17 Mungu Yuko Kwenye Kiti cha Enzi

1

Msifu Mungu mwenye mwili ukizungumza maneno katika siku za mwisho.

Imba kwamba Amerudi na Enzi ya Ufalme.

Wateule wa Mungu wanainuliwa mbele Zake,

na sote tunasujudu kwa ibada kwa Mungu.

Mungu sasa Yuko kwenye kiti kitukufu cha enzi!

Jinsi gani Alivyo mtukufu na Anavyopendeza!

Mwenyezi, Yule aliyepo na aliyekuwepo, anatawala kama Mfalme duniani.

Yanauangaza ulimwengu wa giza, maneno ya Mungu, nuru ya kweli.

Watu wote watatii mbele za Mungu, wakaribishe ujio Wake.

Nyimbo zinazomsifu zinafika angani, Mungu yuko kwenye kiti cha enzi.

2

Maneno ya Mungu hutupa maji ya uzima.

Tunakula, kunywa maneno ya Mungu, ana kwa ana na Yeye,

na hatimaye tunahudhuria karamu.

Mungu hututenga na ulimwengu uliopotoka.

Kisha tunajiondolea minyororo ya ulimwengu,

na kuingia katika mafunzo ya ufalme.

Mwenyezi, Yule aliyepo na aliyekuwepo, anatawala kama Mfalme duniani.

Yanauangaza ulimwengu wa giza, maneno ya Mungu, nuru ya kweli.

Watu wote watatii mbele za Mungu, wakaribishe ujio Wake.

Nyimbo zinazomsifu zinafika angani, Mungu yuko kwenye kiti cha enzi.

3

Hukumu imeanza katika nyumba ya Mungu,

ikifichua utakatifu, haki ya Mungu.

Hukumu na kuadibu kwa maneno Yake

kunatutakasa na kutubadilisha kuwa watu wapya.

Mwenyezi Mungu hufuta machozi yetu,

ili tufurahie maisha ya ufalme milele.

Mwenyezi, Yule aliyepo na aliyekuwepo, anatawala kama Mfalme duniani.

Yanauangaza ulimwengu wa giza, maneno ya Mungu, nuru ya kweli.

Watu wote watatii mbele za Mungu, wakaribishe ujio Wake.

Nyimbo zinazomsifu zinafika angani, Mungu yuko kwenye kiti cha enzi.

4

Mungu ni mwenye busara na uweza katika kazi Yake,

akitumia joka kubwa jekundu kufanya huduma.

Maneno ya Mungu sasa yanatuonyesha uweza Wake,

yanashinda, yafanyiza kikundi cha washindi.

Mungu anatuongoza kuwa na ushuhuda katika dhiki.

Mungu amemshinda Shetani na kupata utukufu wote.

Mwenyezi, Yule aliyepo na aliyekuwepo, anatawala kama Mfalme duniani.

Yanauangaza ulimwengu wa giza, maneno ya Mungu, nuru ya kweli.

Watu wote watatii mbele za Mungu, wakaribishe ujio Wake.

Nyimbo zinazomsifu zinafika mbinguni, Mungu yuko kwenye kiti cha enzi.

Iliyotangulia: 16 Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Utukufu

Inayofuata: 18 Wito wa Tarumbeta ya Hukumu Umesikika

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp