Kuwa Mtu Mwaminifu Ni Kuzuri Kweli!

19/05/2021

Wu Ming, Uchina

Siku moja mnamo mwaka wa 2004 rafiki mmoja aliniambia: “Kila siku unarauka mapema na unashughulika siku nzima ukikata nguo, unajichosha kabisa, ilhali bado hutengenezi pesa. Jamii ya leo inategemea ulimi kutengeneza pesa, kama msemo maarufu unavyosema: ‘Ni heri kuwa na ulimi mjanja kuliko kuwa na mikono na miguu yenye nguvu.’ Unajua kwamba sasa najihusisha katika biashara ya mauzo ya moja kwa moja nikiuza bidhaa za vipodozi, biashara hiyo hainifanyi kuwa mrembo tu, pia sihitaji kutumia juhudi nyingi sana kila siku, nahitaji tu kuzungumza maneno machache na wateja wangu na kuuza bidhaa zangu ili kutengeneza pesa nyingi sana. Mbona usibadili kazi na uje uuze bidhaa za vipodozi nami? Nilimtazama rafiki yangu juu chini, kweli alikuwa anapendeza kuliko awali, na kisha nikafikiri kuhusu jinsi nilivyokuwa mshonaji magauni kwa zaidi ya miaka 10, jinsi ambavyo kweli sikuwa nimetengeneza pesa nyingi katika kazi hiyo, na jinsi ambavyo sikuwa nazidi kuwa kijana. Kama kweli ilikuwa jinsi ambavyo rafiki yangu alikuwa akisema, ikiwa kubadili kazi kuendea ile ambayo ningeuza bidhaa za vipodozi ningetengeneza pesa kwa urahisi, na hata kuzidi kuwa kijana na kuwa wa kupendeza zaidi na kupata sifa kubwa za wengine, basi hilo lingekuwa bora zaidi! Nilipokuwa nikifikiri hili, nilimweleza papo hapo kwamba nilikuwa tayari kuungana na kampuni. Baadaye, baada ya uchunguzi wangu, niliagiza bidhaa za thamani ya zaidi ya yuan 3,000, na nikaanza kazi yangu katika tasnia ya vipodozi kama mshauri wa urembo wa kampuni hii.

Mfanyakazi mwenzangu aliniambia kwamba baada ya kugeuka kuwa mshauri wa urembo, kama tunaweza kukuza washauri wengine wa urembo kati ya 8 na 12 basi tunaweza kupandishwa cheo kufanya kazi kama wauzaji. Lakini iwapo tunataka kuwa wauzaji basi lazima tuwe na wateja zaidi wanaoagiza bidhaa kama sharti la utendaji mzuri. Baada ya hili, nilianza kupiga bongo nikifikiri njia ya kuzidisha utendaji wangu. Nilipata ushauri kutoka kwa watu wengine, na kuchunguza mbinu za elimu ya soko; nikawaalika wateja kwenye duka letu mara kwa mara kujaribu bidhaa zetu, na kuwashawishi kununua bidhaa nilizowaonyesha; nilipokuwa na wakati ningefanya mazoezi ya kuzungumza mbele ya kioo ili kuongeza kiwango cha usemi niliotumia kujieleza, ili kwamba niweze kuathiriana na wateja kwa njia bora zaidi. Kupitia kazi yangu ya bidii ya kila wakati niliwapata wateja zaidi polepole. Ili kuimarisha msingi wa wateja, ilinibidi niwe kasi moja na shughuli za kukuza mauzo katika kampuni na kupiga simu ili kuwaalika wateja kuhudhuria warsha zetu, mahali ambapo wangepitia ufanisi wa bidhaa zetu wao wenyewe na wakati huo huo ningeweza kutambulisha bidhaa za kampuni na mfumo wetu wa zawadi, kukuza mauzo, n.k., na hivyo kuwavutia wateja. Mara nyingi ningezungumza kila wakati kwa zaidi ya saa moja, nisikome hadi wateja waliporidhika vya kutosha na kununua bidhaa hizo. Kuziangalia zile pesa mikononi mwangu ambazo nilikuwa nimepata kwa urahisi sana kulinifanya nihisi furaha sana: Kutegemea mdomo wangu kutengeneza pesa kweli kulikuwa kwa juhudi ya chini zaidi kuliko kutengeneza pesa katika kazi yangu aminifu ya mikono ya awali, na nikaelewa kwamba alimradi ningeendelea kufanya kazi kwa bidii, basi kugeuka kuwa mwuzaji kulikuwa karibu nami.

Wakati mmoja msichana aliyekuwa na chunusi usoni mwake alikuja katika duka, na nikafikiria mwenyewe: Hii ni fursa, nahitaji kumfanya msichana huyu aone haja ya kuonekana mrembo na kumpendekezea bidhaa fulani za faida ya juu. Kwa njia hii sitaweza kutengeneza pesa nyingi tu, lakini pia naweza kumgeuza kuwa mteja wa muda mrefu, na wakati muda uko sawa nitamfanya aniletee wateja zaidi, jambo ambalo basi litaongeza wingi wa mauzo yangu ya bidhaa, hivyo kiasili kuongeza utendaji wangu. Niliona kwamba chunusi usoni mwake hazikuwa mbaya vile, lakini ili kupata faida za juu, nilisema kwa sauti iliyotiwa chumvi: “Ee! Tusipotibu chunusi usoni mwako sasa hivi basi zitakuwa za kina zaidi katika ngozi yako na kuiharibu, na basi hakutakuwa na bidhaa zitakazoweza kuiponya, jambo ambalo pia litaathiri ngozi kwenye uso wako katika siku zijazo. Linaweza kuwa baya zaidi kiasi kwamba uso wako utajawa uvimbe na kujazwa na majipu. Hili halitaathiri sura yako tu, bali pia litakuwa na athari kwa mustakabali wako, hilo litakuwa shida!” Msichana huyo aliposikia hili, aliogopa kabisa na akataka nimpe bidhaa zozote ambazo zingeweza kumsaidia mara moja. Kwa hivyo nilitenda bila kuchelewa. Nikichukua bidhaa kiasi mara moja ili kumwonyesha, na akaishia kuondoka na bidhaa za thamani ya zaidi ya yuan 1,000. Nilijiwazia: Inaonekana kwamba ikiwa nataka kutengeneza pesa siwezi kuwa mwaminifu vile, na kwamba lazima nichukue udhaifu wa mteja na kuutia chumvi kwa msingi wa mapendeleo yake wenyewe, kwa sababu hilo ndilo linalohitajika kumfanya atake kununua bidhaa zetu. Baada ya hilo, nilijifunza jinsi ya kutumia mbinu tofauti kwa wateja wa aina tofauti ili kuuza bidhaa zetu, na kama matokeo utendaji wangu katika kampuni ukaongezeka zaidi na zaidi.

Nilifanya kazi kwa bidii kwa miaka minne, hatimaye kupandishwa cheo hadi kiwango cha mwuzaji, lakini haikuwa rahisi kushikilia cheo hiki. Kulingana na kanuni zisizoandikwa za kampuni hiyo: Utendaji wetu umewekwa kwa msingi wa maagizo pekee. Kadiri utendaji wetu ulivyo wa juu zaidi, ndivyo mishahara yetu ilivyo ya juu zaidi, na kadiri cheo chetu kilivyo cha juu zaidi, ndivyo tutapata zawadi zaidi. Ili kufikia malengo haya na kufikia utendaji wetu kama wauzaji, tulitumia mbinu ya zawadi ili kuwatia moyo washauri wa urembo kuagiza bidhaa. Wakati mwingine ambapo washauri wa urembo hawakuagiza bidhaa, ilibidi tutumie pesa zetu wenyewe kununua bidhaa ili tuweze kupita katika utendaji wetu. Hili lingefanya bidhaa zetu nyingi kuwekwa kupita uwezo wa kuziuza, na baada ya muda mrefu wa kutonunuliwa, bidhaa hizi zingepita tarehe ya kutumika. Ili kudumisha utendaji wetu, tungepunguza bei ya bidhaa hizi ambazo zilikuwa karibu kupita tarehe ya kutumika kuuzia wateja wetu. Wakati mmoja, mfanyakazi mwenza alimwuzia mteja bidhaa ambayo ilikuwa karibu kupita tarehe ya kutumika, na baadaye uso wa mteja huyo ukageuka kuwa mwekundu, kama ua linalochanua. Hili lilimkasirisha mteja huyo naye akaja kumtafuta mfanyakazi mwenza ili amsababishie shida, ambaye aliogopa sana kiasi kwamba hakujua la kufanya. Baada ya kuzungumzia hilo, aliishia kumfidia mteja huyo, jambo ambalo hatimaye lilihitimisha majaribu hayo. Wakati hili lilipotokea, nilifikiri kuhusu jinsi ambavyo kila mwezi, ili kufikia utendaji wangu, mimi pia niliuza bidhaa zilizojaa ambazo zilikuwa karibu kupita tarehe ya kutumika, na jinsi ambavyo bidhaa hizi zilizokuwa karibu kupita tarehe ya kutumika hazikuwa na dhamana za kampuni. Kwa hivyo, iwapo kwa bahati mbaya mteja angepata shida ya ngozi baada ya kutumia mojawapo ya bidhaa hizi na aje kunitafuta akitaka kusajili kesi, ningefanya nini? Jambo hili lilinifanya kuhisi kutotulia zaidi na zaidi, lilinifanya kuogopa kiasi kwamba moyo wangu ulianza kupiga kwa kasi, na nikajiambia kwamba kuanzia sasa na kuendelea singeuza tena bidhaa ambazo zilikuwa karibu kupita tarehe ya kutumika. Lakini nilifikiri kulihusu zaidi: Nisipouza bidhaa mpaka ziishe basi utendaji wangu hautapita, na basi sitakuwa na sifa zinazostahili kuwa mwuzaji, na kabla ya mimi kujua nitashushwa cheo kuwa mshauri wa urembo wa kawaida. Hili lingemaanisha kwamba ndoto niliyokuwa nikifanyia kazi kwa muda mrefu sana ya kuwa tajiri ingekuwa tu ndoto ya mchana, na hiyo kazi yote ngumu niliyokuwa nimefanya kwa miaka mingi ingekuwa bure! Nilipokuwa nikifikiri kuhusu siku za nyuma na mustakabali niligundua kwamba ili kuhifadhi sifa zangu za kuwa mwuzaji basi singeweza kubadilika sana. Kama wengine wangeweza kulifanya mbona isiwe mimi? Kwa hivyo, niliendelea kusonga mbele na kanuni hii isiyoandikwa ya biashara.

Kuwa Mtu Mwaminifu Ni Kuzuri Kweli!

Katika mwaka wa 2012 rafiki yangu mmoja alinifanya nimwamini Mwenyezi Mungu, na tangu wakati huo nimesoma neno la Mungu mara kwa mara, nimesali kwa Mungu na kushiriki pamoja na ndugu. Wakati wa ushirika, ndugu wote huzungumza wazi kutoka moyoni, wakijadili kile wanachojua na kile wamepitia kutoka kwa neno la Mungu, na kweli nafurahia kuwasikiza. Siku moja, nilisoma neno la Mungu linalosema: “Mnastahili kujua kwamba Mungu hupenda binadamu mwaminifu. Mungu ana kiini cha uaminifu, na kwa hivyo neno Lake siku zote linaweza kuaminika. Aidha, matendo Yake hayana dosari wala hayajadiliwi. Hii ndiyo maana Mungu anawapenda wale walio waaminifu kabisa Kwake” (“Maonyo Matatu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kupitia maneno ya Mungu niligundua kwamba Mungu ni mwaminifu na kwamba Anawapenda watu waaminifu. Mungu pia anatuagiza sote tuwe watu waaminifu, tusiseme uongo, tusiwadanganye wengine. Nilifikiri kuhusu maneno yote ya uongo niliyokuwa nimetumia kila siku kuwadanganya wateja nilipoendesha biashara yangu na kujaribu kupata faida, ambayo nilipata kwa kudanganya imani ya wateja wangu. Nilikuwa nimetumia mbinu za udanganyifu kutengeneza pesa. Haya yote yalikuwa maonyesho ya udanganyifu. Iwapo ningeendelea kwa njia hii, Mungu angewezaje kunipenda? Sasa kwa kuwa namwamini Mungu lazima niwe kama ndugu zangu na kufanya mazoezi ya kuwa mtu mwaminifu na kuzungumza ukweli. Hivi ndivyo jinsi nitakavyoweza kumfanya Mungu afurahi na kupata idhini Yake.

Lakini katika maisha halisi, nilipokabiliwa na faida, kufanya mazoezi ya kuwa mtu mwaminifu hakukuwa rahisi kama nilivyokuwa nimefikiri kungekuwa. Siku moja mteja alikuja kwangu na orodha ya bidhaa za vipodozi za thamani ya yuan 7,000 ambazo alikuwa akizitaka. Niliiangalia orodha hiyo na kuona kwamba hatukuwa na bidhaa zote alizozitaka katika duka letu, kwa hivyo nilifikiri nilichopaswa kufanya. Je, nimwambie ukweli, au ... nilihisi vita vikali vikisukasuka moyoni mwangu: Sasa namwamini Mungu, kusema uongo hakukubaliani na mapenzi ya Mungu, siwezi kuendelea kuwadanganya watu kama nilivyofanya awali; lakini nikimwambia mteja huyu ukweli basi bila shaka sitaweza kufanya mauzo naye wakati huu, na labda hatarudi wakati ujao, na hivyo sitakuwa na fursa tena ya kutengeneza pesa kutoka kwake. Lo, kusema uongo hakukubaliani na mapenzi ya Mungu, lakini kutosema uongo ni sawa na kuacha zaidi ya yuan 2,000 ambazo zilikuwa karibu kuangukia mikononi mwangu, ambalo, kama wafanyakazi wenza wangegundua, hakika wangenicheka. Kwa hivyo, ni heri nilifanye wakati huu, na kisha wakati ujao sitalifanya. Kwa hivyo nilimwendea mteja na kusema: “Mimi ni mtaalamu wa utunzaji wa ngozi, ukichukua ushauri wangu na kutumia bidhaa nitakazopendekeza basi nakuhakikishia kwamba ngozi yako itakuwa nzuri zaidi.” Nilitegemea kujua kuongea kwangu, nilizungumza na mteja huyo kwa zaidi ya saa moja hadi hatimaye alikuwa tayari kununua bidhaa ambazo nilikuwa nimependekeza. Kwa hivyo nilikusanya pamoja mkusanyiko wakubahatisha wa bidhaa za kiwango cha juu za thamani ya yuan 7,000. Baada ya yeye kuondoka nilizitazama pesa mikononi mwangu lakini sikuhisi furaha hata kidogo. Nilihisi aibu sana kwa sababu sikuwa nimetenda kuwa mtu mwaminifu kama anavyohitaji Mungu. Baada ya siku kadhaa mteja alinipigia simu pasipo kutarajiwa akitaka kurudisha zile bidhaa. Alisema hakuhisi kutulia kutumia zile bidhaa nilizokuwa nimemwekea pamoja. Nilijaribu kila kitu ili niweze kumshawishi, lakini akili yake haingeweza kubadilishwa. Baada ya tukio hili, mteja mmoja baada ya mwingine alitaka kurudisha bidhaa zake. Wakati mfululizo huu wa matukio ya bahati mbaya ukinifikia, nilianza kufikiria mambo: Ili kujifaidisha nimetumia maneno ya uongo daima kuwadanganya wateja kununua bidhaa. Hili halikubaliani na mapenzi ya Mungu, lakini nililifanya ili kushikilia sifa zangu za mwuzaji. Licha ya kujua ukweli kikamilifu niliuasi kwa makusudi na kuendelea kutumia mbinu za udanganyifu kufanya biashara yangu. Mungu ni safi na mtakatifu, angewezaje kuniruhusu kusema jambo moja na kufanya lingine? Matukio haya ambayo yamenifikia karibuni, kwa yote, wa kumlaumu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nikivuna nilichokipanda. Huku kulikuwa kushughulikiwa na kufundishwa nidhamu na Mungu, na ilikuwa Mungu kuniokoa mimi. Lakini, na faida zikiwa mbele yangu, sikuelewa kwa nini nilitaka kutenda kulingana na neno la Mungu lakini sikuweza kufanya hivyo. Nilichoweza tu kufanya ilikuwa ni kusali na kutafuta mbele ya Mungu.

Baadaye niliona katika neno la Mungu ambapo linasema: “Wakati mwanadamu amechafuliwa na kudanganywa huku, ni sawa na mtu ambaye anahusika na kamari na kisha anakuwa mchezaji kamari. Katika kutoelewa, anapenda tabia yake ya kudanganya na anaikubali. Katika hali yako ya kutoelewa, unakubali udanganyifu. Katika hali yako ya kutoelewa unachukua udanganyifu kuwa tabia halali ya kibiashara, na unachukua kudanganya kuwa mbinu ya manufaa zaidi ya kusalimika kwako na riziki yako; unafikiria kwamba kwa kufanya hivi anaweza kutengeneza mali nyingi haraka. Huu ni mchakato: Mwanzoni mwa mchakato huu watu hawawezi kukubali tabia ya aina hii, wanadharau tabia hii na njia hii ya kufanya mambo, kisha wanajaribu tabia hii wao wenyewe, na kuijaribu kwa njia yao wenyewe, na kisha mioyo yao inaanza kubadilika polepole. Kwa hivyo mabadiliko haya ni yapi? Ni kukubali na kukiri mwenendo huu, kukiri na kukubali wazo hili lililoingizwa kwako na mwenendo wa jamii. Kwa kutojua, unahisi kwamba usipodanganya watu katika kufanya biashara nao, unahisi umebaki nyuma sana; usipodanganya watu unahisi kuwa umepoteza kitu. Bila kujua, kudanganya huku kunakuwa nafsi yako, tegemeo kuu kwako, na kunakuwa aina ya tabia ya lazima ambayo ni kanunimaishani mwako. Baada ya mwanadamu kukubali tabia hii na kufikiria huku, je, moyo wa mwanadamu unapitia mabadiliko? Moyo wako umebadilika, basi uadilifu wako umebadilika? Ubinadamu wako umebadilika? Dhamiri yako imebadilika? (Ndiyo.) Uwepo wote wa mwanadamu unapitia mabadiliko bora, kutoka kwa mioyo yao hadi kwa mawazo yao, hadi kwa kiwango ambapo wanabadilika kutoka ndani hadi nje. Mabadiliko haya yanakuweka mbali na mbali zaidi kutoka kwa Mungu, na unapatana zaidi na zaidi na Shetani, unakuwa sawa zaidi na zaidi na yeye” (“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalifichua fumbo moyoni mwangu. Nilielewa kwamba faida zangu zikiwa mbele yangu, singeweza kuweka maneno ya Mungu katika vitendo, singeweza kuishi kama aina ya mtu mwaminifu ambaye Mungu anamhitaji, na sababu ilikuwa kwamba nilikuwa nimeharibiwa sana na mienendo miovu katika jamii na nilikuwa nimetegemea sumu ya Shetani kuishi. “Mbingu huwaangamiza wale ambao hawajiwakilishi.” “Mtu hufa kwa ajili ya fedha; ndege hufa kwa ajili ya chakula.” “Kwa vile akili ndogo haimfanyi mtu kuwa muungwana, mwanamume mwenye thamani hakosi sumu.” Sumu za Shetani kama hizi zilikuwa zimekita mizizi sana ndani yangu, jambo ambalo lilinisababisha nisiweze kutenda ukweli licha ya kuufahamu kikamilifu na kupoteza hisia yangu ya asili ya mema na mabaya linapokuja suala la kuwa mtu wa kawaida, lililonifanya niwe mbali zaidi na zaidi na Mungu. Nilifikiri kuhusu jinsi nilivyokuwa nimefuata mwenendo wa jamii wa kuweka pesa juu ya kila kitu kingine bila kufikiri, na jinsi nilivyofikiri kwamba kuwa mwaminifu na tayari kufanya kazi kwa bidii hakukuwa kuzuri kama kutumia mbinu za udanganyifu kutengeneza pesa haraka, jambo ambalo lilinifanya kubadili kazi na kuuza bidhaa za vipodozi ambapo kuanzia mwanzo nilifuata falsafa ya maisha ya Shetani kwa njia ambapo “Ni heri kuwa na ulimi mjanja kuliko kuwa na mikono na miguu yenye nguvu.” Nilipokuwa nikiendesha biashara yangu nilitegemea kujua kwangu kuongea, daima nikitumia maneno ya uongo kuwadanganya wateja, nikisema chochote ambacho kingehitajika kufikia malengo yangu. Nilijiambia kwamba tendo hili la udanganyifu lilikuwa la kawaida, kwamba kila mtu alilifanya, kwamba ningekuwa na upungufu kama singelifanya, jambo ambalo lilinisababisha kupuuza dhamiri yangu ikiniambia kile ambacho ningepaswa kufanya na kutotenda ukweli hata ingawa niliufahamu. Ilikuwa dhahiri kwamba sumu mbalimbali ambazo Shetani alikuwa ameziweka ndani yangu zilikuwa zimekita mizizi sana ndani yangu kabisa na kuwa maisha yangu. Moyoni mwangu kila kitu nilichotaka kukifanya kilikuwa kwa ajili ya manufaa yangu mwenyewe, alimradi kitu kilihusisha kuninufaisha moja kwa moja basi nilianza kuasi dhamiri yangu na ukweli na kuwaambia watu uongo. Matendo haya yote na mienendo kweli vilimfanya Mungu kunichukia sana, na ilikuwa wazi kuona kwamba kanuni za Shetani za kuendelea kuishi zilikuwa zinapinga ukweli moja kwa moja, zilipinga ukweli, na zilimpinga Mungu. Mungu alizindua aina hii ya mazingira ili kunishughulikia na kunifundisha nidhamu ili kwamba niweze kubadili tabia yangu potovu, niondoe njia zangu za kudanganya na kusema uongo, niweze kuishi kama mwanadamu mwaminifu, na nisitegemee kanuni za Shetani tena za kusalia ili kuishi. Aliamsha moyo wangu uliokuwa umetia ganzi na kuniwezesha kuona wazi sura yangu mbaya ya kupotoshwa na Shetani. Alinifanya niweze kujidharau na kurudi mbele Yake. Mungu kweli ni mwenye haki na mtakatifu! Mungu ni mwaminifu. Mungu anawapenda watu waaminifu, na Anawabariki watu waaminifu. Ni kwa kufuatilia kuwa mtu mwaminifu tu ndipo tunaweza kupata wokovu wa Mungu. Punde nilipozielewa nia za Mungu nilisali Kwake kufanya azimio: Kuanzia sasa na kuendelea singesema uongo tena ili kuwadanganya watu, na singefanya mambo yaliyoasi dhamiri yangu tena.

Siku moja mteja alipiga simu akisema kwamba alitaka kasha la bidhaa za VC la thamani ya zaidi ya yuan 900, na nilimwambia aje dukani kulichukua. Haikuwa hadi alipofika ambapo niligundua kwamba hatukuwa na bidhaa hizo ambazo alikuwa akizitaka dukani, lakini niliahidi kwamba kama angesubiri siku kadhaa ningezipata bidhaa hizo na kumtumia. Baada ya siku chache alipiga simu tena kuulizia bidhaa hizo na nikajiwazia: Mteja anapouliza kuhusu bidhaa daima nilikuwa nikimuuzia zile ambazo zilikuwa karibu kupita tarehe ya kutumika, lakini sasa siwezi kusema uongo tena kuwadanganya watu. Lakini tena nikajiwazia: Kama siwezi kumtumia bidhaa hizi haraka basi kuna uwezekano sana kwamba nitampoteza mteja, na vile vile pesa! Kwa hivyo nifanye nini? Kutuma bidhaa ambazo zilikuwa karibu kupita tarehe ya kutumika kungekuwa kudanganya, na Mungu hatakuwa na furaha. Baada ya kusita kwa muda nilisali kwa Mungu nikimwomba mwongozo, kunifanya niweze kutenda ukweli, na kunifanya nisiseme uongo tena kwa wateja. Baada ya kusali nilifikiri kuhusu neno la Mungu ambapo linasema: “Mnastahili kujua kwamba Mungu hupenda binadamu mwaminifu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maonyo Matatu). “Katika yote unayofanya na yote unayosema, uweze kuuweka moyo wako uwe sawa na uwe mwenye haki katika matendo yako, na usiongozwe na hisia zako, wala kutenda kulingana na mapenzi yako mwenyewe. Hizi ni kanuni ambazowaumini katika Mungu wanapaswa kutenda” (“Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje?” katika Neno Laonekana katika Mwili).

Kuwa Mtu Mwaminifu Ni Kuzuri Kweli!

Chini ya mwangaza na mwongozo wa maneno ya Mungu nilipata kuelewa matakwa ya Mungu. Anatumai kwamba naweza kutenda ukweli na naweza kuwa mtu mwaminifu, ambayo ni kanuni ninayopaswa kudumisha ninapotenda. Ninaweza kumhisi Mungu kando yangu akichunguza kila mwenendo wangu, na wakati huu sitamsikitisha Mungu tena, ni lazima nimwambie mteja huyu ukweli. Kwa hivyo, nilimpigia mteja simu: “Bidhaa za VC ambazo ulikuwa umeulizia hazijafika bado, ikiwa unazihitaji sasa hivi nina kasha la VC nyumbani ambalo liko karibu kupita tarehe ya kutumika, naweza kukupa hilo kwa bei iliyopunguzwa. Ikiwa unazitaka, kesho unaweza kuja dukani ili uziangalie.” Siku iliyofuata mteja alikuja kuziangalia zile bidhaa, na akazichukua bila kusema neno lingine. Kwa kuwa nilikuwa nimeusaliti mwili wangu na kusema ukweli nilihisi utulivu sana na uhuru kutoka kwa wasiwasi moyoni mwangu. Baada ya kupitia tukio hili nilihisi kuguswa sana moyoni mwangu. Niliona kwamba alimradi nilitenda kulingana na neno la Mungu, nizungumze na wateja kwa ukweli kulingana na mambo ya hakika, na kutenda kama mtu mwaminifu basi kweli ningeweza kuwa na furaha. Ni hapo tu ambapo ningeweza kupata uhuru na ukombozi wa kweli! Shukrani Kwake Mungu!

Baada ya hili nilisoma neno la Mungu ambapo linasema: “Kutenda kama mwanadamu wa kawaida ni kuzungumza kwa kueleweka. Ndiyo inamaanisha ndiyo, na la inamaanisha la. Kuwa mwenye ukweli kwa uhakika na uzungumze inavyofaa. Usilaghai, usidanganye” (“Kuboresha Ubora wa Tabia ni Kwa Ajili ya Kupokea Wokovu wa Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Pia nilisoma ushirika kutoka kwa juu, ambao ulisema: “Kutenda kama mtu mwaminifu kuna kanuni tatu: Moja, lazima uwe mtu wa kweli; mbili, usikimbilie hila; tatu, usiwe mdanganyifu. Ukifanya vitu hivi vitatu basi utakuwa mtu mwaminifu. Kuwa mtu wa kweli ni kuwa mnyoofu na mwaminifu na kusema kwa uaminifu na kutenda kwa kweli, ambapo moja ni moja na mbili ni mbili” (Mahubiri na Ushirika Kutoka kwa Juu). Neno la Mungu na ushirika wa mwanadamu yalinionyesha njia ya jinsi ya kuwa mtu mwaminifu. Bila kujali iwapo ni katika maisha yetu ya kila siku au maisha ya kazi au tunaposhirikiana na watu wengine, tunahitaji kusema tunachokimaanisha daima na kufikiri na kutenda kama mtu wa aina hiyo, kutowadanganya wengine, kutosema uongo, na kuacha moja iwe moja na mbili iwe mbili. Haya ndiyo mambo ambayo Mungu anataka watu walio na ubinadamu wa kawaida wawe nayo. Kwa hivyo nilifanya azimio papo hapo, kuanzia hapo kuendelea, bila kujali iwapo ningekuwa mbele ya ndugu au wateja wangu, ningeishi kwa kutegemea neno la Mungu, kutenda kuwa mtu mnyoofu na mwaminifu na kukubali uchunguzi wa Mungu.

Siku moja nilikutana na mteja na akaniambia: “Bi Wu, ngozi yangu imeparara sana, bidhaa ambazo nimekuwa nikitumia kwa muda hazijabadili chochote. Nilisikia kwamba bidhaa unazoweka pamoja ni bora zaidi katika kuboresha ngozi. Tafadhali, unaweza kunipa seti ya bidhaa za hali ya juu? Pesa siyo hoja.” Nilipomsikia akisema hili nilijiwazia: Seti ya bidhaa za hali ya juu za bei ya kati ya yuan 4,000 mpaka 5,000 zinaweza kunipa faida ya zaidi ya yuan 1,000, lakini nikiweka pamoja seti ya bidhaa zinazofaa ngozi yake itagharimu tu yuan 1,000 na kitu, na nitapata faida ya yuan 400 pekee. Wakati tu ambapo sikujua ni chaguo gani napaswa kufanya nilifikiri kuhusu neno la Mungu ambapo linasema: “Unaweza kumridhisha Mungu leo, iwapo uko makini na masuala madogo, unamridhisha Mungu kwa mambo yote, una moyo unaompenda Mungu kwa dhati, unampa Mungu moyo wa dhati, na japokuwa kuna baadhi ya mambo ambayo huwezi kuelewa, unaweza kwenda mbele za Mungu kurekebisha motisha zako, na kuyafuata mapenzi ya Mungu, na kufanya kila lipaswalo kumridhisha Mungu” (“Kumpenda Mungu tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli” katika Neno Laonekana katika Mwili) “Mimi ni mwenye haki, Mimi ni mwaminifu, Mimi ndimi Mungu anayechunguza moyo wa ndani zaidi wa mwanadamu! Nitafichua mara moja aliye wa kweli na aliye wa uongo” (“Sura ya 44” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili). Ni kweli! Mungu ni Mungu mwenye haki na mwaminifu, pia Yeye ni Mungu anayechunguza moyo wa ndani kabisa wa mwanadamu. Ni lazima nitende kulingana na mapenzi ya Mungu, siwezi kufanya vitu vinavyofedhehesha jina la Mungu tena ili kulinda maslahi yangu mwenyewe. Kwa hivyo, nilimwambia: “Bidhaa za hali ya juu hazifai ngozi yako. Zitaiongezea mzigo mkubwa zaidi. Seti ambayo itafaa ngozi yako zaidi ambayo ningependekeza ni zaidi kidogo ya yuan 1,000. Itaanza kurekebisha ngozi yako kutoka kwenye msingi, jambo ambalo litafanya ngozi yako kuwa bora polepole.” Baada ya kutenda kwa njia hii, akili yangu ilihisi yenye utulivu zaidi. Mteja huyo aliniambia: “Bi Wu, wewe ni mtu mzuri sana, kile unachokisema ni cha uaminifu sana. Nitawatambulisha wateja wengine kuja kutumia bidhaa zako.” Nilitabasamu, nikisema: “Sio kwamba mimi ni mtu mzuri, ni kwamba tu tunapaswa kutenda kama watu waaminifu. Ni hapo tu ndipo tutakuwa na utulivu wa akili.” Kabla ya muda mrefu mteja huyo alirudi kuzichukua bidhaa, na pia aliwaleta baadhi ya marafiki zake kuwatambulisha kwangu, na nikawawekea pamoja bidhaa ambazo zilifaa ngozi zao. Polepole lakini kwa hakika, wateja wengi zaidi waliniamini zaidi na zaidi. Wote walileta pesa kwangu wakinitaka kuwaagizia bidhaa. Kwa hivyo, hakukuwa na shinikizo ya mimi kutafuta fedha ili kufanya biashara hizi. Kwa njia hii nilitenda kama mtu mwaminifu, yule ambaye kweli alitenda kulingana na matakwa ya Mungu, na biashara ikawa bora zaidi na zaidi. Nilijua kwamba hii ilikuwa baraka ya Mungu. Mungu hakunipa vitu yakinifu tu. Muhimu zaidi pia Alinifundisha jinsi ya kutenda. Katika dunia halisi kweli ni vizuri kutenda kama mtu mwaminifu kulingana na neno la Mungu!

Nilikumbuka siku zangu za nyuma, jinsi nilivyofuata mienendo miovu ya Shetani kwa ajili ya maslahi yangu binafsi na kufuatilia falsafa ya maisha ya Shetani kwa njia ambapo “Ni heri kuwa na ulimi mjanja kuliko kuwa na mikono na miguu yenye nguvu.” Nilifikiri kwamba singeweza kufanya mambo bila kusema uongo, kwamba bila kusema uongo singeweza kutengeneza pesa nyingi, na kama matokeo nilichezewa na Shetani hadi sikuishi kama mwanadamu ama mnyama! Nilikuwa nimebadilika zaidi na zaidi kuwa mtu bila ubinadamu, mtu bila dhamiri na bila mantiki. Nilikuwa nimepoteza uadilifu na heshima ambayo mtu anapaswa kuwa nayo anapotenda. Mungu hakuridhika. Sikuwa wa kuaminika kama mtu. Kila siku nilikuwa nikitenda kama mwizi, nikiwa na hofu kwamba siku yoyote ningepatwa na shida na kuingizwa kwenye kesi na mtu. Maisha yangu yalikuwa yenye kuhitaji nguvu nyingi na ya kuchosha sana. Lakini Mungu alijua kwamba nilikuwa nimepotoshwa sana na Shetani, na ili kuniokoa Aliniweka katika mazingira ambayo yangenifundisha nidhamu, na maneno ya kuniongoza na kunielekeza, ili kwamba ningeweza kuona kwa wazi ubaya wa upotovu wangu mwenyewe, ili kwamba niweze kujidharau na kumgeukia Yeye, na kutenda ukweli kama mtu mwaminifu. Nilipotenda kulingana na maneno ya Mungu, nilipotenda kama mtu mwaminifu, nilipofanya wajibu wangu nilipokuwa nikiendesha biashara yangu, nilipokea mwongozo na baraka ya Mungu. Katika uzoefu huu niliona kwamba ilikuwa ni nia ya Mungu kuniokoa na kuniongoza hadi kwa njia sahihi ya maisha, ambapo singeendelea kuchezewa na Shetani. Ninashukuru kwa dhati kwa ajili ya aina hii ya upendo na wokovu wa aina hii ambao Mungu amenipa. Kutoka hapa na kuendelea, bila shaka nitatenda kama mtu mwaminifu kulingana na neno la Mungu, niishi kama mtu wa kweli ili kumridhisha Mungu na kumshuhudia Mungu!

Inayofuata: Hili Jaribu Langu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Pambano la Kuwa Mtu Mwaminifu

Mwenyezi Mungu anasema, “Ufalme Wangu unawahitaji wale ambao ni waaminifu, wasio wanafiki, na wasio wadanganyifu. Je, si watu wenye moyo...

Kupima kwa Sura Ni Upuuzi Tu

Yifan Jiji la Shangqiu, Mkoa wa Henan Katika siku za nyuma, mimi mara nyingi niliwapima watu kwa sura zao, nikiwachukua watu wachangamfu,...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp