Kuzaliwa Upya

16/01/2018

Yang Zheng Mkoa wa Heilongjiang

Nilizaliwa katika familia maskini ya vijijini iliyokuwa nyuma kimaendeleo katika kufikiri kwao. Nilikuwa ovyo kutoka utotoni na hamu yangu ya hadhi ilikuwa hasa yenye nguvu. Baada ya muda, kupitia ushawishi wa jamii na mafunzo ya kitamaduni, nilichukua aina zote za sheria za Shetani za kuponea moyoni mwangu. Aina zote za hoja za uwongo zililea matamanio yangu ya sifa na hadhi, kama vile kujenga nchi nzuri ya asili kwa mikono yako miwili, umaarufu utakufanya kuishi milele, watu wanahitaji nyuso kama mti unavyohitaji ganda lake, kujiendeleza na kuwa juu, mtu anapaswa kuleta heshima kwa mababu zake, nk. Haya hatua kwa hatua yakawa maisha yangu na yakanifanya kuamini kwa thabiti kwamba almuradi tunaishi katika ulimwengu huu, itabidi tufanye kazi ili tuheshimiwe na wengine. Haijalishi tuko katika kikundi kipi ni lazima tuwe na hadhi, inapasa tuwe waliojitokeza zaidi. Kwa kuishi hivi tu ndio tunaweza kuwa wenye uadilifu na heshima. Kuishi maisha kwa njia hii tu ndiko kuna thamani. Ili kutimiza ndoto yangu, nilijifunza kwa juhudi sana katika shule ya asili; kupitia dhoruba na magonjwa, sikuwahi kukosa kuhudhuria darasa. Siku kwa siku, hatimaye nilifikia shule ya kati kwa njia hiyo. Nilipoona kwamba nilikuwa ninaelekea kukaribia ndoto yangu zaidi na zaidi sikuthubutu kuzembea. Nilijiambia mara kwa mara kuwa ilibidi nihimili, kuwa ilibidi nijionyeshe vizuri kwa walimu na wanafunzi wenza. Hata hivyo, wakati huo tu, jambo lisilotazamiwa lilifanyika. Kulikuwa na kashfa kuhusu mwalimu wetu mkuu na mkuu wa shule iliyosababisha vurumai. Walimu na wanafunzi wote walijua kuhusu hiyo. Siku moja darasani, mwalimu huyo alituuliza kama tulikuwa tumesikia kuhusu hiyo na wanafunzi wote wengine walisema “Hapana.” Mimi peke yangu ndiye nilisema kwa uaminifu “Nilisikia.” Kuanzia wakati huo kuendelea, mwalimu huyo aliniona kama mwiba kwa upande wake na mara kwa mara angetafuta vijisababu vya kufanya mambo yawe magumu kwangu, ili kunichukulia hatua kali. Wanafunzi wenza walianza kujitenga nami na kuachana na mimi. Walinifanyia mzaha na kuniaibisha. Hatimaye, sikuweza tena kuvumilia mateso ya aina hiyo na nikaachana na shule. Hivyo ndivyo ndoto yangu ya kujiendeleza na kuwa juu ilivyovunjwa. Nikifikiria kuhusu siku zangu za baadaye huku uso wangu ukiwa kwenye ardhi na mgongo angani, nilihisi huzuni na ghamu isiyoelezeka. Nilifikiri: Inaweza kuwa kwamba maisha yangu yatapitwa kama kawaida tu? Bila hadhi, bila ufahari, bila mafanikio. Haja gani basi ya kuishi namna hii? Kwa kweli sikuwa radhi kukubali ukweli huo wakati huo lakini sikuwa ninajiweza kubadilisha hali zangu. Wakati tu nilipokuwa nikiishi katika uchungu na kutokuwa na matumaini ambayo singeweza kujinasua kwayo, Mwenyezi Mungu aliniokoa na kutia tena tumaini moyoni mwangu ambayo ilikuwa imezimwa. Kutoka wakati huo nilianza maisha mapya kamili.

Ilikuwa Mechi mwaka wa 1999, na kutoka kwa fursa ya bahati niliisikia injili ya siku za mwisho ya Mwenyezi Mungu. Nilipata habari kuwa Mungu mwenye mwili alikuwa amekuja duniani na Yeye Mwenyewe alikuwa akiwazungumzia na kuwaongoza wanadamu ili kutuokoa kutoka kwenye miliki ya Shetani, kuturuhusu kutupa maisha yetu ya kuwa na maumivu, ya kuwa wenye dhambi, kuishi katika mbingu na ardhi mpya. Na kutokana na ushirika wenye ustahamilivu na uangalifu kutoka kwa ndugu zangu, nilisikia ukweli mwingi ambazo sikuwahi sikia hapo awali, kama vile: mpango wa usimamizi wa Mungu wa miaka elfu sita, fumbo la Mungu kuwa mwili, kwamba watu waliopotoshwa wanahitaji wokovu wa Mungu mwenye mwili, ni aina gani ya hisi uumbaji wanapaswa kuwa nayo, jinsi ya kumwabudu Bwana wa uumbaji wote, jinsi ya kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wako halisi, kile ambacho kweli ni maisha ya binadamu…. Nilivutiwa sana na ukweli huu na ulinifanya kabisa kuamini kuwa hii ilikuwa kazi ya Mungu wa kweli. Siku hiyo ndugu zangu pia waliimba wimbo wa uzoefu wa maisha, “Nikifikiri juu ya Siku Chungu za Nyuma na Utamu wa Hivi Sasa, Nampenda Mungu Hata Zaidi”: “Ee Mungu wa vitendo! Nakuomba usikize hadithi yangu. Mimi hulia ninapokumbuka ya kale; moyo wangu ulikuwa wenye giza na bila mwanga; maisha yangu yalikuwa bila matumaini, sikuweza kuzungumza juu ya mateso katika maisha yangu, niliweza tu kupitisha siku bila kujiweza. Ingewezaje kutosababisha moyo wangu maumivu? Ee Mungu wa vitendo! Nisikilize, ninapofikiria mambo ya kale, moyo wangu una maumivu. Ilikuwa Shetani ibilisi aliyekuwa akinidhuru, akinifanya mpotovu na wa kuanguka. Maneno Yako yalinipa nuru na kuniongoza kutoka giza. Ee Mungu wa kweli! Ee Mungu wa kweli! Ninakupenda kutoka ndani ya moyo wangu.” Hii iliangaza nafsi yangu ambayo kwa muda mrefu ilikuwa gizani kama mwali wa mwanga, na singeweza kujizuia kuangua kilio. Miaka mingi ya ukandamizaji, udhalimu, na huzuni ilionekana kuachiliwa huru kwa ghafla. Moyo wangu ulihisi kuwa mwepesi zaidi. Mbali na msisimko huu, nilikuwa mwenye shukrani hata zaidi kwa Mungu kwa kunichagua kutoka miongoni mwa mamilioni ya watu, kukubali nafsi yangu iliyochoka, na yenye huzuni kupata mapumziko vuguvugu. Kutoka wakati huo maisha yangu yakabadilika kabisa. Sikuwa tena mwenye huzuni na wa kuvunjika moyo, ila niliweka akili yangu yote katika kusoma neno la Mungu, kwenda kwenye mikutano, na kushiriki juu ya ukweli. Kila siku ilikuwa kamili na yenye furaha. Baadaye niliinuliwa na Mungu na kuanza kutimiza wajibu wa kuhubiri injili. Kwa sababu nilikuwa mwenye shauku kabisa na mwenye mawazo mema na ukweli kuwa nilikuwa wa uhodari fulani, baada ya kipindi cha muda kazi yangu ilikuwa inazaa matunda kweli. Nilipata sifa kutoka kwa kiongozi wangu wa timu ya injili, na ndugu katika kanisa pia walinienzi. Wangekuwa kila mara wakija kuniuliza kuhusu mambo hawakuwa wakielewa kuhusu kuhubiri injili. Bila kutambua nilianza kuwa wa kujiona kidogo, na nilifikiri: Nimefaidika kwa upesi sana kanisani ile sifa na hadhi niliyotarajia duniani kwa miaka mingi sana. Sehemu yangu ya “ushujaa” hatimaye imepata mahali pake! Nikiona kufanikiwa kwangu nilihisi kama aliyetimiza sana na nilijitahidi hata zaidi kutimiza wajibu wangu. Haijalishi nilikumbana na shida kubwa kiasi gani, ningefanya niwezavyo kuishinda. Haidhuru nini kanisa lililonipangia kufanya, nilitii kwa hiari na kufanya kadri ya uwezo wangu kuikamilisha. Mara nyingine kiongozi wa kanisa alinishughulikia na kupogoa vipengele vyangu kwa sababu sikuwa nimetenda kazi yangu vyema. Haidhuru nilikuwa nimepinduka aje, kijuujuu singeweza kujitolea visababu kwa ajili yangu. Ijapokuwa niliteseka kabisa sana kiasi wakati wa kipindi cha muda huu, mradi nilikuwa na hadhi kati ya ndugu zangu na nilikuwa ninaheshimiwa nao, nilihisi kuwa ilikuwa sawa kabisa kupitia mateso hayo. Lakini Mungu anaweza kubaini kila sehemu ya watu. Ili Aweze kubadilisha maoni yangu yenye kasoro kuhusu maisha na maadili ya binadamu, ili kutakasa uchafu katika imani yangu kwa Mungu na kutekeleza wajibu wangu, Mungu alipanga mazingira mara baada ya nyingine kunihukumu na kuniokoa.

Hiyo ilikuwa mwaka wa 2003, wakati nilipopandishwa cheo kutenda kama kiongozi wa timu yetu ya kiinjili. Pamoja na upandaji cheo huu katika hadhi yangu, upeo wangu wa kazi pia ulienezwa, na nilihisi hata zaidi nimejifurahisha: Dhahabu hung’aa kila mahali. Nina dhamiria kutenda kazi yangu vyema na kupanda kwa hatua ili ndugu zangu waweze kunionea kijicho na kunipenda hata zaidi. Hiyo ingeweza kuwa vyema sana! Wakati nilipofika mahali nilipopaswa kutekeleza wajibu wangu, kiongozi huyo alitia maanani kuwa nilikuwa nimechukua aina hii ya kazi karibuni na nilikosa uzoefu na pia methodolojia, kwa hivyo alikusanya pamoja viongozi wengine kadhaa wa timu ya injili kutoka maeneo ya karibu ili tuweze kujifunza kutoka kwa kila mmoja. Lakini wakati wa ushirika, niliona kuwa wote walikuwa wazee kuliko mimi na kwamba walikuwa wa uhodari duni. Wakati wa ushirika kuhusu maneno ya Mungu pia hawakuzungumza kwa uwazi kama nilivyofanya. Singeweza kujizuia kuwa mwenye kiburi na sikufikiri chochote kuwahusu hata kidogo. Nilihisi kwamba kwa hakika ningeweza kufanya kazi nzuri kwa kutegemea nguvu zangu. Baada ya mkutano nilienda mara moja kwa kila timu ili kupata ufahamu wa kazi yao. Nilipogundua makosa fulani na mambo yaliyoachwa katika kazi zao na kwamba baadhi ya ndugu hawakuwa na uwezo wa kuhubiri injili na kuwa na ushuhuda wa Mungu, nilikuwa na wasiwasi na pia hasira. Singeweza kujizuia kuwakaripia ndugu zangu: “Kutekeleza wajibu wenu namna hii kweli kunaweza kuambatana na mapenzi yake Mungu? Hamtaki kulipa gharama lakini mnataka kuokolewa na Mungu. Mtu wa aina hii ana busara yoyote? …” Na wakati mwingine katika ushirika ningejionyesha, nikiambia kila mtu jinsi nilivyokuwa nimeshiriki katika kazi ya kiinjili, kuhusu matokeo yote niliyoyapata. Nilipoona wivu kwenye nyuso za ndugu zangu, nilijigamba sana na nilihisi kuwa nilikuwa nimewajibika zaidi kuliko wengine. Baada ya muda, ndugu zangu mara zote wangejadiliana masuala yoyote na mimi na sikulenga hata tena kuomba Mungu au kumtegemea Yeye. Na sikukosa tu sikuhisi woga, lakini nilifurahia hilo. Hatimaye, nilipoteza kabisa kazi ya Roho Mtakatifu na kwa kweli sikuweza tena kufanya kazi. Mwanzoni mwa mwaka wa 2004 kanisa liliniondoa kwenye wajibu wangu na kunifanya nirudi nyumbani ili nikatafakari kiroho. Nikiwa nimekabiliwa na tokeo hili, ilikuwa ni kama kwamba nilianguka haraka sana katika shimo la kina kirefu. Mwili wangu wote ulikuwa mlegevu na dhaifu kutokana na hisia kali ya kuvunjika moyo, na sikuweza kujizuia kufikiri: Ilikuwa ni vizuri sana wakati nilipoanza kutekeleza wajibu wangu mara ya kwanza. Na sasa, nikirudi katika aibu hii, nitawezaje kukabili familia yangu na ndugu katika makazi yangu ya kudumu? Watanifikiria aje? Watanifanyia mzaha, wataniangalia kwa dharau? Mara tu nilipofikiria kuhusu kupoteza heshima na hadhi yangu katika akili za watu wengine nilihisi kama nilikuwa karibu kukata tamaa. Nilikuwa nikiishi katika uhasi ambayo singeweza kujinasua kutoka na sikuweza hata kuendelea kusoma maneno ya Mungu. Katikati ya uchungu huu, sikuweza kutomwomba Mungu: “Ewe Mungu! Nimekuwa dhaifu sana sasa na roho yangu iko gizani kwa sababu sina uwezo wa kukubali ukweli kuwa nilibadilishwa cheo. Pia sitaki kutii mipango ya kanisa lakini ninafahamu kuwa chochote Unachofanya ni chema na kina mapenzi yako ya ukarimu. Niko radhi kupata nuru Yako na kuelewa mapenzi Yako.” Baada ya kuomba, maneno haya ya Mungu yaniletea nuru: “Katika kutafuta kwenu, mna dhana, matumaini, na siku za baadaye nyingi sana za kibinafsi. Kazi ya sasa ni ili kushughulikia tamaa yenu ya hadhi na tamaa zenu badhirifu. Matumaini, hadhi, na dhana yote ni mifano bora kabisa ya tabia ya kishetani. … Ingawa mmewasili kwenye hatua hii leo, bado hamjaacha hadhi lakini mnapambana bila kukoma kuuliza kuihusu, na mnaichunguza kila siku, kwa hofu kubwa kwamba siku moja hadhi yenu itapotea na jina lenu litaharibiwa. … Sasa nyinyi ni wafuasi, na mmepata ufahamu fulani wa hatua hii ya kazi. Hata hivyo, bado hamjaweka kando tamaa yenu ya hadhi. Wakati hadhi yenu iko juu mnatafuta vizuri, lakini wakati hadhi yenu iko chini hamtafuti tena. Baraka za hadhi daima ziko katika fikira zenu. Kwa nini watu wengi hawawezi kujiondoa katika uhasi? Je, si jibu bila shaka ni kwa sababu ya matarajio ya kuvunja moyo?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mbona Huna Hiari ya Kuwa Foili?). Ile hukumu iliyofichuliwa katika maneno ya Mungu ilinipa utambuzi wa ghafla wa ukweli usiopendeza, na kunifanya kuelewa kwamba kazi ya Mungu wakati huo ulikuwa kushughulikia matamanio yangu ya hadhi, kunifanya kuingia katika njia ya kufaa katika maisha. Nikifikiria nyuma kwa wakati tangu nilipoanza kutekeleza wajibu wangu, nilikuwa vyema sana wakati nilikuwa na hadhi. Nilikuwa na ujasiri sana na sikuogopa mateso wala dhiki. Nilipokumbwa na mtu akinishughulikia au kupogoa vipengele fulani kunihusu sikuzuia hilo. Lakini tena, baada ya kuachiliwa na nilibidi kurudi nyumbani sikuweza kujinasua kutoka kwa uhasi wangu. Niliona kwamba kwa nje ilionekana kuwa nilikuwa nikitekeleza wajibu wangu, lakini kwa kweli nilikuwa nikipeperusha bendera ya kutekeleza wajibu wangu wakati nilipokuwa nikisimamia mambo mwenyewe. Ilikuwa kabisa kumtumia Mungu kukidhi matamanio yangu ya kibinafsi ambayo yalikuwa yamefichwa kwa miaka mingi—kuenda mbele na kuheshimika sana. Na haikuwa kufuatilia ukweli na ilikuwa hata zaidi si kutekeleza wajibu wa kiumbe ili kutimiza Mungu. Wakati nilipokuwa nikitekeleza wajibu wangu na nikaona upungufu wa ndugu zangu, sio tu kwamba sikuwasaidia kutokana na upendo, lakini nilitegemea hadhi yangu kuwakashifu. Nilijiinua kwa makusudi, nikajisimamia kama shahidi kwa nafsi yangu, na nilikuwa na wasiwasi wa kila mtu kuniheshimu na kunienzi. Kuanzia mwanzo hadi mwisho, nilikuwa na lengo moja tu katika mawazo na matendo yangu—huku hakukuwa kumpinga Mungu bila kuficha? Wanadamu waliumbwa na Mungu, kwa hivyo tunapaswa kumwabudu na kumtazamia. Mioyo yetu inapaswa tu kuwa na hadhi ya Mungu, lakini nilikuwa mtu mchafu na mwovu, mwenye hali ya chini aliyetaka kuwa na nafasi katika mioyo ya wengine. Huku si kukuwa na kiburi mno? Hii si ya kufedheheshana na kuwa kinyume na Mungu? Hii tabia si kosa kubwa kwa tabia ya Mungu? Nilipofikiri hayo, sikuweza kujisaidia kutetemeka na hofu kwa sababu ya asili yangu yenye kiburi. Ilitokea kuwa tayari nilikuwa katika hali hiyo hatari ya kuwa kwenye uelekeo wa adhabu ya Mungu! Tabia ya Mungu ni ya haki na takatifu na haivumilii makosa ya binadamu. Angewezaje kuvumilia kuniruhusu mimi, mtoto huyu mwasi, kuvuruga tele na kufadhaisha kazi Yake? Hapo tu ndipo nilipobaini kwamba kuachiliwa kulikuwa ni uvumilivu mkubwa na upendo mkubwa wa Mungu. Vinginevyo, ningefanya maovu zaidi na makuu hadi kiwango ambacho Hangeweza kunisamehe. Kisha kungekuwa kumechelewa mno. Nilipofikiri zaidi juu ya hilo ndivyo nilivyoogopa zaidi, na ndivyo nilivyohisi zaidi kuwa nilikuwa na deni ya Mungu sana. Sikuweza kujizuia kusujudu mbele Yake na kuomba: “Ee Mungu! Asili yangu ni ya kiburi sana, ya kijuujuu sana. Sijafuatilia ukweli wakati wa kutekeleza wajibu wangu, na sijafikiri kulipiza upendo Wako. Nilikuwa nikijishughulisha nikikimbia hapa na pale kwa ajili ya sifa na hadhi, na nilidhamiria kuwa mbele kanisani, kwa hivyo ningewezaje kukosa kujikwaa na kuanguka wakati wa kutekeleza wajibu wangu nikiwa na nia hiyo? Kama hukumu na kuadibu Kwako, na ushughulikiaji na kupogoa Kwako hakungenijia kwa wakati ufaao, hakika ningeendelea katika njia ya adui ya Kristo. Mwishowe ningeharibu nafasi yangu ya wokovu. Ee Mungu! Ninakupa shukrani kwa ajili ya rehema Yako na wokovu Wako kwangu. Kuanzia siku ya leo kwendelea, niko tayari kuachana na matamanio yangu makuu na kufuatilia ukweli, na kukubali zaidi hukumu na adabu Yako, kupata mabadiliko katika tabia yangu potovu hivi karibuni.” Nuru na mwongozo wa Mungu uliniondoa katika uhasi wangu na kuniruhusu kutambua kiasi asili yangu ya kiburi na kiini changu cha kumpinga Mungu. Pia nilipata ufahamu kiasi wa tabia ya haki ya Mungu, na nilihisi ufunguliwaji mno katika moyo wangu. Nilikuwa pia radhi kuendelea kutafuta ukweli katika mazingira yoyote ambayo Mungu angeniandalia, na kuelewa kwa undani zaidi mapenzi Yake.

Katika ufuatiliaji wangu baada ya hayo, niliona maneno kutoka kwa Mungu yaliyosema: “Ninaamua hatima ya kila mtu si kwa kuzingatia umri, ukubwa, kiwango cha mateso, sembuse kiwango ambacho kwacho anataka huruma, bali kulingana na ikiwa anao ukweli. Hakuna chaguo lingine ila hili. Sharti mtambue kwamba wale wote ambao hawafuati mapenzi ya Mungu wataadhibiwa pia. Huu ni ukweli usiobadilika(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Tayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako). “Kama kiumbe wa Mungu, mwanadamu anapaswa kutafuta kutekeleza wajibu wa kiumbe wa Mungu, na kutafuta kumpenda Mungu bila kufanya chaguo lingine kwa kuwa Mungu anastahiki upendo wa mwanadamu. Wale ambao wanatafuta kumpenda Mungu hawapaswi kutafuta faida zozote za kibinafsi au lile ambalo wanatamani binafsi; hii ndiyo njia sahihi kabisa ya ufuatiliaji(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mafanikio au Kushindwa Kunategemea Njia Ambayo Mwanadamu Hutembea). Maneno ya Mungu yalikuwa tayari yamewaambia watu kwa uwazi kabisa na kwa njia inayoeleweka mapenzi na mahitaji yake yaliokuwa yapi ili wanadamu wangeweza kuelewa njia mwafaka ya ufuatiliaji na njia gani iliyo mbaya. Wakati huo niliweka sifa na hadhi juu ya kila kitu, lakini kwa kweli, Mungu hakuangalia jinsi hadhi ya mtu ilivyokuwa juu, ni aina gani ya ukubwa aliokuwa nao, au alipitia kiasi gani cha mateso katika imani yake kwa Mungu. Aliangalia kama alifuata ukweli na alikuwa na ufahamu wa kweli wa Mungu au la. Wale walio na ukweli lakini hawana hadhi ya juu pia wanaweza kupata sifa Yake, lakini wale wasiokuwa na ukweli na wana hadhi ya juu ndio ambao Mungu huwachukia na kuwakataa. Hii ndiyo tabia Yake Mungu ya haki na utakatifu. Hadhi haiwezi kuamua majaliwa ya mtu, wala si ishara ya wokovu wa mtu katika imani yao kwa Mungu. Hasa sio alama ya mtu ambaye amekamilishwa na Mungu. Lakini mara mingi nilikuwa nimetumia hadhi yangu kupima thamani yangu na furaha yangu kuu ilikuwa kuheshimiwa na kupendwa na wengine. Hii haikuwa kinyume kabisa na mahitaji ya Mungu? Kutoamini Mungu hivi haikuwa bure bilashi kabisa? Singeweza tu kutoweza kuokolewa na Mungu, lakini mwishowe ningekumbwa na adhabu ya Mungu kutokana na njia zangu mbaya. Wakati huo, kile ambacho Mungu alikuwa ameniaminisha nacho kilikuwa kuniruhusu niingie katika ukweli, kuwa na uwezo wa kufuatilia mabadiliko katika tabia, kufuatilia utiifu kwa na upendo wa Mungu, na mwishowe kuokolewa na kukamilishwa na Yeye. Huu tu ndio uliokuwa njia mwafaka. Baada ya kuelewa haya yote, moyo wangu ulijawa na shukrani kwa Mungu. Shukrani kwa hukumu na adabu Yake iliyonitoa katika njia mbaya na kunipa nuru ili nipate kuelewa mapenzi Yake, kuniruhusu hatimaye kuona kwa wazi hatari na matokeo ya kufuatilia sifa na hadhi. Hapo tu ndipo niliweza kuamka na kugeuka kwa wakati ufaao. Kupitia tukio hilo nilikuwa na ufahamu kiasi wa maoni yangu yenye makosa kuhusu kufuatilia, nikaelewa ukweli kiasi pamoja na nia zake Mungu za ukarimu, na hali yangu ya akili ilipata nafuu mara nyingine tena. Nilijitosa katika kutekeleza wajibu wangu tena.

Mnamo Julai mwaka wa 2004 nilikwenda eneo ya mbali katika milima na kushirikiana na ndugu huko kuhusu kazi ya injili. Wakati nilianza hiyo kazi, nilitia maanani kushindwa kwangu kwa awali kama mafunzo. Nilijikumbusha mara nyingi kutofuatilia sifa wala hadhi lakini kutekeleza wajibu wangu kwa uaminifu kama kiumbe, kwa hivyo wakati kulikuwa na masuala ambayo sikuelewa au sikuwa na hakika nayo, ningejitoa na kutafuta kikamilifu ndugu yangu ili tufanye ushirika, ili tuyajadili na tuyatatue. Lakini kadri kazi yangu ilivyoendelea kuzalisha matunda zaidi na zaidi, asili yangu ya kiburi ilijitokeza tena na nilianza kutia maanani taswira yangu binafsi na hadhi yangu tena. Wakati wa mkutano siku moja, mwanachama wa timu ya mahali hapo ya kiinjili aliniambia kwa furaha: “Kwa ajili ya wewe kuja hapa tumewabadili waumini zaidi….” Kinywa changu kilisema kuwa haya yalikuwa matokeo ya kazi ya Roho Mtakatifu, lakini moyoni mwangu nilifurahishwa sana nami. Baada ya mkutano kukamilika na nikarudi kwa nyumba ya mwenyeji wangu, niliketi juu ya kitanda changu na kuchezesha tena katika akili yangu kila tukio la kazi yangu wakati huo. Singeweza kuzuia kujipongeza, nikifikiri: Inaonekana nina uwezo wa kweli katika kazi hii. Almuradi ninaendelea kufanya kazi kwa bidii, bila shaka ninaweza kupandishwa cheo tena. Nilijiona basi kama shujaa kabisa, na hadhi ya Mungu ilikuwa tayari imeniondoka moyoni mwangu. Wakati wa kutekeleza wajibu wangu baada ya hayo, nilianza kushindana kupata hadhi na kulinganisha vyeo na wafanyikazi wenzangu. Nilianza kujionyesha kwa wazi mbele ya ndugu zangu kama kwamba matokeo yoyote kutoka kwa kazi yetu yalikuwa yote kwa sababu ya jitihada zangu. Wakati tu nilipokuwa nikirudi nyuma katika lindi kuu hatua moja kwa nyingine, Mungu mara nyingine tena alininyoshea mkono wa wokovu kwangu. Jioni moja nilipatwa na homa kubwa kwa ghafla. Halijoto yangu ilifikia digrii 102 na hata baada ya kunywa dawa kwa siku kadhaa sikupata afueni. Nilienda hospitalini kupata unyweshaji, lakini hali yangu haikukosa kupata nafuu tu lakini ikawa mbaya zaidi. Sikuweza kushikilia chochote tumboni, hata maji. Hatimaye, nilikuwa mgonjwa kitandani na nilihisi kama kwamba nilikuwa nimetimia kifo. Katika mateso ya maradhi hayo, sikuweza tena kufikiri aina gani ya hadhi ningekuwa nayo siku zingefuata. Nilipiga magoti haraka na kumwomba Mungu: “Ewe Mungu! Huu ugonjwa unaonijia ni mapenzi Yako yenye ukarimu pamoja na tabia Yako yenye haki. Sitaki kutokuelewa au kukulaumu; ninakuomba tu unipe nuru na Uniangazie tena, uniruhusu nipate kuelewa mapenzi Yako ili niweze kuelewa hata zaidi upotovu wangu mwenyewe.” Baada ya kuomba, moyo wangu ulikuwa na amani zaidi. Wakati huo tu, maneno haya ya Mungu ghafla yalinijia: “Asili zenu za majivuno na kiburi huwaelekeza kusaliti dhamiri zenu wenyewe, kuasi na kumpinga Kristo, na kufichua uovu wenu, hivyo basi kuleta kwenye mwangaza fikra zenu, mawazo, tamaa nyingi na macho yaliyojaa ulafi(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?). Kila moja ya maneno haya kutoka kwa Mungu yalidunga moyo wangu kama upanga; yaligonga katika mahali pangu pa kunifisha. Kila aina ya ubaya wa kiburi niliokuwa nimefichua ulinijia kwenye akili kwa uwazi mkubwa. Moyo wangu ulikuwa na uchungu na niliaibika na kufedheheshwa kupindukia. Ilikuwa hapo nilipoona kwa wazi kuwa ilikuwa ni asili yangu yenye kiburi ambayo ilisababisha dhamiri yangu kupoteza utendaji wake wa asili hadi sikuwa na uwezo wa kutii na kumwabudu Mungu mara kwa mara kwa uaminifu. Hii ilinisababisha daima kuhodhi lengo na matamanio, na punde tu nilipopata fursa ningeshindania hadhi, na nilitaka kujionyesha na kuwakandamiza wengine. Singeweza tu kuwa mtu mwenye tabia nzuri. Ilikuwa wazi kuwa matunda yoyote ya kazi yangu yalitegemea kazi ya Roho Mtakatifu; ilikuwa ni baraka za Mungu. Hata hivyo, bila haya niliiba utukufu wa Mungu, kutumia hiyo fursa kujiinua, na kufurahia ndugu zangu kuniheshimu na kuniabudu: Niligeuka kuwa mwenye kiburi sana kiasi kwamba nilipoteza busara yangu. Hapo tu ndipo nilitambua kwamba asili hii yangu ya kiburi ilikuwa hasa ndio kiini cha upinzani wangu kwa Mungu. Ikiwa singeitatua, singewahi kufikia utiifu kwa Mungu au uzatiti wa kutimiza wajibu wangu.

Chini ya uongozo wa Mungu, mara nyingine tena nilifikiria maneno Yake: “Wakati mtu anapotambua asili yake ya kweli ilivyo—jinsi ilivyo mbaya, jinsi inavyostahili kudharauliwa, na jinsi ilivyo ya kusikitisha—basi yeye si mwenye majivuno sana, hajigambi ovyo ovyo sana, hajifurahii kama hapo awali. Mtu kama huyo huhisi, ‘Lazima niwe mwenye ari na mpole, na nitende baadhi ya maneno ya Mungu. Kama sivyo, basi siwezi kufikia kiwango cha kuwa mwanadamu, na nitaona aibu kuishi mbele ya Mungu.’ Kwa hakika mtu hujiona kuwa hafifu, kama kweli asiye na maana. Wakati huu, inakuwa rahisi kwake kutekeleza ukweli, naye ataonekana kwa kiwango fulani kuwa kama mwanadamu anavyopaswa kuwa(“Kujijua Mwenyewe Hasa Ni Kujua Asili ya Binadamu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Maneno ya Mungu yalinielekeza kwa njia ya utendaji na kuingia ndani, na kama nilitaka kuacha kabisa mawazo yangu ya sifa na hadhi, ingebidi kutia juhudi katika kujua asili yangu mwenyewe. Wakati ningeweza kuona kweli vile nilivyokuwa duni, bure, ningeweza kuwa mtu mtulivu na singekuwa tena na kiburi. Kisha, ningeweza kufuatilia ukweli nikiwa imara kabisa. Ukweli ni kuwa, Mungu kunitia adhabu hii ya hukumu na adabu, pigo hili na nidhamu, ilikuwa kwa ajili ya mimi kuwa na ufahamu wa kweli wa nafsi yangu mwenyewe na utambulisho wangu wa asili na hadhi. Ilikuwa ili kuniruhusu kuwa na ujuzi wa kibinafsi mbele ya Mungu, ili niweze kutambua umasikini wangu wa roho, hali yangu ya kutokuwa na thamani. Ilikuwa kuniruhusu kutambua kwamba kile nilichohitaji kilikuwa ni ukweli, wokovu wa Mungu, ambapo ningeweza kuanguka chini mbele ya Mungu na kuwa mtu mwenye tabia njema. Ilikuwa ili niweze kutekeleza wajibu wangu kumtosheleza Mungu na kutofuatilia tena hadhi, hivyo kuumiza moyo Wake. Chini ya uongozi wa maneno Yake nilikuwa na njia ya kuenda mbele pamoja na ujasiri wa kufuatilia ukweli. Hata ingawa nilikuwa nimepotoshwa sana na Shetani na asili yangu ya kiburi ilikuwa madhubuti sana, almuradi nilikuwa na uwezo wa kukubali na kutii hukumu na adabu wa Mungu na majaribu na usafishaji Wake, kutoka hapo kutambua asili yangu mwenyewe na nafsi, na kisha kufuatilia ukweli bila kuchoka, bila shaka ningeweza kufumua vifungo na mateso ya sifa na hadhi, na kuingia katika njia ya kuokolewa, ya kukamilishwa. Baada ya kumrudia Mungu, nilipata nafuu kutoka kwa ugonjwa wangu ndani ya siku mbili. Hii ilinifanya kugundua hata zaidi kwamba alikuwa ametumia ugonjwa huo kama njia ya kunifundisha nidhamu. Haikuwa kunifanya niteseke kwa makusudi, wala hakukuwa na adhabu yoyote ndani yake—ilikuwa ni kuamsha moyo wangu ulioganda, kunifanya kuacha ufuatiliaji wangu wenye kasoro haraka iwezekanavyo na niingie katika njia ya kweli ya kumwamini Mungu. Nilisisimuliwa sana na kuamshwa na mapenzi ya Mungu. Kwa unyoofu mno nilimpa Mungu shukrani zangu na sifa.

Baada ya kupona kutoka kwa ugonjwa wangu nilijirusha tena katika kazi. Niliamua kimoyomoyo kuwa wakati nitakapopatana na jambo litakalohusisha sifa au hadhi, hakika ningemshuhudia Mungu. Miezi kadhaa baadaye, niligundua kuwa timu nyingine ya kiinjili ilikuwa inapata matokeo mazuri sana na ilikuwa imeshuhudia matendo fulani ya ajabu ya Mungu, na ilikuwa imefanya muhtasari wa baadhi ya matukio yao yenye mafanikio na njia zao za utendaji. Hata hivyo, kazi niliyokuwa nikishiriki katika ilikuwa ikididimia. Nilipoona masikitiko katika nyuso za ndugu zangu, hasa niliposikia dada mmoja akisema “Sasa sisi tunafurahia wokovu mkubwa kutoka kwa Mungu lakini hatuwezi kuwa na ushuhuda wa kazi Yake. Kwa kweli sisi tumewiwa Kwake,” na kila mtu hawangeweza kujizuia kulia, moyo wangu ulikuwa una maumivu sana. Sikujua jinsi ya kujiondoa katika mashaka hayo, na nilimwomba Mungu mara kwa mara: “Ewe Mungu! Sisi sote ni wanyonge wakati tunakabiliwa na matatizo ya kiutendaji, lakini ninajua kuwa huyu ni wewe anayejaribu imani yetu, anayepima mapenzi yetu. Lakini kimo changu ni kidogo mno na siwezi kabisa kuubeba mzigo huo. Ninakuomba unipe nuru ili nielewe mapenzi Yako. Niko radhi kutenda kulingana na mwongozo Wako.” Baada ya kuomba, wazo lilinijia kwa ghafla: Ninafaa kumwuliza mfanyakazi mwenza hapo aje ashirikiane nasi katika ushirika ili tuweze kupata baadhi ya nguvu na tajriba zake. Kwa njia hiyo ndugu pia wataweza kufurahia kupata nuru na mwongozo wa Roho Mtakatifu na kujua jinsi ya kufanya kazi zao za injili. Nilijua kwamba mawazo haya yalitokea kutoka kwa mwongozo wa Roho Mtakatifu, lakini bado nilikuwa na mashaka moyoni mwangu. Nilifikiri: Nilikuwa na uwezo zaidi kuliko ndugu huyo kwa kila namna na wakati tulipokuwa kwenye mikutano pamoja ningemdharau, lakini sasa, utendaji wake ni bora kuliko wangu. Wakati ananiona nikionekana mwenye kukata tamaa na kuwa na aibu sasa, atanicheka? Ndugu watanidharau? Je, kuhusu nini kuokoa heshima yangu? … Nilifikiri na kufikiri, na bado sikuweza kuachana na wazo langu la heshima na hadhi yangu, lakini mara tu nilipofikiri juu ya mapenzi ya dharura ya Mungu ya kuwaokoa wanadamu na kuwa ndugu zangu hawakuwa na mwongozo na uongozi wa Roho Mtakatifu, niliadibiwa ndani ya moyo wangu. Wakati tu nilipokuwa nikiyumbayumba, maneno haya kutoka kwa Mungu yalinipa nuru: “Roho Mtakatifu hafanyi kazi tu kwa baadhi ya wanadamu wanaotumiwa na Mungu, lakini hata zaidi kanisani. Anaweza kuwa akifanya kazi kwa yeyote. Anaweza kufanya kazi ndani yako sasa, na baada ya wewe kuwa na uzoefu nayo, Anaweza kufanya kazi ndani ya mtu mwingine ajaye. Fanya hima ufuate; unapozidi kufuata mwangaza wa sasa, ndivyo maisha yako yanaweza ku kua. Haijalishi yeye ni mwanadamu wa aina gani, alimradi Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yake, kuwa na hakika kufuata. Chukua uzoefu wake kupitia wako mwenyewe, na utapokea mambo ya juu hata zaidi. Kwa kufanya hivyo utaona ukuaji haraka zaidi. Hii ni njia ya ukamilifu kwa mwanadamu na njia ambayo maisha hukua. Njia ya ukamilifu inafikiwa kupitia utii wako wa kazi ya Roho Mtakatifu. Hujui ni kupitia kwa mtu wa aina gani ndiyo Mungu Atafanya kazi kukukamilisha, wala kupitia mtu yupi, tukio, ama jambo ndiyo Atakuwezesha kuingia katika umiliki na kupata ufahamu fulani(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Wanaomtii Mungu kwa Moyo wa Kweli Hakika Watapatwa na Mungu). Chini ya uongozi kutoka kwa maneno ya Mungu nilielewa dhamira Yake na nilipata ufahamu fulani wa jinsi ya kuongoza na kuwakamilisha watu katika kazi ya Roho Mtakatifu. Niligundua: Kazi ya Mungu na hekima ya Mungu ni ya ajabu na ya miujiza. Sijui ni kutumia aina gani ya mtu au kitu Yeye atanipatia nuru na kuniongoza kuelewa dhamira Yake, wala sijui ni kwa aina gani ya mazingira atashughulika na tabia yangu potovu. Ni lazima nijifunze kutii kazi ya Roho Mtakatifu, na haijalishi ni ukubwa au udogo jinsi hadhi ya mtu ilivyo, umri wake ni upi, ama kwa muda gani ameamini Mungu, almuradi ushirika wake unakubaliana na ukweli, ni mapenzi Yake Mungu ya sasa, na yanaweza kutuonyesha njia ya utendaji, inayotokana na kazi na nuru ya Roho Mtakatifu. Ni lazima nikubali, nitii, na kutenda–hii ndiyo mantiki ya binadamu ambayo lazima nimiliki. Nisipotii kazi ya Roho Mtakatifu, basi niko radhi kukubali kazi yangu kuwa hatarini ili kudumisha ubatili wangu mwenyewe. Niko radhi kukubali ndugu zangu kuishi katika giza ili niweze kudumisha taswira na hadhi yangu. Katika hali hiyo, mimi ni mtumishi mbaya kupindukia kweli na mpinga Kristo! Nilipogundua hayo, sikuweza kujizuia kuhisi uoga na sikuthubutu tena kwa mara nyingine kuwa mkaidi na kwenda kinyume na kupata nuru na mwongozo wa Roho Mtakatifu. Nilikuwa radhi kuacha asili yangu ya kishetani na kufariji moyo wa Mungu kupitia utendaji halisi. Kwa hivyo, nilimwita mfanyakazi mwenza huyo mara moja na kumsihi aje awasiliane nasi. Kilichonifanya nione haya ni kwamba baada ya kukutana uso kwa uso, ndugu huyo hakunidharau hata kidogo wala kunicheka. Alishirikiana kwa uhalisi kabisa katika ushirika jinsi walivyokuwa wamefanya kazi pamoja wakati Roho Mtakatifu alifanya kazi kati yao, na jinsi walivyomtegemea Mungu na kumwomba Mungu walipokutana na vipingamizi na ushinde, ni matendo gani waliyoyaona kutoka kwa Mungu baada ya hayo, ni aina gani ya mapatano ya kweli waliyoyapata kuhusu Mungu, na zaidi. Nikiona sura ya kaka yangu imetulia na kujawa na furaha, kisha nikiona kuwa ndugu zangu walionekana kusikiliza kwa makini na kwa kuvutiwa, kisha kuona tabasamu zikijitokeza asteaste kwenye nyuso zao, nilihisi maumivu makali kama kwamba nilikuwa nimevunjika moyo. Hata hivyo, wakati huu haikuwa kwa ajili ya kuukidhi heshima au hadhi yangu, ila ni kwa sababu nilikuwa nimekemewa moyoni mwangu kutokana na kuwiwa kwa Mungu. Kwa sababu ya haya, kwa kweli nilipitia ile jukumu na wajibu unaotekwa kiongozi mzuri. Ikiwa barabara ninayochukua binafsi si sahihi, itaudhuru na kuharibu maisha ya watu wengi sana. Italeta mateso ya kiroho kwa watu wengi sana. Kwa hivyo basi, mimi sijakuwa mhalifu mkuu wa kumpinga Mungu? Wakati kazi ya Mungu imekamilika, ninapaswa kutoa maelezo kwake vipi? Ilikuwa ni wakati huo ambapo hatimaye nilijichukia kabisa ndani ya moyo wangu. Nilijichukia kwamba hapo awali nilipokuwa nikitekeleza wajibu wangu sikujishughulisha kwa uaminifu katika kazi yangu lakini nilifikiri tu ufuatiliaji wa sifa na hadhi na kufurahia katika baraka za hadhi. Sio tu kwamba ilikatiza kuingia kwa ndugu na zangu katika maisha, lakini hata zaidi ilikatiza kutenda mapenzi ya Mungu. Nilikuwa pia nimepoteza mara nyingi mshiko wa kazi ya Roho Mtakatifu na kuanguka katika giza. Niliona kwamba ufuatiliaji wa sifa na hadhi ulifanya madhara mengi zaidi kuliko mema. Lakini wakati nilikuwa ninahisi hatia na huzuni, pia nilihisi kuwa na chembe cha faraja. Hii ilikuwa kwa sababu, chini ya uongozi wa Mungu, nilikuwa mwishowe nimeacha faida ya kibinafsi ili niweke ukweli katika vitendo wakati huu mmoja. Nilikuwa nimetenda jambo ambalo lilikuwa la manufaa kwa kazi, kwa ndugu zangu, na kwangu. Nilikuwa nimemwaibisha Shetani kupitia vitendo vya kiutendaji na nilisimama kama shahidi wa Mungu wakati huu.

Katika uzoefu wangu wa kazi ya Mungu na kwa sababu ya kufuatilia kwangu sifa na hadhi, nilikuwa nimepitia vipingamizi vingi na kushindwa. Nilikuwa nimechukua mizunguko mingi, na kwa sababu ya haya nilikuwa nimepitia kushughulikiwa na kutakaswa. Hatua kwa hatua, niliona hadhi kama kitu kisicho na umuhimu sana, na yale niliyoyaamini hapo awali—bila hadhi hakukuwa na mategemeo ya baadaye na hakuna mtu atakayekutazamia—mtazamo huu uliopotoka uligeuzwa. Nimemfuata Mungu sasa kwa miaka 15. Kila wakati ninapofikiri kazi ya Mungu kwangu, kuna hisia nzuri daima ambayo inayonijia. Sitawahi kamwe kusahau upendo wa Mungu na wokovu kwangu. Kama haingekuwa kwa ajili ya Mungu kubuni mazingira yangu na kushughulikia hamu zangu za umaarufu, faida na hadhi katika hatua za mwanzo za maisha yangu, ningewezaje kuwa radhi kuacha imani ambayo nimeishi nayo kwa miaka mingi na ambayo imekuwa maisha yangu? Kama haingekuwa kwa ajili ya wokovu wa Mungu kunijia kwa wakati, bado ningekuwa ninaendelea kuishi kulingana na sumu za Shetani, na kupoteza maisha yangu kwa ajili ya ndoto ambayo haingeweza kufikiwa. Na kama haingekuwa kwa ufunuo na usafishaji wa mara kwa mara kutoka kwa Mungu, ningekuwa bado ninaendelea kusonga mbele kwa njia yenye makosa na singeweza kamwe kufahamu jinsi kiburi changu kilivyokuwa cha hatari na jinsi tamaa yangu ya hadhi ilivyo na nguvu. Mimi hasa singetambua kwamba mimi ni adui wa Mungu. Ilikuwa kazi ya ajabu ya Mungu ambayo iliyoniwezesha kubaini asili na madhara mengi ya kufuatilia umaarufu, faida na hadhi. Iliruhusu maadili na mitazamo yangu yenye kasoro kuhusu maisha kupitia mabadiliko makubwa, na iliniruhusu kuelewa kwamba ni ufuatiliaji tu wa ukweli na kutekeleza wajibu wa kiumbe ndio uhai wa kweli wa binadamu, na kwamba ni kwa njia ya kuachana na ushawishi mbovu wa Shetani na kuishi kulingana na maneno ya Mungu tu ndio naweza kuishi na maana na kwa thamani. Ni kwa sababu ya matunda ya hukumu na adabu ya Mungu kabisa ndio ninaweza kuwa na uelewa na mabadiliko ninayo leo. Ingawa kupitia hukumu na adabu ya Mungu kulihitaji nipitie uchungu wa utakaso, nimepata ufahamu fulani wa kazi ya utendaji wa Mungu, ya nafsi Yake ya ukarimu, na tabia Yake ya haki na utakatifu. Sasa nina uwezo wa kuona wazi, kuchukia, na kuyatupa sumu za Shetani zilizonidhuru kwa miaka mingi, na nina uwezo wa kuwa na maisha ya kweli ya binadamu. Hakuna mojawapo ya haya yalifanyika bure. Kilikuwa kitu chenye cha maana mno, cha thamani zaidi. Nikiwa njiani kuanzia leo kuendelea, niko radhi kukubali zaidi ya hukumu na adabu, na majaribio na utakaso unaotoka kwa Mungu ili kila aina ya tabia yangu mbovu iweze kutakaswa hivi karibuni, na niweze kuwa mtu ambaye anaambatana na Mapenzi ya Mungu.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Masumbuko Makali ya Milele

“Roho zote ambazo zimepotoshwa na Shetani ziko chini ya udhibiti wa miliki ya Shetani. Ni wale tu wanaomwamini Kristo ndio waliotengwa...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp