Tiba ya Wivu

24/01/2021

Na Xunqiu, Uchina

Mwenyezi Mungu anasema, “Mwili wa mwanadamu ni wa Shetani, umejaa tabia za uasi, ni mchafu kiasi cha kusikitisha, na ni kitu chenye najisi. Watu hutamani raha ya mwili kupita kiasi na kuna maonyesho mengi sana ya mwili; hii ndiyo maana Mungu hudharau mwili wa mwanadamu kwa kiwango fulani. Watu wanapotupa mambo machafu, potovu ya Shetani, wao hupata wokovu wa Mungu. Lakini bado wasipoachana na uchafu na upotovu, basi bado wanamilikiwa na Shetani. Ujanja, udanganyifu, na ukora wa watu yote ni mambo ya Shetani. Wokovu wa Mungu kwako ni ili kukuokoa kutoka katika mambo haya ya Shetani. Kazi ya Mungu haiwezi kuwa na kosa; yote inafanywa ili kuwaokoa watu kutoka gizani. Wakati ambapo umeamini hadi kwa kiwango fulani na unaweza kuachana na upotovu wa mwili, na hufungwi tena pingu na upotovu huu, je, hutakuwa umeokolewa? Wakati ambapo unamilikiwa na Shetani huwezi kumdhihirisha Mungu, wewe ni kitu kichafu, na huwezi kupokea urithi wa Mungu. Mara tu unapotakaswa na kufanywa mkamilifu, utakuwa mtakatifu, utakuwa mtu wa kawaida, na utabarikiwa na Mungu na kuwa mtu anayemfurahisha Mungu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Utendaji (2)). Nilikuja kuelewa kupitia maneno ya Mungu kwamba tuna mapambano ya wivu na ugomvi unaofanyika kati ya watu kwa sababu tumepotoshwa na Shetani na sote tunaishi kulingana na tabia zetu za kishetani na mbovu za udanganyifu na ni za ubinafsi sana. Kuna wakati ambapo nilikuwa nikiishi katika hali ya wivu na niliwapangia watu hila kila wakati na nilijitahidi kupata sifa na faida. Kuishi kwa njia hiyo kulisikitisha sana, lakini sikuweza kabisa kujiweka huru. Kuhukumu na kuadibu kwa Mungu ndiko kulinibadilisha kidogo na kuniepusha na masikitiko hayo.

Ilikuwa Juni ya 2017 nilipopewa wajibu wa kiongozi wa kikundi kimoja kanisani na niliwajibikia maisha ya kanisa ya sehemu chache za kukutanikia. Nilifurahia sana kuwa na wajibu huo na nilihisi kwamba Mungu alikuwa Akiniinua na kwamba sikuwa na budi kuufanya vizuri ili kulipa upendo wa Mungu. Baada ya hapo, nilihusika sana katika ushirika katika mikutano na nilipowaona kina ndugu wakikabiliwa na matatizo au wakiwa katika hali mbaya, nilitafuta maneno ya Mungu ya kushiriki na kushughulikia matatizo hayo. Wengine waliniheshimu baada ya muda na wakasema kwamba niliweza kutatua matatizo ya kiutendaji kupitia ushirika katika mikutano na kwamba niliwajibika katika wajibu wangu na nilikuwa mwenye upendo kwa kina ndugu. Niliridhika sana niliposikia hayo.

Muda mfupi baadaye, nilisikia kwamba kutakuwa na uchaguzi wa kiongozi wa kanisa na nikawaza, “Kila mtu ananiheshimu, hivyo kuna uwezekano mkubwa wa mimi kuchaguliwa. Nikichaguliwa, bila shaka kina ndugu watanistahi hata zaidi.” Mimi na Dada Yang tuliteuliwa baada ya kura. Nilitishika kidogo nilipoona kwamba alikuwa amepata kura nyingi zaidi kuniliko. Niliwaza, “Mimi ni mwaminifu katika wajibu wangu na ninaweza kufanya kazi ya vitendo. Anawezaje kupata kura nyingi zaidi kuniliko?” Lakini nikawaza baadaye, “Huu ni uteuzi tu, si kura ya mwisho. Bado nina nafasi. Nahitaji kujiandaa kwa ukweli sasa na kuwasaidia wengine zaidi kutatua matatizo yao katika kuingia uzimani ili wote waweze kuona kwamba yeye si bora kuniliko, kisha bila shaka nitachaguliwa!” Nilikumbuka tatizo ambalo Dada Wang alikuwa ameibua kwenye mkutano wa mwisho ambalo halikuwa limetatuliwa, kwa hivyo nilikwenda upesi kuandaa maneno husika ya Mungu ya kushiriki naye wakati uliofuata. Siku ya kukusanyika ilipowadia, nilienda kwenye mahali petu pa mkutano, lakini mara nilipoingia ndani nilimwona Dada Yang akifanya ushirika na Dada Wang. Sikuridhika kabisa. Niliwaza, “Nilikuja leo kushiriki naye ili kutatua tatizo lake lakini umetangulia kulitatua! Iwapo tayari umelishughulikia, nitaonyeshaje yale ninayoweza kufanya?” Kama nilivyotazamia, tabasamu ilionekana usoni pa Dada Wang baada ya ushirika wa Dada Yang na ndugu wengine wote waliafiki kwa kutikisa kichwa. Sikufurahi kabisa nilipoona hayo. Nilimwonea wivu Dada Yang nikidhani kwamba alikuwa ameniibia sifa yangu. Niliwaza, “Kabla ya wewe kujiunga na mkutano huu, wengine wote walitaka kusikia ushirika wangu. Lakini sasa kila mtu anakuheshimu na hanijali kabisa.” Kila mtu alishiriki katika ushirika kwa furaha wakati huo huo, lakini sikuweza kuvumilia hayo yote na nilikuwa na hamu ya kuondoka.

Nilipofika nyumbani nilikaa kitandani, nikiwa mwenye huzuni, na kadiri nilivyozidi kufikiria hayo ndivyo nilivyozidi kuhisi kwamba nilikuwa hoi. Niliwaza, “Haya yakiendelea, nafasi zangu za kuwa kiongozi zitakuwa chache sana. Hapana, lazima nihusike zaidi katika ushirika. Siwezi kabisa kushindwa naye tena.” Baadaye, niligundua kwamba Dada Xiang alionea wasiwasi mateso makali ya CCP na alikuwa akihisi kwamba alizuiwa katika wajibu wake, kwa hivyo nilitafuta upesi maneno ya Mungu ya kushiriki naye kabla ya mkutano. Nilifika mahali pa mkutano mapema siku iliyofuata, lakini ajabu ni kwamba, Dada Yang alikuwa amefika huko mapema hata zaidi na tayari alikuwa akifanya ushirika na Dada Xiang. Nilifadhaika na nikawaza, “Unawezaje kufanya hivi tena? Nahitaji kuona una nuru ya aina gani katika ushirika wako. Siamini kabisa kwamba inaweza kushughulikia kila kitu.” Kwa kuwa sikusadiki, nilikaa karibu nao ili nisikie alikuwa na yapi ya kusema. Nilipokuwa nikisikiliza, niligundua kwamba Dada Yang alishiri juu ya njia fulani za kutenda kwa kuzingatia maneno ya Mungu, lakini hakuwa ametaja chanzo cha udhaifu na uhasi wa Dada Xiang. Niliwaza, “Nahitaji kutumia fursa hii kushiriki ufahamu wangu mwenyewe na kupunguza ari ya Dada Yang.” Baada ya kufikiria hayo, nilikurupuka kushiriki ushirika wangu, nikisema, “Dada, kuwa na njia ya kutenda pekee hakutoshi kutatua hali hasi. Tunahitaji pia kufahamu ukweli unaohusu jinsi ambavyo Mungu hutumia joka kubwa jekundu kama foil ili kuwakamilisha watu Wake walioteuliwa. Tunaweza kutoka katika hali hasi kwa kuelewa tu kazi, uweza na hekima ya Mungu. Hebu tusome maneno ya Mungu pamoja.” Dada Xiang alipokuwa akitikisa kichwa chake, nilimtupia jicho Dada Yang na nikamwona akiwa ameketi kando kabisa kwa fedheha. Nilihisi kana kwamba nilikuwa nimeshinda mapambano na nikawaza, “Kila mtu ataweza kuona ushirika wa nani kwa kweli ni mzuri atakapoulinganisha. Naweza kujivuna tena na hii inathibitisha kuwa nina uwezo.” Baada ya hayo, nilihusika zaidi katika wajibu wangu. Niliposikia kuhusu watu waliokuwa katika hali mbaya au waliokabiliwa na matatizo, nilitafuta maneno ya Mungu mara moja, nikaandika mihutasari na kisha kushiriki nao. Nilipoona mtu akitikisa kichwa chake nilisisimka, ilhali kama hakukuwa na majibu yoyote nilifadhaika sana, kisha kadiri nilivyozidi kufadhaika, ndivyo nilivyozidi kushindwa kuelewa hali za wengine au kutatua matatizo. Nilizidi pia kuhisi uchovu, na nikawaza, “Mambo yakiendelea hivi bila shaka kina ndugu watasema kwamba sina uhalisi wa ukweli na hawatanichagua kama kiongozi.” Hasa nilipomwona Dada Yang akifanya ushirika wa vitendo juu ya ukweli ambao kina ndugu walikubaliana nao, nilizidi kufadhaika hata zaidi. Wivu wangu na kutoweza kwangu kuukubali ulianza kuwa dhahiri. Nilianza kumchukia na sikutaka hata kuzungumza naye. Nilikuwa nikiishi katika hali hiyo ya kushindania sifa na faida. Hali hiyo ilinisikitisha sana. Sikuwa nikipata nuru yoyote kutoka kwa maneno ya Mungu na nilikuwa nikiomba tu kwa namna isiyo ya dhati. Nilihisi kwamba nilizidi kuwa mbali na Mungu.

Baadaye, nilimwomba Mungu na kumsihi Anipe nuru Yake ili niweze kuelewa tabia yangu potovu na kutoka katika hali hiyo mbaya. Nilipata ufahamu kiasi kuhusu hali yangu potovu kupitia tu maneno ya Mungu pekee. Yanasema hivi: “Watu wengine daima wana hofu kwamba wengine wataiba maarufu wao na kuwashinda, wakipata utambuzi ilhali wao wenyewe wanatelekezwa. Hili huwasababisha kuwashambulia na kuwatenga wengine. Je, huku si kuwaonea wivu wale walio na talanta? Je, huku si kuwa wabinafsi na wachoyo? Je, mwenendo kama huu si wa binafsi na wa kudharauliwa? Hii ni tabia ya aina gani? Ni ovu! Kujifikiria tu, kuridhisha tu tamaa zako mwenyewe, kutofikiria wajibu wa wengine, na kufikiria tu kuhusu maslahi yako mwenyewe na sio maslahi ya nyumba ya Mungu—watu kama hawa wana tabia mbaya, na Mungu hawapendi. Ikiwa kweli unaweza kufikiria mapenzi ya Mungu, basi utaweza kuwatendea wengine kwa haki. Ukimpa mtu pendekezo lako, na mtu huyo akuzwe kuwa mtu wa kipaji, na hivyo kuleta mtu mmoja mwingine mwenye kipaji katika nyumba ya Mungu, je, hutakuwa umefanya kazi yako vizuri? Je, basi hutakuwa mwaminifu katika kutimiza wajibu wako? Hili ni tendo jema mbele za Mungu, na ndiyo aina ya dhamiri na mantiki ambazo watu wanapaswa kuwa nazo(“Mpe Mungu Moyo Wako wa Kweli, Na Unaweza Kupata Ukweli” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Niliona aibu baada ya kusoma maneno ya Mungu na nikafikiria mambo yote ya wivu na jinsi nilivyojitahidi kwa ajili ya sifa na faida. Nilikuwa nimejawa na tamaa tangu niliposikia kwamba kanisa lilikuwa limchague kiongozi, na kisha nilipoona kwamba Dada Yang alipata kura nyingi kunishinda katika uteuzi, nilianza kumwona kama mpinzani wangu, nikipigana na kushindana naye kimyakimya. Kumwona akitatua matatizo ya kina ndugu kupitia ushirika juu ya ukweli kulinifanya nione wivu. Nilidhani kwamba alikuwa ameiba sifa yangu na kwamba alitishia nafasi yanguya kuwa kiongozi. Nilijipambanisha naye kisirisiri, nikilalamika na kukosoa ushirika wake. Nilimdunisha kwa hila huku nikijiinua na kupunguza ari yake katika wajibu wake. Nilipoona kwamba sikuweza kushinda, nilianza kumchukia na hata sikutaka kumtambua. Nilijitahidi kwa ajili ya sifa na faida na niliona wivu katika wajibu wangu. Nilimshambulia kwa maneno na kumtenga. Nilikuwa nimefunua kabisa tabia ya kishetani. Nilikuwa mbinafsi, mwenye kustahili dharau na mwovu sana! Nilikuwa nikitegemeza maisha yangu kwa tabia za kishetani, na mbali na kuwaumiza wengine, pia niliishi katika chuki na maumivu. Ilinikumbusha Zhou Yu katika Mapenzi ya Falme Tatu. Alijihusisha na mambo madogomadogo sana, alimwonea wivu Zhuge Liang kila mara na kabla ya kifo chake alisema, “Kwa kuwa Yu alizaliwa, kuna haja gani ya Liang?” Aliishia kufa kwa hasira. Je, hayo si matokeo mabaya ya wivu? Niligundua kwamba nilikuwa vilevile, kwamba niliona wivu katika juhudi zangu za kupata hadhi na mbali na kuzuia kuingia kwangu katika uzima, pia niliwadhuru wengine. Sikuwa kabisa na ubinadamu. Nilimchukiza na kumtia Mungu kinyongo. Kwa kweli, Mungu alinipangia niwe karibu na mtu mwenye ubora mzuri zaidi wa tabia, Akitumaini kwamba nitajifunza kutoka kwa uwezo wake ili niboreshe uwezo wangu. Lakini nilipambana tu na kujilinganisha. Sikupata chochote mwishowe na nilisikitika sana. Nilikuwa mpumbavu sana. Pia, ukweli hutawala katika nyumba ya Mungu na kuna kanuni za uteuzi wa viongozi. Angalau, wao ni watu wenye ubinadamu mzuri wanaoweza kukubali na kutenda ukweli, lakini niliona wivu kila wakati, nilishindania sifa na faida na sikuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wowote. Hiyo ilinifanya nisistahili kuwa kiongozi. Nilijua kwamba ilibidi niache kushindana, nizingatie kutenda ukweli na niishi kulingana na maneno ya Mungu. Hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee iliyostahili. Nilitulia sana baada ya kugundua yote hayo.

Niliomba mombi haya siku ya uchaguzi: “Ee Mungu! Bila kujali matokeo ni yapi, niko tayari kukutii na nitapiga kura ya haki.” Lakini bado nilisitasita wakati wa kupiga kura ulipofika kwa kweli. Niliwaza, “Nikimpigia kura Dada Yang na aishie kuchaguliwa, wengine watanionaje? Bila shaka watasema kwamba mimi si hodari kama yeye.” Nilikumbuka maneno haya ya Mungu wakati huo huo: “Lazima ujifunze kuacha na kuweka kando vitu hivi, kuwapendekeza wengine, na kuwaruhusu wengine kutokeza. Using’ang’ane au kukimbilia kujinufaisha punde unapopata nafasi ya kutokeza au kupata utukufu. Lazima ujifunze kujiondoa, lakini hupaswi kuchelewesha utekelezaji wa wajibu wako. Kuwa mtu anayefanya kazi kwa ukimya bila kuonekana, na ambaye hajionyeshi kwa wengine unapotekeleza wajibu wako kwa uaminifu. Kadiri unavyoacha ufahari na hadhi yako, na kadiri unavyoacha masilahi yako mwenyewe, ndivyo utakavyokuwa mwenye amani zaidi, na ndivyo nafasi itakavyofunguka zaidi ndani ya moyo wako na ndivyo hali yako itakuwa bora zaidi(“Mpe Mungu Moyo Wako wa Kweli, Na Unaweza Kupata Ukweli” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Niliwaza baada ya hayo, “Lazima nitende maneno ya Mungu. Siwezi kuendelea kuishi kwa ajili ya sifa na hadhi yangu.” Nilifikiria jinsi Dada Yang alivyokuwa mwenye ubora mzuri wa tabia na ushirika wake ulivyokuwa wa vitendo, kwa hivyo kumfanya awe kiongozi kungelifaidi kanisa na vile vile kuingia katika uzima kwa kina ndugu. Ilinibidi nitende ukweli na nitetee masilahi ya kanisa. Na kwa hivyo, nilimpigia kura. Alichaguliwa kama kiongozi na nilikuwa mtulivu sana na mwenye amani. Nilihisi kwamba mwishowe nilikuwa nimeweza kutenda ukweli. Shukrani kwa Mungu!

Baadaye, mnamo Aprili 2018, nilichaguliwa kwa ajili ya wajibu wa kiongozi wa kanisa, na nilifanya kazi na kina ndugu wengine wachache waliowajibikia kazi ya kanisa. Mwanzoni, tulijadili kazi zote za kanisa na tukashirikiana vizuri sana. Lakini baada ya muda, niligundua kwamba Dada Li, ambaye alisimamia kazi yetu ya uandishi, alikuwa mwenye ubora mzuri wa tabia na alijifunza mambo haraka. Ushirika wake uliwatia nuru na kuwaadilisha wengine. Nilivutiwa naye sana lakini nilihisi wivu kidogo. Nilianza kutarajia kuhusika katika kazi katika wajibu wake, kwa kuwa nilitaka kujifunza ustadi na kanuni zaidi ili nisishindwe naye. Siku moja nilipata barua kutoka kwa kiongozi wetu akisema kwamba alimhitaji mtu afanye kazi fulani katika kanisa moja katika eneo lingine na akiuliza iwapo Dada Li atafaa vizuri. Aliuliza iwapo ningeweza kukusanya tathmini zake. Wivu wangu uliibuka mara moja na nikawaza, “Wanataka kumkuza Dada Li. Ubora wake wa tabia ni mzuri na yeye huelewa mambo haraka, lakini yeye hajakuwa muumini kwa muda mrefu na kuingia kwake katika uzima ni kwa juujuu. Je, silingani naye kwa namna gani? Kwa nini nisiende? Dada Li akichukua wajibu huo, wengine watanionaje? Bila shaka watasema yeye ni bora kuniliko.” Mawazo haya yalinifanya nizidi kuwa na wasiwasi na hata sikumtambua nilipomwona baada ya hayo. Alipoona nikitenda hivyo, alihisi kwamba alizuiwa na akaacha kujadili mambo nami kama zamani. Nilipata tathmini za kina ndugu za Dada Li siku chache baadaye na niliona wivu sana nilipoona kwamba zote zilikuwa chanya na hata bora zaidi kuliko walivyo nitathmini. Nilikuwa kiongozi, lakini hata sikuwa sawa na mfanyakazi mwenzangu. Ilikuwa aibu sana kwangu! Nilizidi kuwa na wasiwasi nilipokuwa nikifikira hayo. Nilimwambia dada mwingine, “Uliandikaje tathmini yako? Huna utambuzi wowote. Dada Li ameendelea, lakini kuingia kwake katika uzima ni kwa juujuu. Umemfanya aonekane mzuri mno, lakini akienda katika kanisa lingine na acheleweshe kazi ya kwa sababu hawezi kufanya kazi ya vitendo, huko kutakuwa kutenda uovu kwa upande wako!” Yule dada aliogopa kidogo aliposikia haya kutoka kwangu. Alisema kwamba alikuwa ameiandika kulingana na hali halisi, lakini hakuwa amezingatia kila kitu na kwamba ataiangalia tena. Hata ingawa nilikuwa nimefanya kile nilichokuwa nimeamua kufanya, sikuhisi furaha kabisa. Hasa nilipomwona Sista Li, nilijawa na majuto na niliona hatia sana. Nilikuwa nimefanya kitu kibaya, kitu cha aibu na sikuweza kuthubutu kumtazama machoni. Alipoona kwamba nilionekana mwenye tatizo, alikuja na kusema kwa wasiwasi, “Kuna tatizo?” Niliona hatia hata zaidi nilipomsikia akisema hivyo, kwa hivyo nilisema tu huku nikigogota maneno “Na-naam,” kisha nikakwenda kwenye chumba kingine upesi na nikapiga magoti na kumwomba Mungu. Nilisema, “Ee Mungu, sina mantiki kabisa. Nilimwonea wivu Dada Li nilipoona tathmini za kila mtu na hata nilimdunisha kisirisiri. Mungu, najua kwamba Unachukia jambo kama hili, lakini nimefungwa na tabia yangu potovu. Siwezi kujizuia. Mungu naomba Unitie nuru kusudi niweza kujijua na kuacha kuishi kulingana na tabia yangu potovu.” Nilipotulia kidogo baada ya maombi yangu, niliwasha kompyuta yangu na kusoma vifungu kadhaa vya maneno ya Mungu.

Mungu anasema, “Wakimwona mtu aliye bora kuwaliko, wanamkandamiza, wanaanzisha uvumi kumhusu, au kutumia njia za uovu ili watu wengine wasimheshimu, na kwamba hakuna mtu aliye bora kuliko mtu mwingine, basi hii ni tabia potovu ya kiburi na yenye kujidai, na vile vile ya uovu, udanganyifu na kudhuru kwa siri, na watu hawa hawazuiwi na chochote katika kufikia malengo yao. Wanaishi namna hii na bado wanafikiria kuwa wao ni wazuri na kwamba wao ni watu wema. Hata hivyo, je, wana mioyo inayomcha Mungu? Kwanza kabisa, kuzungumza kutoka katika mtazamo wa asili za mambo haya, je, watu ambao hutenda hivi hawafanyi vile wapendavyo tu? Je, wao hufikiria masilahi ya familia ya Mungu? Wanafikiria tu kuhusu hisia zao na wanataka tu kufikia malengo yao wenyewe, bila kujali hasara inayopatwa na kazi ya familia ya Mungu. Watu kama hawa sio tu wenye kiburi na wa kujidai, pia ni wabinafsi na wenye kustahili dharau; hawajali kabisa kuhusu kusudi la Mungu, na watu kama hawa, bila shaka yoyote, hawana mioyo inayomcha Mungu. Hii ndiyo sababu wanatenda chochote wanachotaka na kutenda kwa utundu, bila hisia yoyote ya lawama, bila hofu yoyote, bila wasiwasi au shaka yoyote, na bila kuzingatia matokeo. Hawamchi Mungu, wanajiamini kuwa muhimu sana, na wanaona kila kipengele chao kuwa cha juu kumliko Mungu na cha juu kuliko ukweli. Mioyoni mwao, Mungu ndiye wa chini zaidi anayestahili kutajwa na Asiye na maana zaidi, na Mungu hana hadhi yoyote mioyoni mwao hata kidogo. Je, wale ambao hawana nafasi ya Mungu mioyoni mwao, na wasiomcha Mungu, wamepata kuingia katika ukweli? (Hapana.) Kwa hivyo, kwa kawaida wakati wao huzunguka wakijishughulisha kwa furaha na kuweka nguvu nyingi, wao huwa wanafanya nini? Watu kama hao hata hudai kuwa wameacha kila kitu ili kutumika kwa ajili Mungu na kwamba wamepitia shida nyingi, lakini kwa kweli, nia, kanuni, na lengo la vitendo vyao vyote ni kujinufaisha; wanajaribu tu kulinda masilahi yao yote. Je, mnaweza kusema kwamba mtu wa aina hii ni mbaya sana au la? Je, mtu asiyemcha Mungu ni mtu wa aina gani? Je, si yeye ni mwenye kiburi? Je, si yeye ni Shetani? Je, ni mambo ya aina gani ndiyo yasiyomcha Mungu? Kando na wanyama, wale wote wasiomcha Mungu ni pamoja na pepo, Shetani, malaika mkuu, na wale wanaobishana na Mungu(“Masharti Matano Ambayo Watu Wanayo Kabla ya Kuingia Kwenye Njia Sahihi ya Kumwamini Mungu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). “Tabia ya upotovu ya mwanadamu inatokana na hali yake ya kupewa sumu na kukanyagwa na Shetani, kutokana na madhara mabaya sana ambayo Shetani ameweka katika mawazo yake, maadili, ufahamu, na hisia. Ni hasa kwa sababu mambo ya msingi ya mwanadamu yamepotoshwa na Shetani, na ni tofauti kabisa na jinsi Mungu aliwaumba kwa asili, kwamba mwanadamu humpinga Mungu na haelewi ukweli(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu).

Nilifadhaishwa na kutiwa hofu sana na maneno ya Mungu. Je, Hakuwa amefunua hali yangu hasa? Nilianza kuwa na wivu na chuki kiongozi alipotaka kumkuza Dada Li na hata nilimdunisha na kumhukumu kwa njia zilizostahili dharau. Niliwazia kila kitu ili kumzuia kupata wajibu huo bila kuzingatia masilahi ya kanisa hata kidogo. Nilifanya chochote nilichopenda ili kupata kile nilichotaka. Nilikuwa mwenye kiburi, dhalimu na sikumcha Mungu. Mungu anatarajia watu wengi zaidi waweze kuzingatia mapenzi Yake na watekeleze wajibu wao. Nilijua vizuri … Nilijua vizuri kwamba Dada Li alikuwa na ubora mzuri wa tabia na alilenga kufuatilia ukweli, hivyo kama angepata fursa zaidi za mafunzo, kuingia kwake katika uzima na ustadi wake ungeendelea na hilo lingefaidi kazi ya kanisa. Lakini nilimzuia huku nikijaribu kulinda heshima na hadhi yangu, na hata nikatumia njia za hila kumzuia ili asipewe wajibu huo. Kufumba na kufumbua, nilikuwa mtumishi wa Shetani na nilikuwa nikivuruga kazi ya kanisa. Nilijilaumu sana. Nilikuwa nimejua kwamba wivu unakinzana na mapenzi ya Mungu, lakini sikuwahi kufikiri kwamba itanisababisha nifanye kitu cha ukatili sana, kwamba nitavuruga kazi ya kanisa, nitafanya maovu na kumpinga Mungu. Nilikumbuka maneno haya ya Mungu: “Tabia ya upotovu ya mwanadamu inatokana na hali yake ya kupewa sumu na kukanyagwa na Shetani” Nilifikiria jinsi nilivyoona wivu kila wakati na sikuweza kuvumilia kumwona mtu yeyote aliyekuwa bora kuniliko kwa sababu mawazo na maoni yangu yalikuwa yamepotoshwa na sumu za Shetani, kama vile “Kila mwamba ngoma huvutia upande wake,” “Mimi ni bwana wangu mwenyewe kotekote mbinguni na ardhini,” na “Kunaweza kuwa tu na ndume alfa mmoja” Kwa kuwa niliishi kulingana na hizi sumu, nilitaka kupigania kupata uongozi katika kikundi chochote, nikidhani kwamba nilipaswa kuwatawala wengine, na sikuweza kumtendea mtu yeyote kwa haki iwapo nilidhani kwamba alikuwa na uwezo zaidi kuniliko. Niliona wivu na nilikuwa mwenye ubaguzi na nilimwona kama maudhi. Niliona wivu, niliwatenga na nilikuwa adui kwa watu waliokuwa karibu nami ambao walifuatilia ukweli na hata niliwadunisha kisirisiri. Sikuwa na ubinadamu hata kidogo! Nilitaka kila mara kujiboresha na kuwadunisha wengine, kupigana, kushinda na sikukubali kushindwa na mtu yeyote. Nilitaka tu kujionyesha. Je, sikuwa Shetani aishiye? Wakati huo tu ndipo nlipoona kwamba sumu na sheria hizo za kishetani za kuendelea kuishi zilikuwa asili yangu. Nilizitegemeza katika maisha yangu na nikazidi kuwa mbinafsi, mwenye kiburi na mwovu. Kama ningeendelea kukataa kutubu kwa Mungu, nilijua kwamba ningechukiwa na kuondolewa na Yeye. Nilihisi hofu sana nilipogundua haya yote. Nilikimbia kumwomba Mungu, nikimwambia kwamba nilitaka kutubu, kwamba nitajaribu kutenda ukweli kuanzia wakati huo na kuacha kuishi kulingana na sumu hizo za kishetani.

Siku chache baadaye nilipokea barua kutoka kwa kiongozi akisema kwamba kwa ujumla, Dada Li alionekana kama aliyestahili kazi hiyo katika kanisa hilo lingine. Nilihisi kwamba kitu kilichochewa ndani yangu nilipoisoma, lakini nikagundua mara moja kwamba ni wivu wangu uliokuwa ukinitawala tena. Nilimwomba Mungu mara moja na nikawa tayari kuukana mwili wangu. Nilisoma vifungu vingine viwili vya maneno ya Mungu baada ya kuomba. Mungu anasema, “Unapojidhihirisha kuwa mbinafsi na mtu wa aibu, na unapogundua haya, unapaswa kutafuta ukweli: Je, ninapaswa kufanya nini ili nilingane na mapenzi ya Mungu? Je, ninapaswa kutenda jinsi gani ili imfaidi kila mtu? Yaani, lazima uanze kwa kupuuza masilahi yako mwenyewe na kuyaacha polepole kulingana na kimo chako, kidogo kidogo. Baada ya kupitia haya mara chache, utakuwa umeyapuuza kabisa, na utakapokuwa ukifanya hivyo, utazidi kuwa thabiti. Kadiri utakavyozidi kuyapuuza masilahi yako, ndivyo utakavyozidi kuhisi kwamba kama binadamu, unapaswa kuwa na dhamiri na mantiki. Utahisi kwamba bila nia zenye ubinafsi, wewe ni mtu mwaminifu, mwadilifu na unafanya mambo ili kumridhisha Mungu tu. Utahisi kuwa tabia kama hii hukufanya ustahili kuitwa ‘mwanadamu,’ na kwamba katika kuishi duniani kwa njia hii, wewe ni mkweli na mwaminifu, wewe ni mtu halisi, una dhamiri safi, na unastahili mambo yote uliyopewa na Mungu. Kadiri utakavyozidi kuishi kwa njia hii, ndivyo utakavyozidi kuwa thabiti na mchangamfu. Kwa hivyo, je, hutakuwa umetembea kwenye njia ifaayo?(“Mpe Mungu Moyo Wako wa Kweli, Na Unaweza Kupata Ukweli” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). “Ikiwa kweli unaweza kufikiria mapenzi ya Mungu, basi utaweza kuwatendea wengine kwa haki. Ukimpa mtu pendekezo lako, na mtu huyo akuzwe kuwa mtu wa kipaji, na hivyo kuleta mtu mmoja mwingine mwenye kipaji katika nyumba ya Mungu, je, hutakuwa umefanya kazi yako vizuri? Je, basi hutakuwa mwaminifu katika kutimiza wajibu wako? Hili ni tendo jema mbele za Mungu, na ndiyo aina ya dhamiri na mantiki ambazo watu wanapaswa kuwa nazo(“Mpe Mungu Moyo Wako wa Kweli, Na Unaweza Kupata Ukweli” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Maneno ya Mungu yalionyesha waziwazi njia ya kutenda. Napaswa kuacha masilahi yangu mwenyewe na kufikiria masilahi ya nyumba ya Mungu. Napaswa kumpendekeza mtu yeyote ambaye ni hodari kunishinda katika uwanja fulani ili kila mtu mwenye kipaji aweze kutumia uwezo wake katika nyumba ya Mungu na kufanya wajibu wake mdogo katika kueneza injili ya ufalme. Mtu kama huyo pekee ndiye aliye na ubinadamu na ndiye anayezingatia mapenzi ya Mungu na anayeweza kutetea masilahi ya nyumba ya Mungu. Yeye hupata kibali cha Mungu na hilo ni tendo zuri. Nilikwenda kumtembelea Dada Li jioni hiyo hiyo na nikamuuliza iwapo alitaka kwenda kufanya wajibu huo. Alisema kwamba alikuwa tayari kuufanya, lakini aliona wasiwasi kwamba hatafanya vizuri kwani alikuwa mgeni katika imani na kimo chake kilikuwa kidogo. Baada ya kusikia wasiwasi wake, nilishiriki naye juu ya mapenzi ya Mungu, na nikamtia moyo amtegemee Mungu na alenge kutafuta kanuni za ukweli katika wajibu wake. Alienda kufanya wajibu wake mpya siku chache baadaye. Nilifurahi sana, na nikahisi kwamba kuwa na uwezo wa kutenda ukweli na kutoishi kwa ajili ya heshima na hadhi yangu kulikuwa njia pekee ya kuishi kwa uadilifu na heshima. Nilikuwa na amani kabisa moyoni mwangu.

Ninapokumbuka wakati ambapo nilikuwa nikiishi kulingana na tabia yangu potovu, nikiona wivu na kushindania sifa na hadhi kila mara, na kupotoshwa na kuchezewa na Shetani, naona kwamba njia hiyo ya kuishi ilikuwa ya masikitiko. Mungu alipanga watu, vitu, matukio na mazingira ya kila aina ili Anifunue na kuniokoa. Alitumia pia maneno Yake kunifichua na kunihukumu, na kuninyunyizia na kuniruzuku mpaka hatimaye nikawa na ufahamu kiasi wa na ya kustahili dharau, na nikaona asili na matokeo ya kuona wivu na kushindania sifa na faida. Wakati huo tu ndipo nilipoweza kutenda ukweli kidogo na kupata dhamiri na mantiki kidogo.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Kuinuka licha ya kushindwa

Na Fenqi, Korea ya Kusini Kabla ya kumwamini Mungu, nilifundishwa na CCP, na sikufikiria chochote ila jinsi ya kufaulu kutokana na juhudi...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp