Ishara za Nyakati za Mwisho: Mwezi Mkuu wa Damu Kutokea tena mnamo 2021

26/05/2021

Ujumbe wa Mhariri: Katika miaka ya hivi karibuni, katika upeo wa mbingu “mwezi wa damu” umeonekana mara kwa mara. Majanga mbalimbali kama vile magonjwa ya mlipuko, tetemeko ya ardhi, na njaa zinazidi kuwa mbaya. Unabii wa Biblia kuhusu siku za mwisho tayari umetimia, na siku kuu na ya kutisha ya Yehova iko karibu. Majanga makubwa sasa iko juu yetu, kwa hivyo tunapaswaje kukaribisha kurudi kwa Bwana? Nakala hii ina jibu.

Ishara za Nyakati za Mwisho: Mwezi Mkuu wa Damu Kutokea tena mnamo 2021

Kama ilivyotabiriwa na wataalam husika, mnamo Mei 26, 2021, jambo nadra litafanyika angani: Mwezi mkuu wa damu , mwezi mkuu zaidi wa damu mwaka huu, utaonekana wakati wa kupatwa kamili kwa mwezi. Habari inayohusiana inasema kwamba neno “Mwezi Mkuu” linamaanisha wakati mwezi kamili unapoelekea karibu na dunia, wakati ambapo kipenyo dhahili cha mwezi kinachoonekana ni 14% kubwa kuliko kawaida na mwangaza wake pia huongezeka kwa 30% - ni mviringo mkubwa kabisa wa mwezi unaoonekana kwa macho. Mnamo Mei 26 mwaka huu, mwezi wa damu utatokea wakati wa kupatwa kabisa kwa mwezi, kwa hivyo huitwa pia mwezi mkuu wa damu, ambayo ni nadra sana kuona angani. Kwa kweli, vituko vya ajabu kama vile miezi ya damu na miezi mikuu imekuwa ikionekana mara kwa mara kwa miaka ya hivi karibuni, kwa mfano miezi ya damu ya 2011 na 2013, safu ya miezi minne ya damu ambayo ilionekana kupitia 2014 na 2015, mwezi mkuu wa damu 2018, ambayo pia ilitokea miaka 152 iliyopita, na mwezi mkuu wa mbwa mwitu wa damu ulionekana mnamo tarehe 21 Januari 2019 ambayo iliunganisha kabisa vituko vitatu vya angani vya mwezi mkuu, mwezi wa damu na mwezi wa mbwa mwitu, na ilisifiwa kama maajabu ya kushangaza zaidi ya anga.

Manabii wengi wametabiri kuwa kuonekana kwa miezi ya damu kunaashiria matukio na makubwa ya kushangaza yanayokuja. Pia kuna wataalam wengi wa Biblia ambao wanaamini kabisa kwamba kuonekana kwa miezi ya damu ni utimilifu wa unabii katika Kitabu cha Yoeli 2: 29-31: “Na pia juu ya watumishi wa kiume na wa kike nitamwaga roho wangu katika siku zile. Na nitaonyesha maajabu mbinguni na duniani, damu, na moto, na miimo ya moshi. Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja kwa siku kuu na ya kutisha ya Yehova.” Pia katika Ufunuo 6:12 inasema “Na nikaona wakati ambapo alikuwa ameufungua muhuri wa sita, na, tazama, kulikuwa na tetemeko kubwa la ardhi; na jua likageuka kuwa jeusi kama gunia la nywele, na mwezi ukageuka kuwa kama damu.” “Siku kuu na ya kutisha” iliyotajwa katika unabii katika Kitabu cha Yoeli inahusu majanga makubwa. Sote tumeona majanga yakiongezeka kwa kiwango katika miaka michache iliyopita, na kutokea mara kwa mara kwa majanga kama vile matetemeko ya ardhi, njaa, magonjwa na mafuriko ambayo ni ya kutisha kwetu kushuhudia; hali ya ulimwengu iko katika machafuko na inabadilika kila wakati, kuna kuzuka kwa vita mara kwa mara, visa vya vurugu na mashambulizi ya kigaidi ambayo inaendelea kuongezeka; hali ya anga inazidi kupata joto, na hali ya hewa iliyokidhili mno na kila aina ya maajabu ya angani zinajitokeza kila wakati. Ishara za siku za mwisho zilizotabiriwa katika Biblia zimeonekana moja kwa moja, na majanga makubwa yameshuka. Kwa hivyo, tunapaswaje kumkaribisha Bwana na kupata wokovu wake? Bwana Yesu alisema, “Kondoo wangu huisikia sauti yangu, nami nawajua wao, nao hunifuata(Yohana 10:27). “Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati Yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, Atawaongoza hadi kwenye ukweli wote(Yohana 16:12-13). Imetabiriwa katika sehemu nyingi katika sura ya 2 na 3 ya Ufunuo: “Yeye ambaye ana sikio, na asikie vile Roho anaambia makanisa.” Kutoka kwa unabii huu, tunaweza kuona kwamba Mungu atazungumza maneno na kutekeleza hatua mpya ya kazi katika siku za mwisho na kutakasa na kuokoa watu, na kuwaleta watu katika ufalme wa Mungu. Ni kwa kusikiliza sauti ya Mungu tu, na kutamani na kutafuta kuonekana kwa Mungu na kazi ya siku za mwisho tunaweza kupokea kurudi kwa Bwana Yesu, kupata fursa ya kuokolewa na kukamilishwa na Mungu, na kuingia mahali pazuri na Mungu. Vinginevyo, tutapoteza wokovu wa Mungu, tutaanguka katika majanga makubwa ya siku za mwisho, na kuondolewa na kuadhibiwa. Hivi ndivyo Mungu anasema juu ya hilo:

Maafa yote yatatokea moja baada ya nyingine; mataifa yote na maeneo yote yatapitia maafa—tauni, njaa, mafuriko, ukame na matetemeko ya ardhi yatakuwa kila mahali. Maafa haya hayatokei tu sehemu moja au mbili, wala hayataisha kwa siku moja au mbili, lakini badala yake yataeneza juu ya eneo kubwa zaidi na zaidi, na maafa yatakuwa makali zaidi na zaidi. Wakati huu kila namna ya wadudu tauni watatokea kwa mfululizo, na tukio la watu kuwala watu litatokea kila mahali. Hii ni hukumu Yangu juu ya mataifa yote na watu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matamko ya Kristo Mwanzoni, Sura ya 65).

Katika upana mkubwa wa dunia hii, mabadiliko yasiyohesabika yamefanyika, bahari kujaa hadi kuziba mashamba, mashamba kufurika hadi baharini, tena na tena. Isipokuwa Yule ambaye anatawala kila kitu katika ulimwengu, Hakuna anayeweza kuongoza na kuelekeza jamii hii ya wanadamu. Hakuna yeyote hodari kufanya kazi au kufanya maandalizi kwa ajili ya jamii hii ya binadamu, sembuse yule anayeweza kuiongoza jamii hii ya wanadamu hadi hatima ya mwanga na kuikomboa kutokana na udhalimu wa duniani. Mungu hulalamikia wakati ujao wa wanadamu, huhuzunishwa na kuanguka kwa mwanadamu na anaumizwa kwamba binadamu wanatembea, hatua baada ya nyingine hadi kuoza na katika njia ambayo hawawezi kurudi. Wanadamu ambao wameuvunja moyo wa Mungu na wakamkana kumfuata yule mwovu: je, kuna yeyote ambaye amewahi kuwaza kuhusu mwelekeo ambao wanadamu wa aina hii huenda wanafuata? Ni kwa sababu hii haswa kwamba hakuna anayehisi hasira ya Mungu, hakuna anayetafuta njia ya kumpendeza Mungu au kujaribu kuja karibu na Mungu na isitoshe, hakuna anayetafuta kufahamu huzuni na maumivu ya Mungu. Hata baada ya kusikia sauti ya Mungu, binadamu anaendelea tu kwenye njia yake mwenyewe, anazidi kwenda mbali na Mungu, kukwepa neema na huduma ya Mungu, na kuepuka ukweli Wake, akiona heri kujiuza kwa Shetani, adui wa Mungu. Na ni nani amefikiri—iwapo mwanadamu ataendelea kuwa mkaidi—jinsi Mungu atakavyowatendea wanadamu hawa ambao wamempuuza bila kusita? Hakuna anayejua kwamba maana ya ukumbusho wa mara kwa mara na kusihi kwa Mungu ni kwa sababu Yeye anayo katika mikono yake maafa yasiyokuwa ya kawaida ambayo ameandaa, maafa ambayo yatakuwa magumu kwa mwili na nafsi ya mwanadamu kustahimili. Maafa haya siyo tu adhabu ya mwili bali pia ya roho. Unafaa kujua hili: Mpango wa Mungu utakaposhindikana na wakati makumbusho Yake na kusihi Kwake hakutapata majibu yoyote, atatoa hasira ya aina gani? Hii itakuwa kama kitu ambacho hakijawahi kushuhudiwa hapo awali au hata kusikika na viumbe vyovyote. Na hivyo Nasema, majanga haya hayana mengine ya kulinganishwa nalo awali na kamwe hayatawahi kurudiwa. Hii ni kwa sababu ni mpango wa Mungu kuumba wanadamu mara hii moja tu na kuwaokoa wanadamu mara hii moja tu. Hii ndiyo mara ya kwanza na pia ni ya mwisho. Kwa hivyo, hakuna anayeweza kuelewa nia za bidii na hamu ya ari ambazo kwazo Mungu huokoa wanadamu wakati huu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu).

Kazi ya Mungu ni kama mawimbi yanayotapakaa kwa nguvu. Hakuna anayeweza kumweka kizuizini, na hakuna anayeweza kusimamisha nyayo Zake. Wale tu wanaosikiza maneno Yake kwa makini, na wanaomtafuta na kuwa na kiu naye, wanaweza kufuata nyayo Zake na kupokea ahadi Zake. Wasiofanya hivyo watakabiliwa na maafa makuu na adhabu inayostahili(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 2: Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote).

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ishara 6 za kurudi kwa Bwana Yesu Zimeonekana

Miaka elfu mbili iliyopita, Bwana Yesu alituahidi: “Tazama, Naja upesi” (Ufunuo 22:12). Sasa, kila aina ya ishara za kurudi Kwake zimeonekana, na ndugu wengi wamekuwa na maono kwamba siku ya Bwana iko karibu. Je, Bwana tayari Amerudi? Je, tunaweza kufanya nini ili kumkaribisha Bwana? Hebu tujadili hili sasa kwa kuchunguza unabii ulio katika Biblia.

Je, Yesu Kristo Ni Mungu au Mwana wa Mungu?

Waumini wengi wanafikiria kwamba Bwana Yesu ni Mwana wa Mungu, lakini ufahamu huo unapatana na neno la Mungu? Je, Bwana Yesu kwa kweli ni Mwana wa Mungu au ni Mungu Mwenyewe? Endelea kusoma ili kujua.

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp