—na hakuna atakayeepuka hili(“Amri Kumi za Utawala Ambazo Lazima Wateule wa Mungu katika Enzi ya Ufalme Wazitii” katika Neno Laonekana katika Mwili).”

Mke wangu aliposoma hili, nilikumbuka tukio lililokuwa limetokea katika msimu wa kuchipua wa 2016. Wakati huo, nilikuwa bado sijachunguza vizuri kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Nilikuwa nikimwendesha mke wangu na mmoja wa akina dada kutoka kanisani kwenda jimbo lingine. Njiani, tulisimama ili mke wangu ashughulikie kitu fulani, na alipotoka nje ya gari dada huyo pia alitoka. Kulikuwa na baridi na upepo nje, na yule dada alisimama kando ya gari akigonga miguu yake chini ili apate joto. Nilimwita aingie ndani ya gari lakini akasema: “Ni sawa. Nitasimama nje kwa muda kidogo.” Ilikuwa ni muda kabla ya mke wangu arudi, na hapo tu ndipo dada huyo aliingia ndani ya gari. Kuona kwamba alikuwa akitetemeka kwa ajili ya baridi mke wangu alimwuliza: “Kuna baridi sana nje. Kwa nini hukukaa ndani ya gari?” Alijibu: “Kuna sheria ya utawala kanisani kwetu kwamba mwanamume na mwanamke hawawezi kuwa peke yao pamoja au kuwasiliana kimwili. Hili ni mojawapo ya mahitaji ambayo Mungu anayo kwa watu Wake wateule, na tunapaswa tulifuate hilo kabisa.” Baada ya kusikia haya, nilihisi kuwa watu walio katika Kanisa la Mwenyezi Mungu kweli ni tofauti na watu wa ulimwengu—hata katika mambo madogo kama haya bado wanajichunguza. Kwa kuzingatia hili, sikuweza kujizuia ila kujipiga kichwa changu kwa kujidharau kwa kutochunguza uhalisi wa ukweli na badala yake kuamini uvumi huo wa mtandaoni bila kufikiria. Nilipofikiria juu ya nyakati zote ambazo nilishirikiana na ndugu wa Kanisa la Mwenyezi Mungu na kuona jinsi mipaka kati ya wanaume na wanawake ilivyokuwa wazi, jinsi walivyokuwa waadilifu na wenye heshima katika usemi na vitendo, jinsi walivyokuwa waadilifu wanaposhirikiana na watu au kushughulikia masuala, ni dhahiri kwamba uvumi huo mtandaoni haukuwa wa kweli. Wakati huo nilihisi aibu sana—iliibuka kuwa uvumi huo wa mtandaoni ulikuwa uwongo, kashfa, upotoshaji dhahiri wa ukweli—lakini mimi nilichukua uwongo huo na nikawa na shaka juu ya Mwenyezi Mungu na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Nilikuwa mjinga aliyechanganyikiwa sana! Mke wangu basi aliendelea katika ushirika: “Katika siku za mwisho, Mungu kuwa mwili na kuonyesha ukweli wa kuwahukumu na kuwasafisha watu ni ili awaokoe kabisa wanadamu kutoka katika umiliki wa Shetani na kutuondolea tabia zetu potovu—kiburi, ujanja, udanganyifu, ubinafsi, ubaya, uovu, na uchafu—na kutusaidia kufanikisha mabadiliko katika tabia yetu ya maisha ili tuweze kuishi kwa kudhihirisha mfano wa kweli wa binadamu. Mungu anajua kuwa wanadamu wamepotoshwa kwa kina sana na Shetani na hawana uwezo wa kushinda dhambi; kwa hivyo ili kuhakikisha kuwa watu hawaikosei tabia ya Mungu wakati wanakubali wokovu wa Mungu na hivyo kuondolewa na kuadhibiwa, Mungu ameweka sheria za utawala za Enzi ya Ufalme ili awaelekeze waumini. Yeyote atakayevunja sheria hizi ataadhibiwa na Mungu, na wakosaji wakubwa watafukuzwa kutoka kanisani na kupoteza nafasi yoyote ya wokovu. Mungu kutoa amri hizi kwa kanisa ni kutupa maarifa ya kweli ya tabia ya Mungu yenye haki na isiyokosewa, na pia ili tuwe na sheria za kutuelekeza. Kwa njia hii, katika tabia zetu zote kutakuwa na mstari ambao hauwezi kuvukwa, na tukisalia ndani ya mipaka hii basi tunaweza kuepuka majaribu mengi ya Shetani. Hii ni njia ya Mungu ya kutulinda na, aidha, ni upendo wa kweli wa Mungu kwetu!” Nikiusikiliza ushirika wa mke wangu nilijikuta nikitikisa kichwa changu kwa kukubali bila kutaka, na kwa hivyo fundo lililokuwa moyoni mwangu lilifunguka na maumivu yaliyokuwa yakiusonga moyo wangu yaliondoka. Baada ya hapo, nilianza tena kuhudhuria mikutano ya kanisa.

Kila ninapokumbuka tukio hili daima kuna hofu fulani inayoelea moyoni mwangu. Niliona jinsi uvumi huu unavyoharibu; nilikuwa karibu nihadaiwe nao na karibu nipoteze nafasi ya wokovu wa Mungu wa siku za mwisho. Katika Enzi ya Neema, Waisraeli pia walidanganywa na uvumi wa uwongo na hawakumtambua Bwana Yesu kama ujio wa Masihi. Walimkataa Bwana Yesu na kwa hivyo walipoteza wokovu wa Bwana. Hili lilinifanya nigundue uvumi kama huo ni ulivyo vizuizi vikubwa kwenye njia ya imani ya kweli! Lakini kile ambacho bado sikuelewa vizuri kilikuwa ni kwa nini kuna uvumi mwingi wa uwongo na tuhuma za uwongo juu ya Kanisa la Mwenyezi Mungu mtandaoni wakati ni wazi kuwa ni kanisa nzuri. Kwa hivyo, wakati wa mkutano mmoja wa kanisa niliibua swali hili na ndugu ili tuweze kushirikiana kwa uaminifu kulihusu. Walinichezea moja ya filamu za injili za kanisa, Kupita Katika Mtego, ambayo ilisuluhisha kabisa mkanganyiko wangu. Kwa kushirika zaidi na ndugu nilipata ufafanuzi zaidi. Kutumia uvumi kuvuruga na kuharibu kazi ya Mungu imekuwa mbinu thabiti ya Shetani. Bwana Yesu alipokuwa akifanya kazi Yake, makuhani wakuu wa Kiyahudi, waandishi na Mafarisayo walitaka kuhakikisha kuwa wanawadhibiti watu wateule wa Mungu, na kwa hivyo walibuni uvumi mwingi wa uwongo kumhusu Bwana Yesu. Walimkufuru Bwana Yesu kwa kusema kwamba alitegemea nguvu ya Belzebuli kutoa pepo, walimtuhumu kwa uwongo Bwana Yesu kwa kutowaruhusu watu kulipa ushuru wao kwa Kaisari, na pia walitoa ushuhuda wa uwongo kwa kusema kwamba mwili wa Bwana Yesu uliibwa na wanafunzi Wake na kwamba Hakuwa amefufuka. Nina hakika kwamba mtandao ungalikuwapo wakati huo, viongozi hao wa kidini wangeweka uvumi wao wote na ushuhuda wa uwongo mtandaoni ili wamkufuru, kumshambulia, na kumshutumu Bwana Yesu. Siku hizi, katika Enzi ya Ufalme, Mwenyezi Mungu anafanya kazi ya maneno kuwahukumu na kuwatakasa wanadamu; serikali ya Uchina na vile vile wachungaji na wazee katika jamii ya kidini wanatumika kama vyombo vya Shetani. Ili kufikia lengo lao la kuwadhibiti na kuwatega watu, wanamkufuru na kumshutumu Mwenyezi Mungu, wakibuni uvumi na ushuhuda wa uwongo kwa ukaidi, na kulipaka tope Kanisa la Mwenyezi Mungu ili kuwachanganya watu na kuwaacha bila ufahamu. Katika kiburi chao, wanafikiria wanaweza kuwafanya watu waachane na kazi ya wokovu ya Mungu ya siku za mwisho na kuwafuata katika kumpinga Mungu. Kwa kweli Shetani ni mwovu na mwenye kuchukiza sana!

Kisha ndugu walinisomea vifungu vingine viwili vya maneno ya Mungu: “Duniani, kila aina ya pepo wanazungukazunguka bila mwisho wakitafuta mahali pa kupumzika, na bila kukoma wanatafuta maiti za wanadamu zinazoweza kuliwa(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 10). “Shetani daima anagugumia maarifa ambayo wanadamu wameshikilia kunihusu mioyoni mwao, na daima, kwa meno na makucha wazi, akishiriki kwa maumivu ya mwisho ya mapambano yake ya kifo. Je, unataka kukamatwa na mipango yake danganyifu wakati huu? Unataka, wakati awamu ya mwisho ya kazi Yangu imekamilika, kukata maisha yako mwenyewe?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 6). Pia walishiri ushirika nami kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu hutuambia ukweli juu ya vita vya kiroho, ambao ni kwamba ili kuzuia watu kuja mbele za Mungu na kuwameza, Shetani hutekeleza ujanja wa kila aina. Hii ni pamoja na udanganyifu wa kueneza uvumi na ushuhuda wa uwongo kwenye mtandao, kuwafanya viongozi wa dini wawanyanyase na kuwatishia waumini, na kuwafanya washiriki wa familia wawalazimishe na kuwazuia wasimfuate Mwenyezi Mungu. Kwa ufupi, chochote kinachotufanya tuwe na shaka, kumkataa au kwenda mbali na Mungu hutoka kwa Shetani. Ikiwa hatuwezi kutafuta ukweli, basi hatutaweza kung’amua ujanja wa Shetani, tutapoteza nafasi ya kupata wokovu wa Mungu kwa urahisi, na tutazama katika janga pamoja na Shetani. Kwa sababu ya uongozi wa Mungu, niliweza kuona wazi kabisa ubaya na kiini cha Shetani kinachostahili dharau na kung’amua njama za Shetani kupitia kutazama filamu za injili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu na kusikiliza ushirika wa ndugu.

Tangu nimfuate Mwenyezi Mungu nimepata kuachiliwa na uhuru wa kweli. Sasa, kila ninapokumbana na ugumu naweza kusoma maneno ya Mungu na kumwomba Mungu anisaidie kupata njia ya kutenda. Ndugu kanisani wote hufuata mahitaji ya Mungu na wanatafuta kuwa watu waaminifu. Mahusiano yao ya pamoja hayana mkanganyiko na ni ya wazi; wanasaidiana na kutiana moyo. Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu mtu kujaribu kunishusha, kunidanganya, au kuniibia. Ninajisikia mwenye furaha na utulivu, na haya ndiyo maisha ninayotaka kuishi kila wakati.

Iliyotangulia: 42. Dhoruba ya Talaka Yazimwa

Inayofuata: 44. Nimerudi Nyumbani

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

2. Njia ya Utakaso

Na Christopher, UfilipinoJina langu ni Christopher, na mimi ni mchungaji wa kanisa la nyumbani huko Ufilipino. Mnamo mwaka wa 1987,...

38. Wokovu wa Aina Tofauti

Na Huang Lin, ChinaNilikuwa mwumini wa kawaida katika Ukristo wa Kipaji, na tangu nianze kuamini katika Bwana sikuwahi kukosa ibada....

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp