Vurugu Kutoka kwa Uvumi wa “Mei 28” (Sehemu ya 1)

30/05/2021

Xingwu, Ufaransa

Yaliyomo
Mara ya Kwanza Nilipousikia Uvumi Huu Moyo Wangu Ulihuzunika
Kwa kudanganywa na Uvumi, Nilimkomesha Mamangu Kuliamini Umeme wa Mashariki
Uvumi Ulianguka Kutokana na Ukweli, na Kupitia Kuisikiza Sauti ya Mungu Nilirudi Mbele Yake Mungu

Mara ya Kwanza Nilipousikia Uvumi Huu Moyo Wangu Ulihuzunika

Mamangu ni Mkristo wa dhati. Tangu nilipokuwa mkubwa kutosha kuelewa mambo, angeniambia hadithi kumhusu Bwana Yesu mara nyingi, akiniambia kwamba Bwana Yesu ndiye Mungu wa kweli pekee. Nilipokuwa na umri wa miaka 13 nilienda na mamangu kanisani. Wakati huo nilifurahia kweli kusikiza mahubiri ya wachungaji, na nilikuwa na imani nyingi sana. Ningeshiriki kwa shauku katika kila ushirika. Lakini polepole niligundua kwamba hakukuwa na mwangaza katika mahubiri yaliyohubiriwa na wachungaji hao. Daima walirudia nadharia na maarifa fulani kuhusu Biblia au nadharia za kitheolojia, na muda ulivyoendelea kusonga sikupata raha hata kidogo kutokana na kusikiza mahubiri yao, wala sikuhisi kwamba nilikuwa nikipewa uhai. Kwa hiyo, nilianza kuenda katika ushirika mara chache na chache.

Baada ya kuhitimu, nilienda Ufaransa, na nikafikiria mwenyewe: “Hali katika makanisa ya ng’ambo hakika ni bora zaidi kuliko hali ya makanisa kule nyumbani.” Hivyo, nilianza mara moja kutafuta kanisa. Nilipoenda katika kanisa la Kichina, niligundua kwamba mahubiri waliyohubiri yalikuwa sawa kwa kweli na yale yaliyohubiriwa kule nyumbani, na hayakuwa na yoyote mapya ya kusema. Muda fulani baadaye kanisa liliwaalika wachungaji wengine kuhubiri mahubiri, lakini wao pia hawakuzungumza na mwangaza. Ili kulisisimua kanisa, wachungaji na wazee hata walipanga matembezi ya sisi waumini kwenda, wakitumia kutalii sehemu maarufu na burudani kusisimua shauku ya waumini, hivyo kuimarisha nguvu na umaarufu wao wa nje. Nilipoona kuwa hivi ndivyo kanisa lilivyokuwa, nilihisi kutoridhika sana, na kwa sababu ya kukosa chaguo bora yote niliyoweza kufanya ilikuwa ni kuliacha. Baada ya hili, dadangu mkubwa alinipeleka katika kanisa lingine, lakini lakushangaza ni kwamba hali katika kanisa hili lilikuwa mbaya hata zaidi. Waumini wote walikuwa waking’ang’ania umaarufu na mali. Ugomvi na vita vilizuka ndani ya kanisa hadi hatimaye polisi walilazimika kuvikomesha. Baada ya kushuhudia matukio haya sikuwahi kutaka kuenda kwa kanisa tena.

Siku moja, nilipokuwa nikiingia nyumbani mwa dadangu, alinikimbilia akisema: “Umesikia? Kuna Kanisa la Umeme wa Mashariki ambalo limetokea, na wanahubiri mahubiri ya juu sana, wakilenga “kuiba” kondoo wazuri kutoka kwa makanisa. Nimesikia kwamba kondoo wengi wazuri na wachungaji wao kutoka madhehebu na vikundi vyote wamelikubali Umeme wa Mashariki, na kwamba kila mahali wanaeneza neno na kushuhudia kurudi kwa Bwana Yesu. Hata nilisikia kwamba mara unapoanza kuliamini Umeme wa Mashariki, huwezi kutoka, kwamba ukitaka kutoka watatoa macho yako, kulikata pua yako na kukunyang’anya mali yako.” Dadangu alinionya tena na tena, akiniambia kwamba lazima niwe mwangalifu na kwamba lazima nijilinde dhidi ya Umeme wa Mashariki. Niliporudi nyumbani mume wangu pia alishiriki nami utangazaji hasi kuhusu Umeme wa Mashariki ambao alikuwa ameupata mtandaoni. Hasa kulikuwa na Kesi ya Mauaji ya Mei 28 katika McDonald huko Zhaoyuan, Shandong ambayo CCTV ilikuwa ikitolea ripoti. Baada ya kusikia kuhusu hili nilihisi kuogopa hata zaidi, na baada ya muda huo Umeme wa Mashariki lilikuwa limehuzunisha moyo wangu.

Kwa kudanganywa na Uvumi, Nilimkomesha Mamangu Kuliamini Umeme wa Mashariki

Jioni moja, kwa ghafla nilipokea simu kutoka kwa kakangu huko nyumbani akiniambia kwamba mama yetu aliliamini Umeme wa Mashariki. Nilishtuliwa na habari hii: Haliwezi kuwa kweli, laweza? Mama anawezaje kuliamini Umeme wa Mashariki? Nilifikiri kuhusu uvumi niliokuwa nimesikia, na nilikuwa na wasiwasi kwamba jambo lingemtokea mama. Kwa usiku kadhaa, niligaagaa na kugeukageuka, nisiweze kulala. Nilifikiri wenyewe: “Jambo hili si sawa! Lazima nimkomeshe mamangu, siwezi kumruhusu aliamini Umeme wa Mashariki.” Lakini kila nilipompigia mamangu simu na kumwambia kuhusu uvumi wa Umeme wa Mashariki uliokuwa mtandaoni, angekata simu mara moja. Sikuwa na njia ya kumshawishi. Baada ya hilo mimi na kaka yangu tulizungumzia jambo hili na kuamua kwamba angemfuata mama yetu na kumkomesha kuliamini Umeme wa Mashariki. Hata hivyo, haikujalisha alitumia mbinu gani, ilikuwa bure, mama yetu hakuyumbayumba hata kidogo katika imani yake. Tukiwa bila chaguo lingine, mimi na kaka na dada zangu tulizungumzia jambo hilo na kuamua tungemtisha mama yetu mara ya mwisho: Kama angeendelea kuliamini Umeme wa Mashariki basi tungemwacha. Tulishangaa kwamba alikuwa imara katika njia yake, na kusisitiza kuliamini Umeme wa Mashariki. Mnamo Machi 2017, mimi na dada yangu mkubwa tuliamua kurudi nyumbani na kumleta mama yetu Ufaransa, tukifikiri kwamba kama tungefanya hili tungemfanya aache kumwamini Mwenyezi Mungu. Lakini bila kutarajiwa, hakuwa tayari kukuja hata ingawa tulifanikiwa katika kuomba visa yake, basi mimi na dadangu tulikwea huku na kule kama paka juu ya paa la bati tukijaribu kuelewa kile tungetenda kumfanya mama yetu kutoka. Hatimaye, tulifikiria tegemeo la mwisho: Tungemdanganya mama yetu kuja Ufaransa kutenda imani yake katika Umeme wa Mashariki hapa. Tulishangaa wakati hila hii ilifanikiwa kweli, na mama yetu bila shaka aliikubali. Hata hivyo, alitufanya tukubali sharti moja. Nilifikiri mwenyewe: “Alimradi itamleta mama Ufaransa nitakubaliana na sharti kumi, sembuse moja.” Baadaye, niligundua kwamba sharti yake ilikuwa kwamba alitumai mimi na dadangu tungechunguza kazi ya Mungu katika siku za mwisho. Ili kumdanganya mama yetu kuja Ufaransa sikuwa na chaguo ila kujifanya kukubali hili, lakini nilifikiri mwenyewe: “Ha! Sitachunguza hilo asilani! Alimradi tumlete Ufaransa basi tutakuwa na mbinu ya kumkomesha.” Na hivyo mama yetu alikubali kuja na sisi Ufaransa kwa kuwa alidhani kwamba tulikuwa tumekubali ombi lake kwa kweli.

Mama yetu hakuwa amekaa Ufaransa wiki mmoja kabla ya kutuambia kwamba alikuwa amewasiliana na dada kutoka kwa kanisa na hata alikuwa amepanga muda kukutana uso kwa uso. Nilifikiri mwenyewe: “Kweli wanafanya mambo haraka. Tumewasili tu na wameshawasiliana, tufanye nini? Tumruhusu mama akutane nao kwa kweli au la? Tukimwambia hawezi kukutana nao hakika hatakubali hili; tukimwambia anaweza kuwaona basi hilo litavunja matumaini yetu ya kumkomesha kuliamini Umeme wa Mashariki.” Niliishia kuamua kwamba ningeenda pamoja na mama yangu, lakini nilishangaa nilipokutana na upinzani mkubwa kutoka kwa mume wangu, dada yangu na mume wake. Baada ya uamuzi wetu wa kutomruhusu mama kuenda kukutana nao, alisema kwa hasira: “Mbona mnasisitiza kuamini uongo uliobuniwa na CCP? CCP ni nini? Ni chama cha kisiasa kinachomkana Mungu, na tangu kiwe mamlakani kimekuwa kikiendelea kuwakandamiza na kuwapiga marufuku waumini wa dini, na kutaja Ukristo kuwa dhehebu ovu, kikiwakamata na kuwatesa Wakristo kila mahali, jambo ambalo limesababisha Wakristo wengi kukamatwa na kuteswa hadi kiwango ambacho wanaumia vibaya au hata kufa. Umesahau kuhusu ukweli huu wa kihistoria? CCP daima kimempinga Mungu na kimekuwa adui wa Mungu, kinachukia neno la Mungu na ukweli, kinachukia wale wanaomwamini Mungu wa kweli na kutembelea njia sahihi, na ili kuzuia watu kumwamini Mungu kinatenda kila aina ya uovu kama kuanzisha uvumi, kupaka tope majina ya watu na kuwasingizia na kuwanasa. Inaweza kuwa kwamba ninyi hata hamwezi kutambua hili? Inaweza kuwa kwamba mimi kama mama yenu angewatosa wana wangu wa kiume na kike katika shimo la moto? Nilikuja Ufaransa ili kuwafanya nyote mumwamini Mwenyezi Mungu hapa, mfuate kazi ya Mungu katika siku za mwisho, na kupokea fursa ya kupata wokovu kamili wa Mungu. Bwana Yesu alitabiri wakati mmoja kwamba Atarudi, na sasa Bwana Yesu amerudi, akija katika mwili kama Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu Amenena mamilioni ya maneno, na kwa msingi wa kazi ya ukombozi iliyotekelezwa na Bwana Yesu, Amekuwa akitekeleza kazi ya hukumu katika siku za mwisho akianzia nyumba ya Mungu, ili kututakasa kikamilifu na kutupata sisi sote ambao tumepotoshwa kwa kina na Shetani na kutuleta ndani ya ufalme wa mbinguni. Hii ni fursa nadra mno! Mbona mnasikiza uvumi tu bila kutafuta na kuchunguza kazi na neno la Mwenyezi Mungu? Je, imani yetu katika Bwana hii miaka mingi haijakuwa ili kukaribisha kurudi kwa Bwana? Msiponiruhusu kuenda kumwona dada huyu kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu basi ninunulieni tikiti ya ndege sasa, naenda nyumbani!” Kwa kumwona mamangu akiwa thabiti sana katika mtazamo wake na kumsikia akisema maneno ya ufahamu na umaizi kama hayo, sote tuliachwa bila cha kusema. Hata hivyo, bado hatukukubali. Hatukutaka kumpeleka mama yetu kuenda kumwona dada yule. Kwa siku kadhaa zilizofuata, bila kujali jinsi tulivyojaribu kumchangamsha mama yetu, bila kujali mahali tulipompeleka au kile tulichomnunulia, hakuonyesha shauku hata kidogo. Siku nzima alikuwa na huzuni sana kiasi kwamba hata hangekula chakula. Kuona kwamba mama yetu hakutaka kula au kunywa hivi kulinifanya kutotulia sana. Nilifikiri kuhusu jinsi mama yetu alivyotupenda tulipokuwa tukikua, jinsi alivyokasirika mbele yetu mara chache. Hii ilikuwa mara ya kwanza ambapo nilimwona mama yangu akiwa amekasirika sana na kusononeka sana, na ilinifanya mwenye huruma. Basi, nilizungumza jambo hili na dada zangu na kuwaambia kwamba wakati huu ningekabili bila woga “hatari” na kumpeleka mamangu kwenda kuwaona wale waumini wa Umeme wa Mashariki.

Uvumi Ulianguka Kutokana na Ukweli, na Kupitia Kuisikiza Sauti ya Mungu Nilirudi Mbele Yake Mungu

Vurugu Kutoka kwa Uvumi wa “Mei 28” (Sehemu ya 1)

Siku mbili baadaye dada wawili kutoka kwa Kanisa la Mwenyezi Mungu walikuja kwa duka letu jioni, na punde walipomwona mama yetu walisisimka sana na kuja na kumkumbatia. Ilikuwa ni kama kwamba walikuwa jamaa wa karibu waliokutana tena baada ya kutengana kwa miaka mingi. Walijaliana na kuheshimiana. Nilishtuka kuona hili, lakini sikuweza kujizuia kuguswa hisi na tukio hili la kutia huruma, na machozi yalianza kutiririka usoni mwangu bila kudhibitiwa. Mbona hivi? Ni vipi watu ambao hatukuwahi kukutana nao kabla waonekane sawa na washirika wakunjufu wa familia wakikusanyika? Niliona pia kwamba walikuwa na heshima sana katika usemi na tabia yao na wema na wakarimu katika jinsi walivyowatendea watu. Hawakuwa kama walivyodaiwa kuwa hata kidogo! Lakini tena nilifikiri mwenyewe: “Sawa, huenda hivi ndivyo wanavyoonekana kwa sasa, lakini siwezi kujiruhusu kudanganywa na wao. Lazima niendelee kuwachunguza.” Baada ya hili, nilianza kuwasiliana na ndugu kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu.

Baada ya kukutana nao mara kadhaa niligundua kwamba ndugu kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu walitaka tu kushiriki kuhusu ukweli nasi na kushiriki uzoefu na maarifa yao, hawakutudanganya kwa njia yoyote, wala kutudhuru. Kinyume chake, walitusaidia kwa ustahimilivu na upole sana kuelewa mikanganyo na magumu fulani katika kumwamini Mungu. Mwanzoni walimshuhudia Mwenyezi Mungu kuwa kuonekana kwa Bwana Yesu. Sikukubali hili moyoni mwangu, hivyo basi waliitumia Biblia kunielezea kwa ustahimilivu sababu ambazo dunia ya dini imekuwa ya ukiwa sana. Walinipa mfano, wakiniambia: “Mbona mwishoni mwa Enzi ya Sheria hekalu liligeuka kuwa pango la wezi ambapo pesa ilibadilishwa na mifugo na kuku kuuzwa? Sababu moja ya hili ilikuwa kwamba viongozi wa dini hawakufuata sheria na amri za Mungu, walikuwa wanatii tu kile kilichopitishwa na mwanadamu, na sheria, na walikuwa wakitenda matendo maovu, kumpinga Mungu na kukataliwa na Mungu; sababu nyingine ya hili ilikuwa kwamba kazi ya Roho Mtakatifu ilikuwa imeendelezwa mbele tayari, Mungu alikuwa amegeuka kuwa mwili tayari, Akitekeleza kazi ya Enzi ya Neema nje ya hekalu. Roho Mtakatifu hakuwa akitekeleza kazi katika hekalu tena, hekalu lilikuwa limegeuka kuwa la ukiwa. Kwa njia hiyo hiyo, kanisa leo pia ni lenye ukiwa kwa sababu wachungaji na wazee hawafuati njia ya Mungu, wanaenda dhidi ya amri za Mungu, wanaipinga kazi mpya ya Bwana kwa wayowayo, Mungu amewakataa kitambo, Roho Mtakatifu hatekelezi kazi miongoni mwao; wakati huo huo, pia ni kwa sababu Mungu anatekeleza kazi mpya katika siku za mwisho ndio amechukua tena kazi yote ya Roho Mtakatifu katika ulimwengu mzima na kuwapa wale wanaoifuata kazi Yake mpya. Watu hawa washapokea kazi ya Roho Mtakatifu kwa mara nyingine na kuingia katika mji wa “mvua”. Lakini wale ambao hawajapokea kazi mpya ya Mungu wataachwa katika mji ambapo hakuna “mvua,” na hapo watafifia. “Mvua” hii inahusu kazi ya Roho Mtakatifu, unahusu neno jipya la Mungu. Hili limekamilisha hasa kile kinachosemwa katika Kitabu cha Amosi 4:7: ‘Na pia nimeizuia mvua isije kwenu, ilipokuwa miezi mitatu kabla ya wakati wa mavuno: Na nimefanya kunyeshe katika mji mmoja, na kufanya kusinyeshe katika mji mwingine: kulinyesha katika sehemu moja, na sehemu ambayo haikunyesha ikanyauka.’”

Ushirika wao kweli ulilingana na Biblia, na ulilingana na neno la Bwana. Kile walichokisema kilikuwa cha maana sana, lakini kwa kuwa nilikuwa nimeshawishiwa sana na uvumi ulioenezwa na CCP na wachungaji na wazee katika dunia ya dini, bado nilitahadhari dhidi yao na kuwapinga moyoni mwangu. Nilifanya kila kitu ambacho ningeweza kutafuta kosa ambalo ningetumia kuwakanusha. Hata ingawa hivi ndivyo nilivyowatendea bado walishiriki kwa ustahimilivu sana nami, jambo ambalo lilinifanya nitambue mapenzi ya Mungu na kujua kazi ya Mungu. Baadaye dada hao pia walishiriki na mimi kuhusu ukweli wa hatua tatu za kazi za Mungu. Baada ya kusikia kuhusu hili nilishtuka, inavyoonekana Kristo wa siku za mwisho—Mwenyezi Mungu amefunua siri zote za mpango wa usimamizi wa Mungu wa miaka 6000 ili kuwaokoa wanadamu. Kazi ya Mungu katika Enzi ya Sheria ilikuwa kwamba Alitumia jina “Yehova” kuyaongoza maisha ya Waisraeli, na kumpitia Musa kutoa sheria alimfanya mwanadamu kuelewa dhambi zake; kazi ya Mungu katika Enzi ya Neema ilikuwa kwamba Alitumia jina “Yesu” kutekeleza kazi ya ukombozi, hatimaye akisulubiwa na kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya mwanadamu, hivyo kubeba dhambi zake na kumsamehe kwa ajili ya dhambi hizo; kazi ya Mungu katika Enzi ya Ufalme ni kwamba Anatumia jina “Mwenyezi Mungu” kutekeleza kazi ya kumhukumu na kumtakasa mwanadamu katika siku za mwisho. Mwenyezi Mungu ametoa maneno ili kumhukumu na kumwadibu mwanadamu, hivyo kumwondolea mwanadamu asili yake ya dhambi na kumruhusu mwanadamu kutakaswa na kupata wokovu wa Mungu, akimleta katika ufalme wa Mungu, na kuingia katika mbingu mpya na dunia mpya. Hatua tatu za kazi ya Mungu zinaunganishwa pamoja kwa ukaribu, zikiendelea kuwa kina hatua kwa hatua, zikikamilishana, hakuna hata moja yazo ambayo si ya lazima, ni kazi ya Mungu mmoja, na inakamilisha unabii katika Kitabu cha Ufunuo, ambapo kunasema: “Mimi ndiye Alfa na Omega, Mwanzo na tena mwisho, Akasema Bwana, ambaye yuko, na ambaye alikuweko, na ambaye atakuja, Mwenyezi(Ufunuo 1:8). “Imekwisha. Mimi ndiye Alfa na Omega, mwanzo na pia mwisho(Ufunuo 21:6). Wakati huo moyo wangu ulihisi kama ulikuwa ukizinduliwa, na nilihisi kusisimka sana. Hadi sasa nilikuwa tayari na imani katika Bwana kwa zaidi ya miaka ishirini, lakini bila kujali iwapo ilikuwa China Bara au ng’ambo sikuwa nimewahi kusikia awali mchungaji yeyote au mzee akihubiri mahubiri mazuri kama haya. Kuhusu mpango wa Mungu na unabii wa Biblia, zote ni siri, hakuna mtu anayejua, ilhali wale wanaoliamini Umeme wa Mashariki wanazungumza kwa wazi sana kuhusu mambo mengi sana, kama vile mpango wa Mungu wa kusimamia wanadamu, na hatua, kanuni, maelezo na athari za kutimizwa katika kila enzi ya kazi ya Mungu, na pia tabia inayoonyeshwa na Mungu, na matakwa ya Mungu na mapenzi kwa ajili ya wanadamu, kama kwamba wanahesabu mambo ya thamani ya familia yao. Nilihisi uthibitisho moyoni mwangu kwamba neno la Mwenyezi Mungu ni onyesho la Roho wa ukweli, kwamba kweli ni sauti ya Mungu. Bwana Yesu aliwahi kusema: “Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana hatazungumza juu yake mwenyewe; bali chochote atakachosikia, atakinena: na atawaonyesha mambo yajayo(Yohana 16:13). Sasa unabii huu wote umetimizwa na kukamilishwa kupitia Mwenyezi Mungu wa siku za mwisho kuonekana na kutekeleza kazi Yake! Mwenyezi Mungu ndiye kurudi kwa Bwana Yesu, na haya yote ni kazi iliyotekelezwa na huyo Mungu mmoja.

Baadaye pia nilisoma neno la Mwenyezi Mungu ambapo linasema: “Kristo wa siku za mwisho huleta uzima, na huleta kudumu kwa njia ya kweli na ya milele. Ukweli huu ni njia ambayo kwayo binadamu atapata uzima, na njia pekee ambayo mtu atamjua Mungu na kuidhinishwa na Mungu. Kama hutatafuta njia ya maisha inayotolewa na Kristo wa siku za mwisho, basi kamwe hutapata kibali cha Yesu, na kamwe hutastahili kuingia lango la ufalme wa mbinguni, maana wewe ni kikaragosi na mfungwa wa historia … Bila kuja kwa Mungu, je, unaweza kujichukua mwenyewe kwenda mbinguni kufurahia pamoja na familia ya Mungu? Je, wewe bado unaota sasa? Basi, Napendekeza sasa acha kuota, na kuangalia Anayefanya kazi sasa, na Anayefanya kazi ya kuwaokoa binadamu siku za mwisho. Kama huwezi, wewe kamwe hutapata ukweli, na kamwe hutapata uzima” (“Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele” katika Neno Laonekana katika Mwili). Neno la Mwenyezi Mungu limejaa mamlaka na uadhama wa Mungu, na linafichua tabia ya haki ya Mungu. Najua kwamba kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho ni inatekeleza kazi ya kuonyesha ukweli na kumpa mwanadamu uhai. Alimradi tumkubali Kristo wa siku za mwisho—Mwenyezi Mungu, na kukubali neno lililoonyeshwa na Mungu, basi hatimaye tutaweza kutatua chanzo cha dhambi zetu. Ni wakati huo tu ndio tutaweza kupata njia ya uzima wa milele. Na wale wasioweza kuwa sambamba na kazi ya Mungu, wasioukubali wokovu wa Mungu katika siku za mwisho hawatawahi kustahili kuingia katika ufalme wa mbinguni, na mwishowe wanaweza tu kuondolewa na Mungu, kuwasababisha kufa na kuangamizwa. Katika makabiliano na maneno ya Mungu ya hukumu, nilifikiri kuhusu jinsi nilikuwa mzembe sana hii miaka michache iliyopita katika jinsi nilivyouchukulia ukweli wa kurudi kwa Bwana, na sikuweza kujizuia kuhisi woga kiasi, na sikuthubutu tena kuendelea kuchukulia ukweli huu bila heshima hivi. Nilikumbuka pia hali ambapo nilielewana na ndugu kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu na kuona kwamba waliishi kwa kudhihirisha kiasi maneno ya Mungu: Haijalishi ni masuala gani niliyoyaibua, daima walikuwa wastahimilivu sana katika kunipa jibu kwa kutumia neno la Mwenyezi Mungu, hawangekoma hadi nilipoelewa; wakati mwingine dada wangekuja kwa duka langu, na kwa sababu duka lilikuwa dogo na halikuwa na nafasi ya kutosha ya wao kuketi, wangesimama kwa saa kadhaa, na hata wangeleta chakula chao kujilisha; wakati mwingine, ili kutoathiri biashara yangu, wangesubiri hadi usiku nilipokuwa nimemaliza biashara yangu ili kukutana nami na kushiriki kuhusu ukweli na mkutano wetu ulipokuwa umeisha ilikuwa saa sita usiku tayari waliporudi nyumbani. Wakati mmoja kulikuwa na dada wawili walioshiriki nami usiku wa manane sana na hakukuwa na garimoshi la wao kurudi nyumbani, kwa hivyo walikaa usiku huo katika kituo cha treni ya chini kwa chini. Niliona hawa ndugu wakivumilia taabu kama hizi na kuwa wenye upole na wastahimilivu, na sikuweza kujizuia kufikiria kile Biblia inasema: “Mtawajua kupitia matunda yao. Je, wanadamu hukusanya zabibu za miiba, au matini ya mibaruti? Hata zaidi kila mti mzuri hutoa matunda mazuri; lakini mti mbaya hutoa matunda mabaya. Mti mzuri hauwezi kutoa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kutoa matunda mazuri(Math 7:16-18). Tangu nilipowasiliana na ndugu hawa kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu, niliona kwamba waliishi kwa njia ambayo ilipendeza sana, kwamba waliweka katika vitendo amri mbili kuu ambazo Bwana Yesu anawataka wanadamu watende: “Wewe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako mzima, na roho yako nzima, na akili yako nzima. Hii ni amri ya kwanza na kubwa. Na ya pili ni kama hiyo, Wewe mpende jirani yako kama unavyojipenda(Mathayo 22:37-39). Singethubutu kusema kwamba tayari walikuwa wamefikia matakwa ya Bwana, lakini niliona kwamba walikuwa wakiishi kwa kudhihirisha sehemu ya uhalisi wa amri hizi mbili. Na wakati hili lililinganishwa na jinsi ndugu walivyoishi kwa kudhihirisha hili kutoka madhehebu na vikundi mbalimbali, yalikuwa tofauti kabisa kama mbingu na ardhi, ndugu hawa hawakuishi kwa kudhihirisha hata kiasi kidogo cha msamaha na ustahamilivu, na walijaa wivu na ugomvi, na kupigana na kupambana wao kwa wao, kiasi kwamba wangepigana kwa ajili ya umaarufu na faida na hadhi ndani ya kanisa, na kuhusu walikuwa wa mti wa aina gani, ingeweza kujulikana kulingana na aina ya tunda walilozaa. Lakini nilihisi udhibitisho moyoni mwangu kwa njia ambayo ndugu kutoka Kanisa la Mwenyezi Mungu waliishi, jinsi walivyoishi haikuwa ya uongo, ilikuwa onyesho la maisha yao baada ya kutenda maneno ya Mungu. Kwa sababu walizifuata nyayo za Mwanakondoo, walikuwa na kazi ya Roho Mtakatifu, na walikuwa na neno la Mungu kama uzima wao, waliweza kuishi kwa kudhihirisha mfano wa Mkristo wa kweli anayeleta utukufu kwa Mungu na kumshuhudia Mungu. Wakati huu, chini ya uongozi wa neno la Mungu na majibu ya mapigo kwa ukweli huu, uvumi huu kuhusu Umeme wa Mashariki ulianguka polepole moyoni mwangu.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Umeme wa Mashariki Unatoka Wapi?

Sasa tuko katika siku za mwisho, unabii wa kurudi kwa Bwana umetimizwa kimsingi, na waumini wengi sana wanaomcha Mungu wanatumai kurudi kwa...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp