Bwana Ameonekana Mashariki

06/01/2020

Na Qiu Zhen, China

Siku moja, dadangu mdogo alinipigia simu akisema kwamba alikuwa amerudi kutoka kaskazini na kwamba alikuwa na jambo muhimu la kuniambia. Aliniomba niende kwake mara moja. Nilikuwa na hisia kuwa jambo baya laweza kuwa limetokea, kwa hivyo nilienda nyumbani kwake mara moja. Ni wakati tu nilipofika nyumbani kwake na kumwona akisoma kitabu ndipo nilipoacha kuwa na wasiwasi. Dadangu aliniona nikiingia, akaruka na kusema kwa moyo mkunjufu, “Qiu Zhen! Wakati huu nikiwa kaskazini nilisikia habari njema: Bwana Yesu amerudi!”

Baada ya kusikia dadangu akisema hivi, nilifikiria nikiwa mwenye wasiwasi: “Katika miaka michache iliyopita kanisa la Umeme wa Mashariki limekuwa likishuhudia kwamba Bwana Yesu amerudi; Je, inawezekana kuwa dadangu amekubali Umeme wa Mashariki?” Kabla ya kuongea, dadangu alisema kwa uzito kabisa, “Ah, Qiu Zhen! Bwana amekuwa mwili tena naye Amekuja katika nchi yetu, China.” Nilisema kwa haraka, “Usiamini kila kitu unachosikia. Je, Mungu anaweza kuja China? Katika Biblia inasema waziwazi kabisa: ‘Na miguu yake itasimama siku hiyo juu ya mlima wa Mizeituni, ambao uko mbele ya Yerusalemu upande wa mashariki, na mlima wa Mizeituni utamamanuka katikati hapo kuelekea mashariki na kuelekea magharibi, na kutakuwa na bonde kubwa mno; na mlima nusu utajiondoa kuelekea kaskazini, na nusu yake kuelekea kusini(Zekaria 14:4). Kuja kwa Mungu kutakuwa katika Israeli. Hawezi kuja nchini China. Unamfanyia Bwana kazi na bado hata hujui jambo hili!”

Dadangu alisema kwa unyofu, “Nilikuwa nikifikiri jinsi unavyofikiri, lakini kupitia maneno ya Mwenyezi Mungu na ushirika wa ndugu, nimegundua kuwa kwa kweli Bwana amekuwa mwili nchini China. Andiko unalozungumzia ni unabii, lakini unabii hauwezi kufasiriwa jinsi tunavyotaka. Unatimizwa na kuonekana wazi kwa mwanadamu kupitia ukweli wa kazi ya Mungu. Bwana Yesu alipokuja kutekeleza kazi, Petro wala yule mwanamke Msamaria, wala towashi wa Uhabeshi hakufuata maana halisi ya unabii wa Biblia, lakini badala yake ilikuwa ni ukweli wa yale ambayo Bwana Yesu alisema na kazi ambayo Alitimiza ndivyo vilivyowathibitishia kwamba Masihi alikuwa Amekuja kama Bwana Yesu. Wote walizifuata nyayo za Mungu na kupokea wokovu wa Bwana. Na wale Mafarisayo ambao walishikilia maana halisi ya unabii wa Biblia wote walimchukulia Bwana Yesu, Masihi ambaye Alikuwa amekwisha kuja, kama mtu wa kawaida na kumkana, kumpinga na kumhukumu Bwana Yesu. Mwishowe walimsulibisha Bwana Yesu, na kwa hiyo waliadhibiwa na Mungu. Qiu Zhen, lazima tushughulikie kuja kwa Bwana kwa uangalifu na lazima tuwe na mioyo inayomcha Mungu. Kwa kweli usiwe mwenye haraka sana kuamua jambo hili!”

Nilimtazama dadangu na kuiinua Biblia na kusema, “Yehova Mungu aliitangaza sheria katika Israeli na Bwana Yesu alisulubiwa huko Israeli pia. China ni nchi inayotawaliwa na chama kisichoamini kuwa Mungu yupo, kwa hiyo Mungu angekuja katika nchi kama hiyo? Tumemwamini Bwana kwa miaka mingi sana, na hakika hatupaswi kuamini kila kitu tunachosikia!”

Dadangu alisema kwa wasiwasi, “Qiu Zhen, wakati Bwana Yesu alikuwa Akiitekeleza kazi Yake wakati huo, Mafarisayo walimpinga Bwana na kusema, ‘Tafuta, na utazame: maana hakuna nabii yeyote hutoka Galilaya’ (Yohana 7:52). ‘Je, Kristo atatoka Galilaya?’ (Yohana 7:41). Lakini kwa kweli, Bwana Yesu alilelewa katika Nazareti kule Galilaya. Biblia inasema: ‘O busara na maarifa ya Mungu ni makuu! Hukumu Zake haziwezi kuchunguzwa, na njia Zake haziwezi kutafutika! Kwa kuwa ni nani ameifahamu akili ya Bwana? Ama ni nani aliyemshauri?’ (Warumi 11:33-34). Je, tunawezaje kuielewa hekima ya Mungu? Hatuwezi kuichambua kazi ya Mungu kwa akili zetu wenyewe. Tunatazamia ujio wa Bwana kila siku. Sasa kwa kuwa Bwana amerudi kweli, ikiwa tutashikilia mawazo yetu wenyewe na tusitafute au kuchunguza, tutakosa nafasi ya kumkaribisha Bwana na tutajuta sana!”

Nilipomwona dadangu akionekana kuwa mwenye uzito sana, niliwaza: “Dadangu anamwamini Bwana kwa dhati naye ni mtu anayefikiria mwenye uwezo wa kuamua. Kwa kawaida yeye ni mwangalifu kuhusu kile anachofanya, na kwa shughuli kubwa kama kuja kwa Bwana, si rahisi kwake kuamini tu bila kufikiria kile mtu mwingine anachosema. Kwa sasa amekubali kanisa la Umeme wa Mashariki, kwa hiyo inawezekana kuwa ni kweli Bwana amerudi naye Anatekeleza kazi Yake nchini China?” Lakini wazo lingine likanijia: “Bwana angewezaje kutekeleza kazi Yake nchini China? Ni ajabu sana!” Kwa hivyo nikasema kwa uthabiti, “Biblia ni kama keki iliyo na rusu elfu, na njia ya kila mtu ya kuitafsiri ni tofauti. Biblia inatabiri kuwa kwa kweli Mungu atashuka katika Israeli katika siku za mwisho. Isitoshe, Wachina wengi wanaabudu Budha na serikali ya kitaifa daima imezitesa imani za kidini. Mungu hatakuja China kutekeleza kazi Yake!”

Dadangu alisema kwa hamu, “Qiu Zhen, Bwana amerudi na Amejitokeza nchini China ili kutekeleza kazi Yake. Hili ni jambo muhimu sana. Nimeikubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho hivi karibuni tu kwa hiyo bado siwezi kuelezea wazi ukweli huu, lakini ndugu wa Kanisa la Mwenyezi Mungu wanashuhudia kwa njia inayoangaza. Nitawaleta washiriki nawe!” Niliupunga mkono wangu na kusema, “Usijisumbue. Naondoka.” Baada ya kurudi nyumbani, nilikaa kwenye kochi bila kuonyesha hisia na kufikiria kuhusu kile dadangu alichokuwa amesema. Akili yangu ilikuwa ikiwaza sana nami sikuweza kutulia. Siku zote nilikuwa nimemngoja Bwana Yesu ashuke kwenye Mlima wa Mizeituni, kwa hivyo dadangu angewezaje kusema ghafla kuwa Bwana alikuwa amekuja China? Jambo hili lingewezekanaje? Nilipitia Biblia haraka haraka lakini sikuweza kupata sura au aya yoyote ambayo ilitabiri kwamba Bwana atakuja kutekeleza kazi Yake nchini China. “Bwana Yesu alipokuwa Akitekeleza kazi Yake wakati huo, Mafarisayo walimpinga Bwana na kusema: ‘Tafuta, na utazame: maana hakuna nabii yeyote hutoka Galilaya’ (Yohana 7:52). ‘Je, Kristo atatoka Galilaya?’ (Yohana 7:41). Lakini kwa kweli, Bwana Yesu alilelewa katika Nazareti kule Galilaya. …” Maneno ya dadangu yalinijia mara kwa mara akilini mwangu, nami nilifikiri kwamba kile alichosema kilikuwa kweli. Niligeuka kati ya hali ya kuipitia Biblia na hali ya kufikiri kuhusu kile alichokuwa amesema dadangu. Akili yangu ilikuwa ikifikiri sana nami sikujua ni nini kilicho bora kufanya, kwa hivyo nilimwomba tu Bwana moyoni mwangu, “Ee Bwana, nifanye nini? Ee Bwana, utashuka wapi hasa?”

Siku chache baadaye dadangu alinitafuta tena. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba alitabasamu na kusema, “Qiu Zhen, Dada Xie na Dada Hao kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu walikuja kwangu kunipa msaada. Wamemwamini Mwenyezi Mungu kwa muda mrefu na wanaelewa zaidi kuliko mimi. Ikiwa kuna jambo lolote ambalo huelewi kuhusu kurudi kwa Bwana, nenda ukashiriki nao.” Niliwaza: “Nimemwamini Bwana kwa miaka mingi nami daima nimetumainia kuja kwa Bwana. Bwana amekuja kweli? Labda napaswa kutumia fursa hii kushiriki nao.” Na kwa hiyo, nilienda na dadangu nyumbani kwake. Mara tu nilipoingia chumbani, dada hao wawili walinisalimia kwa ukunjufu sana na kuzungumza kwa upendo sana. Waliniambia nizungumze ikiwa nilikuwa na maswali yoyote, na kisha kila mtu angeshiriki kwa pamoja. Niliuliza, “Mnasema kwamba Bwana Yesu amesharudi naye Anatekeleza kazi Yake nchini China. Je, kuna sababu zozote za madai haya katika Biblia?” Dada Hao alitabasamu na kusema, “Dada, kweli kuna unabii katika Biblia kuhusu Bwana kuja kutekeleza kazi Yake nchini China katika siku za mwisho.” Nilishangaa na kusema, “Hii inawezekanaje? Nimepitia Biblia mara nyingi, lakini sijagundua kumbukumbu hata moja ya kibiblia kuhusu jambo hili. Ni wapi katika Bibia ambako kuna msingi wa madai yako?” Dada Hao alisema kwa uvumilivu, “Dada, hebu tusome aya mbili za maandiko nawe utajua. Katika Malaki 1:11 inasema: ‘Kwa kuwa kuanzia kuchomoka kwa jua hadi hata kutua kwake jina langu litakuwa kubwa miongoni mwa Mataifa; … akasema Yehova wa majeshi.’ Katika Mathayo 24:27 inasema: ‘Kwa kuwa kama umeme unavyotokea mashariki, na kumulika pia magharibi; ujio wa Mwana wa Adamu utakawa hivyo pia.’ Kutoka katika aya hizi mbili za Maandiko, tunaweza kuona wazi kuwa mahali ambapo Mungu atashuka tena ni Mashariki ya ulimwengu nayo iko katika nchi za mataifa. Sote tunajua kuwa China iko Mashariki ya dunia. Hatua zote mbili za kwanza za kazi ya Mungu zilikuwa katika Israeli. Kulingana na Israeli, China ni nchi ya mataifa. Kwa hiyo, Mungu kuja China ili kujitokeza na kutekeleza kazi Yake katika siku za mwisho inatimiza unabii huu.” Baada ya kusikiliza ushirika wa akina dada hao na kutafakari maana ya aya hizi mbili za Maandiko, niliuona ushirika wao ukiwa wenye kuangaza sana. Ingawa nilikuwa nimezisoma aya hizi mbili hapo awali, sikuwahi kuona maana ya kurudi kwa Bwana kukiwa Mashariki, nchini China. Nilipokuwa nikisikiliza maelezo yao, nilihisi kwamba ushirika wao ulikuwa na chimbuko lake katika kuelimisha kwa Roho Mtakatifu.

Dada Hao aliendelea kusema, “Hebu tuone kile anachosema Mwenyezi Mungu. ‘Kotekote katika ulimwengu Ninafanya kazi Yangu, na katika Mashariki, mashambulio ya radi yanapiga bila kukoma, yakiyatingisha mataifa yote na madhehebu. Ni sauti Yangu ndiyo imewaleta watu katika wakati wa sasa. Nitawasababisha watu wote kushindwa na sauti Yangu, kuingia katika mkondo huu, na kunyenyekea mbele Yangu, kwa maana Nilijirudishia utukufu Wangu kutoka duniani kote zamani na Nikautoa upya Mashariki. Ni nani asiyetamani kuuona utukufu Wangu? Ni nani asiyesubiri kwa hamu kurudi Kwangu? Ni nani asiye na kiu cha kuonekana Kwangu tena? Ni nani asiyetamani kuona kupendeza Kwangu? Ni nani hangetaka kuja kwenye nuru? Ni nani hangeuona utajiri wa Kanaani? Ni nani hangoji kwa hamu kurudi kwa Mkombozi? Ni nani asiyempenda kwa dhati Mwenyezi Mkuu? Sauti Yangu itaenea kotekote duniani; Ningependa, kuwazungumzia maneno mengi zaidi wateule wangu, Nikiwatazama. Kama radi yenye nguvu inayotingisha milima na mito, Nanena maneno Yangu kwa ulimwengu wote na kwa wanadamu. Hivyo maneno yaliyo kinywani Mwangu yamekuwa hazina ya mwanadamu, na watu wote wanayahifadhi maneno Yangu kwa upendo mkubwa. Umeme wa radi unaangaza kutoka Mashariki mpaka Magharibi. Maneno Yangu ni kiasi kwamba mwanadamu huchukia kuyaacha na pia huyaona kama yasiyoeleweka, lakini zaidi ya yote mwanadamu huyafurahia. Wanadamu wote wana uchangamfu na furaha, wakisherehekea kuja Kwangu, kana kwamba mtoto mchanga amezaliwa hivi karibuni. Kwa sauti Yangu, nitawaleta wanadamu wote mbele Yangu. Tangu hapo, Nitaingia rasmi katika jamii ya wanadamu ili waje kuniabudu. Kwa utukufu Ninaoutoa na maneno yaliyo kinywani Mwangu, Nitawafanya watu wote kuja mbele Yangu na kuona kwamba umeme unaangaza kutoka Mashariki na kwamba Mimi pia Nimeshuka kwenye “Mlima wa Mizeituni” wa Mashariki. Wataona kwamba Mimi tayari Nimekuwa duniani kwa muda mrefu, sio kama Mwana wa Wayahudi tena lakini kama Umeme wa Mashariki. Kwani Nimeshafufuka kitambo, na Nimeondoka miongoni mwa wanadamu, na kisha Nimeonekana tena miongoni mwa wanadamu Nikiwa na utukufu. Mimi ndiye Niliyeabudiwa enzi nyingi kabla ya wakati huu, na pia Mimi ni “mtoto mchanga” Aliyeachwa na Israeli enzi nyingi kabla ya wakati huu. Zaidi ya hayo, Mimi ndiye Mwenyezi Mungu mwenye utukufu wote wa enzi hii! Hebu wote waje mbele ya kiti Changu cha enzi ili waone uso Wangu mtukufu, wasikie sauti Yangu, na kuangalia matendo Yangu. Huu ndio ukamilifu wa mapenzi Yangu; ni mwisho na kilele cha mpango Wangu, na vilevile madhumuni ya usimamizi Wangu. Hebu kila taifa liniabudu Mimi, kila ulimi unikiri Mimi, kila mtu aniamini Mimi, na watu wote wawe chini Yangu!(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni). Sote tunajua kuwa Mungu aliileta injili ya ufalme wa mbinguni mara ya kwanza Alipokuwa mwili, na injili hii ilienea kutoka Magharibi hadi Mashariki. Lakini hatukuwahi kufikiri hata mara moja kuwa Mungu atarudi katika mwili upande wa Mashariki ya ulimwengu, nchini China, Akileta injili ya milele na kutekeleza kazi ya kuhukumu, kuwatakasa na kuwaokoa watu. Wakati huu kazi ya Mungu itaenea kutoka Mashariki hadi Magharibi—”

Niliposikia jambo hili, nilimkatiza yule dada na kumuuliza kwa mshangao, “Dada, Biblia inanukuu kuwa Yehova Mungu alitekeleza kazi Yake huko Israeli, na kazi ya Bwana Yesu ilikuwa huko Yudea. Hatua zote mbili za kazi ya Mungu zilikuwa katika Israeli, kwa hiyo kurudi kwa Bwana kunapaswa pia kuwa katika Israeli. Unawezaje kusema kuwa kuko nchini China?” Dada Hao alitabasamu na kusema, “Tunadhani kwamba kwa sababu hatua zote mbili za kwanza za kazi ya Mungu zilikuwa huko Israeli, hakika Bwana atatekeleza kazi Yake katika Israeli Atakaporudi. Lakini je, kufikiri kwa aina hiyo kunalingana na ukweli? Inawezekana kuwa Mungu ni Mungu wa Waisraeli tu? Hebu tuone kile ambacho Mwenyezi Mungu anasema.”

Dada Xie alifungua kitabu cha maneno ya Mungu na kusoma: “Mwokozi atakapofika katika siku za mwisho, kama bado angeitwa Yesu, na kuzaliwa mara nyingine katika Uyahudi, na kufanya kazi Yake katika Uyahudi, basi hii ingethibitisha kuwa Niliumba Wayahudi peke yao na kuwakomboa Wayahudi peke yao, na kuwa Sina uhusiano wowote na Mataifa. Je, hii haitakuwa kinyume cha maneno Yangu kwamba ‘Mimi ni Bwana aliyeumba mbingu na nchi na vitu vyote’? Nilitoka Uyahudi nami Nafanya kazi Yangu kati ya Mataifa kwa sababu Mimi si Mungu wa Wayahudi tu, ila Mungu wa viumbe vyote. Ninaonekana kati ya Mataifa katika siku za mwisho kwa sababu Mimi si Yehova, Mungu wa Wayahudi tu, lakini, zaidi ya hayo, kwa sababu Mimi ni Muumba wa wateule Wangu wote kati ya Mataifa. Sikuumba Uyahudi, Misri, na Lebanoni pekee, bali pia Niliumba Mataifa yote mbali na Israeli. Na kwa sababu hiyo, Mimi ni Bwana wa viumbe vyote. Nilitumia Uyahudi tu kama hatua ya kwanza ya kazi Yangu, Nikayatumia Uyahudi na Galilaya kama ngome za kazi Yangu ya ukombozi, nami Natumia Mataifa kama msingi ambao Nitatumia kuikamilisha enzi nzima(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya “Wingu Jeupe”). “Nitawafanya watu wote wajue kwamba Mimi siye tu Mungu wa Waisraeli, lakini Mimi ni Mungu wa Mataifa yote, hata mataifa yale Niliyoyalaani. Nitawafanya watu wote waone kwamba Mimi ndimi Mungu wa viumbe vyote. Hii ndiyo kazi Yangu kubwa zaidi, kusudio la mpango wa kazi Yangu katika siku za mwisho, na kazi ya pekee kutimizwa katika siku za mwisho(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi ya Kueneza Injili Ni Kazi ya Kuokoa Binadamu Pia). “Aliwaongoza Waisraeli na alizaliwa Yudea na vilevile amezaliwa katika nchi ya Mataifa. Je, kazi Yake yote haifanywi kwa ajili ya wanadamu wote Aliowaumba? Je, Anawapenda Waisraeli mara mia moja na kuwachukia Mataifa mara elfu moja? Je, hayo siyo mawazo yenu? Ni ninyi ambao hamtambui Mungu; si kwamba Mungu Hakuwa Mungu wenu. Ni ninyi mnaomkataa Mungu; si kwamba Mungu hapendi kuwa Mungu wenu. Ni nani kati ya walioumbwa hayuko mikononi mwa mwenye Uweza? Kwa kuwashinda leo, je, lengo si kuwafanya mtambue kuwa Mungu ni Mungu wenu? Iwapo bado mnashikilia kuwa Mungu ni Mungu wa Waisraeli tu, na kuendelea kushikilia kuwa nyumba ya Daudi huko Israeli ni asili ya uzao wa Mungu na kuwa hakuna taifa tofauti na Israeli limewezeshwa ‘kumzaa’ Mungu, na hata zaidi kuwa hakuna familia ya Mataifa yenye uwezo wa kupokea kazi ya Yehova—ikiwa bado unafikiria hivi, je, haikufanyi kuwa mshikiliaji wa ukaidi? … Hujaamini katika Mungu kwa muda mrefu, ilhali una mawazo mengi kuhusu Mungu, kiasi kwamba unathubutu kutofikiri hata kwa sekunde moja kuwa Mungu wa Waisraeli Anaweza kuwatunukia na uwepo wake. Wala hamthubutu kufikiri jinsi mnavyoweza kumwona Mungu Akijitokeza binafsi, ikitiliwa maanani jinsi mlivyo wachafu. Aidha hamjawahi kufikiri jinsi Mungu anavyoweza kushuka miongoni mwa Mataifa. Anapaswa kushuka juu ya Mlima Sinai au Mlima wa Mizeituni na kuonekana kwa Waisraeli. Je, si watu wa Mataifa (yaani watu wa nje ya Israeli) ndio walengwa wa chuki Yake? Anawezaje kufanya kazi miongoni mwao? Haya yote ni mawazo yaliyokita mizizi ndani yenu ambayo mmeyakuza kwa miaka mingi. Kusudi la kuwashinda leo ni kuyaharibu haya mawazo yenu. Kwa njia hiyo mmeweza kumwona Mungu akijionyesha Mwenyewe miongoni mwenu—si katika Mlima Sinai au Mlima wa Mizeituni, bali miongoni mwa watu ambao Hajawahi kuwaongoza hapo awali(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Ushindi (3)). “Kama kazi Yake ya sasa ingefanywa miongoni mwa Waisraeli, ikifika wakati ambao mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita kukamilika, kila mtu angeamini kuwa Mungu ni Mungu tu wa Waisraeli, kuwa Waisraeli tu ndio wateule wa Mungu, kuwa Waisraeli tu ndio wanaostahili kurithi baraka na ahadi za Mungu. Katika siku za mwisho, Mungu anapata mwili katika taifa lisilo la Kiyahudi la joka kubwa jekundu; Ametimiza kazi ya Mungu kama Mungu wa viumbe wote; Amekamilisha kazi Yake yote ya usimamizi, na Atamaliza sehemu kuu ya kazi Yake kwa taifa la joka kubwa jekundu. Kiini cha hatua hizi tatu za kazi ni wokovu wa mwanadamu—ambao ni, kufanya viumbe wote vimwabudu Bwana wa viumbe. Hivyo basi, kila hatua ya kazi hii ni muhimu sana; Mungu hatafanya chochote kisicho na maana ama thamani(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Ndiye Bwana wa Viumbe Vyote).

Kisha Dada Hao akashiriki, akisema, “Hapo zamani tuliamua mioyoni mwetu kuwa Mungu alikuwa Mungu wa Waisraeli kwa sababu hatua mbili za kwanza za kazi ya Mungu zilifanywa katika Israeli. Israeli ilikuwa mahali pa kuzaliwa kwa kazi ya Mungu na pia eneo la msingi kwa kazi ya Mungu, kwa hiyo tulidhani kwamba kazi ya Mungu inaweza kuwa katika Israeli tu, kwamba injili inaweza kutoka Israeli tu na kwamba ni Waisraeli pekee ambao ni watu wa Mungu wateule kwa kweli. Kwa hiyo, ikiwa Mungu bado Angeitekeleza hatua hii ya mwisho ya kazi Yake katika Israeli, basi tungeamini hata zaidi kwamba Mungu anaweza kufanya kazi Yake huko Israeli tu, kwamba Mungu angewabariki tu Waisraeli na kwamba Yeye hana uhusiano wowote na mataifa. Katika siku za mwisho, Mungu amechagua kutekeleza kazi Yake ya kuwahukumu na kuwatakasa watu katika nchi ya mataifa, ikiwa ni nchi ambako joka kubwa jekundu limelala likiwa limejikunja—China. Kwa kufanya hivi, Ameboresha maoni ya kila mtu, ili watu waweze kuona kwamba Mungu si Mungu wa Waisraeli tu, bali pia Mungu wa nchi zote za mataifa, na Mungu wa viumbe wote. Mungu hawabariki tu Waisraeli lakini pia huwabariki mataifa. Hii inafanikisha kazi ya ‘Mungu Ndiye Bwana wa Viumbe Vyote.’ Ni wazi kwamba Mungu kuchagua kufanya kazi Yake katika siku za mwisho nchini China ni muhimu sana. Kwa kweli Mungu ni mwenye kudura na mwenye busara sana.”

Nilipousikiliza ushirika wa dada huyo, nilizama katika kutafakari: “Ndiyo,” niliwaza, “Mungu ndiye Bwana wa viumbe vyote. Je, si wanadamu wote waliumbwa na Mungu? Mungu hawaokoi tu Waisraeli, lakini pia anawaokoa watu wa Uchina. Je, Mungu kuja kufanya kazi nchini China leo hakuonyeshi upendo Wake kwa mataifa? Inaonekana kwamba kwa kweli siyaelewi mapenzi ya Mungu!” Nilipofikiria kuhusu jambo hili, niliona aibu kwa kiasi fulani. Nilipunguza sauti yangu na kusema, “Dada, ninaelewa unachosema. Ikiwa Mungu angetekeleza kazi Yake katika Israeli tena, tungemwekea Mungu mipaka na kudhani kuwa Mungu ni Mungu wa Waisraeli tu. Mungu anafanya kazi kwa njia hii leo ili kuyaharibu mawazo ya watu na kuwafanya watu waelewe kuwa Mungu ndiye Bwana wa viumbe wote, kwamba Mungu anaweza kutekeleza kazi Yake huko Israeli na pia nchini China, na kwa hiyo ipasavyo tusiiwekee mipaka kazi ya Mungu. Inaonekana kwamba kwa kuiwekea mipaka kazi ya Mungu kulingana na mawazo na fikira zangu, kwa kweli nimekuwa mpumbavu na mjinga! Hata hivyo, bado kuna jambo moja ambalo sielewi. Kuna nchi nyingi sana ulimwenguni, kama vile nchi nyingi za Ulaya na Amerika ya Kaskazini, ambapo Uprotestanti na Ukatoliki ni dini za kitaifa na ambapo Mungu amekuwa akiabudiwa daima. Haingekuwa rahisi kwa Mungu kuja na kufanya kazi Yake ya kuhukumu na kuwatakasa watu katika nchi hizo? China ni nchi inayomkana Mungu, iliyojaa waabudu sanamu. Serikali ya kitaifa inawatesa kwa nguvu wale wanaomwamini Mungu, kwa hiyo mbona Mungu atekeleze kazi Yake nchini China?”

Dada Xie alitabasamu na kusema, “Dada, swali lako ni muhimu sana! Mbona Mungu alichagua kutekeleza kazi Yake ya hukumu na utakaso nchini China? Ni kwa kuelewa kusudi na umuhimu wa Mungu kutekeleza kazi Yake huko Israeli na Uchina tu ndipo tutafahamu kipengele hiki cha ukweli. Hebu tuangalie kile ambacho neno la Mungu linasema. Mwenyezi Mungu anasema: ‘Agano la Kale hurekodi maneno ya Yehova kwa Waisraeli na kazi Yake katika Israeli; Agano Jipya linarekodi kazi ya Yesu huko Uyahudi. Lakini kwa nini Biblia haina majina yoyote ya Kichina? Kwa sababu sehemu mbili za kwanza za kazi ya Mungu zilifanyika katika Israeli, kwa sababu watu wa Israeli walikuwa wateule—ambayo ni kusema kwamba wao walikuwa wa kwanza kukubali kazi ya Bwana. Walikuwa wenye upotovu wa chini zaidi ya wanadamu wote, na hapo mwanzo, walikuwa na nia ya kumtazamia Mungu na kumheshimu Yeye. Walitii maneno ya Bwana, na daima walitumika katika hekalu, na walivaa mavazi ya kikuhani au mataji. Walikuwa watu wa kwanza kabisa kuabudu Mungu, na chombo cha kwanza kabisa cha kazi yake. Watu hawa walikuwa kielelezo na mfano wa kuiga kwa wanadamu wote. Walikuwa kielelezo na mfano wa kuiga wa utakatifu na haki. Watu kama Ayubu, Ibrahim, Lutu, au Petro na Timotheo—wote walikuwa Waisraeli, na vielelezo na mifano mitakatifu zaidi ya watu wote. Israeli ilikuwa nchi ya kwanza ya kuabudu Mungu miongoni mwa wanadamu wote, na watu wengi wenye haki walitoka hapa kuliko mahali pengine popote. Mungu Alifanya kazi kati yao ili aweze kusimamia vizuri mwanadamu katika nchi zote na katika siku zijazo. Mafanikio yao na haki ya ibada yao ya Yehova yaliandikwa kwenye kumbukumbu, ili waweze kuhudumu kama vielelezo na mifano kwa watu waliokuwa nje ya Israeli wakati wa Enzi ya Neema; na matendo yao yamezingatia miaka elfu kadhaa ya kazi, mpaka hivi leo(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maono ya Kazi ya Mungu (2)). ‘Kazi ya Yehova ilikuwa uumbaji wa ulimwengu, ilikuwa mwanzo; awamu hii ya kazi ni mwisho wa kazi, na ni hitimisho. Hapo mwanzo, kazi ya Mungu ilifanyika miongoni mwa wateule wa Israeli, na ilikuwa mapambazuko ya kipindi kipya katika pahali patakatifu zaidi ya popote. Awamu ya mwisho ya kazi inafanywa katika nchi ambayo ni chafu zaidi ya zote, kuhukumu ulimwengu na kuleta enzi kwenye kikomo. Katika awamu ya kwanza kazi ya Mungu ilifanyika katika maeneo yenye kung’aa kuliko maeneo yote, na awamu ya mwisho inafanyika katika maeneo yaliyo katika giza kuliko maeneo yote, na giza hili litaondolewa, na mwanga kufunguliwa, na watu wote kushindwa. Wakati watu wa maeneo haya yaliyo chafu kuliko yote na yaliyo na giza watakuwa wameshindwa na idadi yote ya watu wametambua kuwa Mungu yupo, na ya kuwa ni Mungu wa kweli, na kila mtu Amemwamini kabisa, basi ukweli huu utatumika kutekeleza kazi ya ushindi katika ulimwengu mzima. Awamu hii ya kazi ni ya ishara: Punde tu kazi ya kipindi hiki itakapomalizika, kazi ya miaka 6,000 ya usimamizi itafikia mwisho kabisa. Mara baada ya wale walioko katika maeneo yaliyo na giza kuliko yote watakapokuwa wameshindwa, bila shaka itakuwa hivyo pia kila mahali pengine. Kwa hivyo, kazi ya ushindi tu katika China inabeba ishara ya maana. China inajumuisha nguvu zote za giza, na watu wa China wanawakilisha wale wote ambao ni wa mwili, wa Shetani, na wa mwili na damu. Ni watu wa China ndio wamepotoshwa sana na joka kubwa jekundu, ambao wana upinzani wenye nguvu dhidi ya Mungu, ambao wana ubinadamu ulio mbovu zaidi na ulio mchafu, na kwa hivyo hao ni umbo asili la wanadamu wote wenye matendo maovu. Hii si kusema kwamba nchi nyingine hazina shida kabisa; dhana za mwanadamu ni sawa zote, na ingawa watu wa nchi hizi wanaweza kuwa na uhodari mzuri, ikiwa hawamjui Mungu, basi ni lazima iwe kwamba wanampinga. Kwa nini Wayahudi pia walimpinga na kumwasi Mungu? Kwa nini Mafarisayo pia walimpinga? Kwa nini Yuda alimsaliti Yesu? Wakati huo, wengi wa wanafunzi hawakumjua Yesu. Kwa nini, baada ya Yesu kusulubiwa na kufufuliwa tena, watu bado hawakumwamini? Je, uasi wa mwanadamu sio sawa wote? Ni tu kwamba watu wa China wamefanyika mfano, na watakaposhindwa watakuwa mfano na kielelezo, na watatumika kama kumbukumbu kwa wengine. Kwa nini mimi daima Nimesema yakuwa nyinyi ni kiungo cha mpango wangu wa usimamizi? Ni katika watu wa China ambapo upotovu, uchafu, udhalimu, upinzani, na uasi unadhihirishwa kikamilifu zaidi na kufichuliwa kwa hali zao mbalimbali. Kwa upande mmoja, wao ni wa kimo cha umaskini, na kwa upande mwingine, maisha yao na mawazo yao ni ya nyuma kimaendeleo, na tabia zao, mazingira ya kijamii, familia ya kuzaliwa—yote ni ya umaskini na ya nyuma kimaendeleo kuliko yote. Hadhi yao, pia, ni ya chini. Kazi katika eneo hili ni ya ishara, na baada ya kazi hii ya majaribio hufanywa kwa ukamilifu wake, na kazi yake inayofuata itakwenda vizuri zaidi. Kama awamu hii ya kazi inaweza kukamilika, basi kazi inayofuata itakamilika bila shaka. Mara baada ya awamu ya kazi hii kutimizwa, na mafanikio makubwa kufikiwa kikamilifu, kazi ya ushindi katika ulimwengu mzima itakua imefikia kikomo kamili. Kwa kweli, mara baada ya kazi miongoni mwenu imekuwa ya mafanikio, hii itakuwa sawa na mafanikio katika ulimwengu mzima. Huu ndio umuhimu wa sababu Yangu kuwafanya mfano wa kuigwa na kielelezo. Uasi, upinzani, uchafu, udhalimu—yote haya hupatikana kwa watu hawa, na ndani yao pamewakilishwa uasi wote wa wanadamu. Wao ni wa kushangaza kweli. Hivyo, wanafanywa kuwa mfano wa ushindi, na punde tu watakaposhindwa watakuwa kama ilivyo kawaida kielelezo na mfano wa kuigwa na wengine(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maono ya Kazi ya Mungu (2)).”

Baada ya kuyasoma maneno ya Mungu, Dada Xie aliendelea na ushirika wake. “Maneno ya Mwenyezi Mungu yanatuambia wazi kuwa, kwa kila hatua ya kazi Yake, aina ya mahali na vyombo vya kazi Yake vyote vimechaguliwa kulingana na mahitaji ya kazi Yake, na kwamba vyote vina maana kubwa mno. Kwa mfano, hatua mbili za kwanza za kazi ya Mungu zilikuwa katika Israeli kwa sababu Waisraeli walikuwa watu wa Mungu wateule. Walikuwa watu waovu kwa kiasi kidogo zaidi kati ya wanadamu wote na walikuwa wenye mioyo ya kumcha Mungu. Akitekeleza kazi Yake kati yao, ilikuwa rahisi zaidi kwa Mungu kufanya kikundi cha mifano na vielelezo ili wamwabudu Yeye. Hivyo, kazi ya Mungu ingeweza kuenea kwa haraka na kwa urahisi zaidi, ili jamii nzima ya wanadamu iweze kujua kuhusu uwepo wa Mungu na kazi ya Mungu, na ili watu wengi zaidi waweze kuja mbele za Mungu na kuupokea wokovu wa Mungu. Kwa hiyo, lilikuwa jambo lenye maana zaidi kwa Mungu kufanya hatua mbili za kwanza za kazi Yake katika Israeli. Katika siku za mwisho, Mungu anatekeleza kazi ya kuwashinda na kuwatakasa watu. Pia Anahitaji baadhi ya wawakilishi waukubali ushindi na utakaso wa Mungu kwanza. Kati ya wanadamu wote, watu wa Uchina ndio waovu zaidi na wenye maendeleo kidogo mno, na China ndilo taifa ambalo linamwamini Mungu kidogo zaidi na linalotoa upinzani thabiti zaidi kwa Mungu. Katika siku za mwisho, kwa hivyo, kwa Mungu kutekeleza kazi Yake ya kuhukumu na kushinda kwanza nchini China, kwa kutekeleza kazi Yake ya kuadibu na hukumu juu ya wale ambao wamepotoshwa kwa kina zaidi, na kwa kuwashinda na kuwatakasa watu wa China ambao ndio walio wapotovu zaidi ulimwenguni, kudura, utakatifu na haki ya Mungu vinadhihirishwa vyema na Shetani anaaibishwa zaidi. Wale walio wapotovu zaidi wanaposhindwa na Mungu, ni wazi kwamba wanadamu wengine watashindwa na kwamba Shetani pia atashindwa kabisa. Kutoka mahali na walengwa wa kazi Yake vilivyochaguliwa na Mungu katika kila hatua ya kazi Yake, na kutoka kwa matokeo ya mwisho yaliyopatikana, tunaweza kuona bora zaidi kuwa kazi ya Mungu ni yenye busara na ya ajabu sana!”

Baada ya kusikiliza maneno ya Mungu Mwenyezi na ushirika wa akina dada hao, nilielewa: hapo awali Mungu alifanya kazi Yake huko Israeli kwa sababu Alitaka kufanya kikundi cha mifano na vielelezo miongoni mwa watu wapotovu kidogo zaidi kati ya wanadamu na, kupitia ushuhuda wao na kuhubiri kwa injili ya Mungu, kuwawezesha watu zaidi kupata wokovu Wake. Kazi ambayo Mungu anatekeleza katika siku za mwisho ni kazi ya kumshinda na kumtakasa mwanadamu, na Amewachagua watu wa Uchina, ambao ni wapotovu zaidi na waliotiwa unajisi zaidi ulimwenguni, kama walengwa wa kazi Yake, Akiwafanya watu hawa kuwa mifano na vielelezo ambao wameshindwa na kuokolewa. Huu ni ufichuzi hata zaidi wa hekima na uwezo wa Mungu. Sikuwahi kuyaelewa mapenzi ya Mungu na niliposoma katika Biblia kwamba Bwana atarudi kwa kushuka juu ya Mlima wa Mizeituni wa Israeli, nilikubali maana halisi nami nikafikiri kwamba hakika Mungu atatekeleza kazi Yake katika Israeli. Sikuwahi kutarajia kwamba Mungu angekuwa Ameshakuja nchini China! Ilionekana kuwa kazi ya Mungu haikuwa rahisi kama watu wanavyofikiria!

Wakati huo, Dada Xie aliendelea kusema, “Haijalishi ni katika nchi gani ambapo Mungu anatekeleza kazi Yake yote ni kwa ajili ya kazi Yake na kuokoa wanadamu bora zaidi, na yote yana maana kubwa. Ikiwa tunataka kutafuta kuonekana kwa Mungu leo, lazima kwanza tuweke kando fikira na mawazo yetu. Hatupaswi kuziwekea mipaka nyayo za Mungu ndani ya eneo fulani, tukifikiri kwamba Mungu anapaswa kuja katika nchi hii au ile. Mungu ni Mungu wa wanadamu wote. Anaweza kuchagua kwa hiari mahali pa kazi Yake kulingana na mahitaji ya kazi Yake. Mwenyezi Mungu anasema: ‘Mungu ni Mungu wa wanadamu wote. Hawi mali binafsi ya nchi au taifa lolote na hufanya kazi ya mpango Wake bila kuzuiwa na mfumo wowote, nchi au taifa. Labda hujawahi kuwazia mfumo huu, au labda wewe hukana kuwepo kwake, au labda nchi au taifa ambapo Mungu huonekana limebaguliwa na lina maendeleo duni sana duniani. Na bado Mungu ana busara Yake. Na uwezo Wake kupitia ukweli na tabia Zake kwa hakika Amepata kundi la watu wenye mawazo sawa na Yeye. Na Amepata kundi la watu ambao alitaka kutengeneza: kundi lililoshindwa Naye, watu ambao wameyavumilia majaribu machungu na aina zote za mateso na wanaweza kumfuata mpaka mwisho(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kiambatisho 1: Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya).”

Baada ya kusikia maneno ya Mwenyezi Mungu, nililia kwa shangwe na kuwaambia akina dada hao, “Maneno haya yana nguvu na mamlaka ya Mungu nayo yanatoka kwa Mungu. Sasa hatimaye ninaelewa: Mungu si Mungu wa Waisraeli tu, bali pia ni Mungu wa watu wa China na, hata zaidi, Yeye ni Mungu wa wanadamu wote. Kwa kweli Mungu amerudi! Siku hizi chache zilizopita, sijaweza kula au kulala vizuri kwa sababu niliogopa kuchukua njia mbaya! Kwa sababu ya kushiriki nanyi leo, uzito ulio moyoni mwangu umepotea. Namshukuru Mungu kwa kweli kwa kutoniacha!” Baadaye, dada hao wawili walinipa nakala ya Neno Laonekana katika Mwili, nami nilirudi nyumbani kwa furaha nikiwa nimekishikilia kitabu hicho kwa mikono yote miwili. Kupitia kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu, nilisadikishwa kuwa Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerejea. Bwana wetu Yesu amerudi!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Sauti Hii Yatoka Wapi?

Na Shiyin, ChinaNilizaliwa katika familia ya Kikristo, na jamaa wangu wengi ni wahubiri. Nilimwamini Bwana pamoja na wazazi wangu tangu...

Nimerudi Nyumbani

Na Chu Keen Pong, MalasiaNilimwamini Bwana kwa zaidi ya muongo mmoja na kuhudumu kanisani kwa miaka miwili, na kisha nikaliacha kanisa...

Nimekaribisha Kurudi Kwa Bwana

Na Chuanyang, Vereinigte StaatenMajira ya baridi kali ya mwaka wa 2010 huko Amerika yaliniacha nikihisi baridi sana. Kando na baridi kali...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp